Oct 5, 2016

CHADEMA Wanakaribia Kuiua CUF Bara Kama Walivyofanya kwa NCCR

Wadau, amani iwe kwenu.

Kadri siku zinavyoenda tunazidi kuona mengi na inadhihirika rasmi kuwa UKAWA ulijengwa kwa msingi wa matofali ya barafu. Baada ya uchaguzi wa 2015, tumeshuhudia chama cha NCCR Mageuzi kikisambaratika kwa kupoteza wabunge wote wa Mkoa wa Kigoma. NCCR wakajikuta wanabaki na mbunge mmoja tu ambaye ni Mwenyekiti wake Francis Mbatia aliyeshinda jimbo la vunjo kwa mgongo wa CHADEMA.

Baada ya uchaguzi huo, tumeshuhudia CUF wakijiimarisha Tanzania Bara kwa kushinda viti kadhaa vya wabunge. Pia wameshinda viti vya udiwani. Hii ni tofauti na uchaguzi wa 2010. Hali hii haijawafurahisha CHADEMA hata kidogo. Kuimarika kwa CUF maana yake ni kudhoofika kwa CHADEMA hasa katika maeneo ya Mikoa ya Mwambao.

Ili kukabiliana na nguvu ya CUF, CHADEMA wametumia mbinu za DIVIDE AND RULE. Wamefanikiwa kuigawa CUF vipande viwili. Kwa upande wa Tanzania Bara, Julius Mtatiro ndiye anayetumiwa na CHADEMA kuwaua CUF. . Kwa upande wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na watu walio karibu naye wapo mikononi mwa CHADEMA.

Inadaiwa kuwa wafadhili wa CHADEMA ambao ni Taasisi ya KAS ya Ujerumani inawapa fedha viongozi hao na inagharamia shughuli zote za chama kutokana na uamuzi wao wa kususia uchaguzi mkuu wa marudio hali iliyosababisha wapoteze wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Maalim Seif kutokuwa Makamu wa Kwanza wa Rais. Inadaiwa kuwa taasisi hiyo ya KAS ndiyo iliyogharamia safari za viongozi wa CUF Jumuiya ya Ulaya na Marekani.

Tukumbuke kuwa CHADEMA ilifanya hila ili CUF isifanikiwe kupata Meya kwenye Halmashauri walizoshinda. Hayo yametokea KInondoni na Temeke.
Kinachoshangaza zaidi ni kwamba CUF hawajashtuka. Wapo viongozi wachache kama akina Magdalena Sakaya ambao wanaona jahazi linazama. Wanajaribu kufurukuta lakini hawaoni mwelekeo.

CHADEMA wamewazunguka CUF kila kona. Wanaingilia mambo ya ndani ya chama ambayo hayawahusu. CHADEMA wanajaribu mpaka kuweka mawakili wakiongozwa na wanasheria wa chama hicho Tundu Lissu ili tu Prof Lipumba asifanikiwe kutwaa tena madaraka yake ya Mwenyekiti wa CUF.

CUF inaelekea kuzimu. Karibuni watatumbukia kwenye shimo refu ambalo limejaa wadudu, wanyama na takataka hatarishi. Hawatapita salama. Hawatasalimika. Hata kama CHADEMA watafanikiwa kuwaondoa wale wanaoona hatarishi ndani ya CUF, haitakuwa na tija kwa CUF bali faida kwa CHADEMA. Ndio lengo lao kuu. Ili watakapoingia 2020, CUF isiaminike tena na iwe imepoteza wafuasi wake wengi. Mwisho wa siku, UKAWA utavunjika rasmi na CHADEMA itasimamisha wagombea kwenye majimbo yote. Mwisho wa siku CUF kitakufa.

Nawahurumia sana CUF. Laiti wangalijua unafiki wa viongozi wa CHADEMA wasingalithubutu hata kuwaalika sebuleni.

Imeandikwa na Lizaboni/Jamii Forums



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger