Oct 5, 2016

VITA vya Syria na Hatari ya Kuzuka Vita vya Tatu vya Dunia

VITA vinavyoendelea nchini Syria vilivyodumu kwa miaka mitano sasa viko mbioni kuiingiza dunia yetu katika Vita Vikuu vya Tatu vya Dunia. Wakubwa wa Dunia yetu, Marekani na Urusi, wanaonekana kutofautiana kwa kiasi kikubwa ambapo sasa Marekani anasema hataki tena mazungumzo na mwenziwe Urusi kuhusu suluhisho la mgogoro wa Syria kwa njia ya amani bali anaangalia "Njia Mbadala" ya kumaliza mgogoro huo. Je, njia hiyo ni ipi?

Urusi yeye anadai yupo nchini Syria kwa mwaliko wa Rais Bashar Al Assad ili kumsaidia kupambana na makundi ya kigaidi yanayotishia utawala wake. Marekani kwa upande wake anaunga mkono kundi linalojiita Free Syrian Army kwa lengo la kumng'oa Rais Bashar Al Assad madarakani, ingawa wachambuzi wa mambo wanadai makundi yote ya kigaidi yanayopigana nchini Syria dhidi ya serikali ya Rais Bashar Al Assad, likiwemo kundi la Al Qaeda, yaliundwa na yanafadhiliwa na Marekani na nchini nyingine za Magharibi.

Urusi tayari ina zana za kutosha nchini Syria yakiwemo makombora yake ya kujihami ya S-400 kwa ajili ya kulinda anga. Vivyo hivyo Marekani nayo inadaiwa kupeleka silaha nchini Syria kupitia kwa makundi ya kigaidi.

Mapigano makali kwa sasa yanaripotiwa jijini Aleppo kati ya majeshi ya Assad na yale ya kigaidi, wote wakigombea umiliki wa mji huo.

Je, kivipi mgogoro huo unaweza kugeuka vita vya dunia? Kutokana na wakubwa hawa wawili Marekani na Urusi kuwa na masilahi yanayokinzana katika ardhi ya Syria yanayohusisha matumizi ya silaha, upo uwezekano mkubwa wa mgogoro huo kuwa wa dunia nzima. Hivi sasa Vladimir Putin anaonekana kuutawala uwanja wa mapigano nchini Syria kitendo ambacho Marekani hawatakubali kuona wakishindwa na kuaibishwa! Watakapoamua kuingilia kati moja kwa moja kwa kutuma askari wake na silaha zake, hapo ndipo patakuwa patamu maana Urusi naye hatakuwa na njia nyingine bali kuingia kimoja Syria na ikizingatiwa kwamba Urusi wana "ka historia ka kushinda vita japo kwa mbinde"; mfano, mwaka 1812 waliwanyuka Ufaransa na wakati wa WWII (1939 - 1945) tena wakawanyuka Wajeremani wa Hitler.

Kama inavyofahamika, Marekani ni mjumbe wa NATO, hivyo kuingia kwa marekani nchini Syria kupigana, kutamaanisha kundi la NATO kuingia vitani. Kwa upande wake Urusi, naye anao washirika wake kama China na Iran na wengine. Ikifikia hatua hiyo, nchi kama Korea ya Kaskazini inaweza kutumia mwanya huo kushambulia masilahi ya Marekani popote pale itakapoona panafaa.

Pale Mashariki ya Kati penyewe hapaeleweki hata kidogo -- Marekani iko na Israel na Saudi Arabia; Urusi ndiyo hivyo tena iko na Iran, Syria yenyewe, na Uturuki kwa mbali japo nayo ni ndumilakuwili.

Cha kutisha zaidi kuhusu wakubwa hawa kuingia vitani, ni silaha za kisasa na hatari zaidi, zikiwemo za Nyuklia wanazozimiliki, ambazo wakiamua kuzitumia basi ni majanga tupu.

TUOMBE TU HAWA WAKUBWA WAELEWANE ILI KUEPUSHA ZAHAMA HII
Imeandaliwa na:
Pasaka Osunga Rucho
0756231744.
Mwalimu anayesubiria ajira.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger