Oct 13, 2016

LUKUVI: Watumishi Ardhi Wezi

WILLIAM Lukuvi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema kuwa, watumishi wengi katika idara ya ardhi nchini ni wezi, anaandika Moses Mseti.

Na kwamba, watumishi hao wamekuwa wakishirikiana na matajiri kunyanyasa wananchi wanyonge.
Kauli hiyo ameitoa leo wakati akizungumza na wananchi walio na kero mbalimbali za ardhi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Shule ya Msingi Buhongwa ‘B’ Kata ya Buhongwa wilayani Nyamagana, mkoani humo.

Lukuvi aliutumia mkutano huo kugawa hati kadhaa za nyumba za wananchi wa kata hiyo, huku akimuagiza mkuu wa mkoa huo, John Mongella na viongozi wengine kuhakikisha nyumba zaidi ya 3,5000 zilizo katika makazi holela zinapimwa, kupangwa na kutolewa hati kabla ya 30 Juni mwakani.
Amesema kuwa, makazi na viwanja vinavyokuwa vinapimwa na wataalamu wa ardhi, viwanja vingi wamekuwa wakijimilikisha wao wenyewe kitendo kinachosababisha kuendelea kuwepo kwa migogoro ya ardhi kila kukicha.

Lukuvi ambaye pia ni Mbunge wa Isimani mkoani Iringa amesema kuwa, wataalamu hao wamekuwa wakishirikiana na baadhi ya matajiri kuuza viwanja vya umma kwa manufaa yao binafsi kitendo ambacho alidai hatakubaliana nacho kukiona kikiendelea kujitokeza.

“Wataalamu hawa wanapoenda kupima shamba watakwambia viwanja vimetoka 10 lakini wao tayari wameishabaki na viwanja vyao vya kutosha na wakija wanakuonesha michoro na kukueleza maeneo mengi ni bondeni, milima na maeneo ya wazi.

“Ukiangalia zaidi ya asilimia 88 ya Watanzania hawana hati za nyumba na tumekuwa tukipoteza Sh. 1 trioni kwa mwaka kutokana na nyumba za Watanzania hao kutokuwa na hati za umiliki na kama wangekuwa na hati tungekusanya kodi kutoka kwao,” amesema Lukuvi.

Amesema kuwa, asilimia 82 ya Watanzania hususani wa mijini wamekuwa wakiishia kwa hofu ya nyumba zao kubomolewa na kwamba, umefika wakati wananchi wapimiwe viwanja vyao ili waweze kufahamu kama wapo katika eneo salama huku akidai tatizo hilo linatokana na urasimu wa watumishi hao.

Hata hivyo amesema kuwa, kutokana na nyumba nyingi kuwa katika makazi holela, wizara yake imekuja na mpango mkakati wa miaka 10 kuanzia sasa wa kuhakikisha nyumba zote za mjini zinapimwa na kupatiwa hati ili serikali iweze kukusanya kodi na kuongeza pato la  taifa.
Mongella amesema kuwa, atahakikisha anasimamia suala la upimaji wa ardhi na nyumba zote zitakazo pimwa zinapatiwa hati ya umiliki ili wananchi waweze kuzitumia kukopa fedha katika taasisi za kifedha.

“Mkuu (Lukuvi) labda niseme tu, hiyo kazi ulionipa kwamba ifikapo Juni 30 mwakani nyumba hizo ziwe zimepatiwa hati na nyumba nyingine zipimwe mimi nasema 1 Januari ya mwaka mpya zoezi litakuwa limekamilika,” amesema Mongella huku watumishi wakiguna wakiashiria kupinga.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger