May 8, 2016

Barua ya wazi kwa John Pombe Magufuli, Rais wa awamu ya tano Tanzania.


Nianze kwa kusema wewe, Rais Magufuli ni binadamu na hakuna binadamu mkamilifu asiye na mapungufu, hiyo ni sifa ambayo Muumba wetu pekee anayo na anastahili kuwa nayo.

Mimi Mag3, nina hakika 100% kwamba nakusaidia Magufuli kuliko wanafiki wanaoshinda mitandaoni wakikusifia hata pale inapotakiwa uambiwe, hapana Mkuu, hapa umejikwaa.

Naamini Rais unasukumwa na nia ya dhati ya kuwasaidia ndugu zako Watanzania waondokane na matatizo yaliyoliandama taifa letu kama kupe kwa nusu karne toka tupate uhuru.

Katika misingi hiyo nina hakika kwamba Rais unafuatilia ukosoaji wetu ukijua unakusaidia katika kujua kwa nini wengine wetu tulikunyima kura na tulifanya hivyo kwa kusukumwa na nini.

Kila mtu anajua fika kwamba kuitoa CCM madarakani kwa Katiba tuliyo nayo ni ndoto, hata hivyo bila kujali maslahi binafsi, tuliwapigia kura wapinzani kwa kuzingatia maslahi ya taifa.

Tulifanya hivyo tukijua juhudi zitakazotumiwa na chama tawala kuhakikisha ndoto zetu zitabaki ndoto kwani uhuru na haki ni vitu viwili adimu sana katika msamiati wa CCM.

Wapo waliatanguliza maslahi binafsi na kwa tamaa ya ajira serikalini, mafanikio kibiashara na kitaaluma, walikupigia kura wakitegemea upendeleo kiitikadi katika teuzi mbali mbali.

Watu kama hao kamwe hawawezi kupata ujasiri wa kukuambia ukweli na kwa kuwa wengi ni wa chama chako, watakusifu mchana huku usiku wakilalama walivyo na wasiwasi nawe.

Wengine hatuko hivyo, hakuna tunachotaka kwako bali utawala bora unaotoa uhuru na haki kwa wananchi wote bila kujali kabila, jinsia, rangi, itikadi...yote kama yalivyooanishwa ndani ya Katiba.

Hivyo hatutasita kuita koleo kwa jina lake kama tutahisi hatutendewi haki kwa kufuata sheria na kwa bahati wote tunakubaliana kwa jambo moja la msingi...kutanguliza maslahi ya kwa taifa.

Tunajua kwamba watendaji wote wakuu waliotufikisha hapa tulipo ama walikuwa ni viongozi wa CCM na serikali yako kwani ndio wamekuwa waamuzi wa hatma ya nchi miaka yote.

Hivyo inajulikana wazi kuwa kama majipu yapo, ama yapo tele ndani ya chama chako au ndani ya serikali yako na yaendelee kutumbuliwa tu hata kama mengine yapo sehemu nyeti.

Tatizo linakuja pale majipu yanapokushangilia ukitumbua majipu, ni jukumu ketu kukushtua uwe mwanagalifu na huo ushangiliaji kwani hakuna namna unaweza kuwa kwa nia njema.

Tukikosoa tunaitwa maadui lakini kwa ukweli sisi tunafanya hivyo kwa nia njema tu na hapa tunasisitiza nia ni kukusaidia kiutekelezaji kuliko inavyopotoshwa na wanafiki waliokuzunguka.

Huna haja ya kutuogopa kama nia yako na yetu tunaokukosoa ni moja...kuliona taifa linanusurika kutoka lindi la umasikini...achana kabisa na wanafiki, ungana na wananchi wa Tanzania. Mungu ibariki Tanzania.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger