Tafadhali mama yangu mwite kijana wako mwanamke na mwanachama mwezio mpe darasa mambo yanamwndea Kombo, mwelekeze namna ya kua mvumilivu kama kiongozi anayeweza kua na uwezo wa kutumia mizani vizuri awapo katika kiti chake.Sipendi sana kuona mwanamama akilalamikiwa sana kwa utendaji wake, mfunde namna ya kuchuja hoja zenye maslahi ya kitaifa na zisizokua na maslahi ya kitaifa, mfunde namna ya kusikiliza hata kama anona ni pumba maana kila mtu anayo haki ya kutoa hoja na kusikilizwa, mwele atambue kua anaongoza kila aina ya kichwa na asili yake.Mwambie ifike mahali apime upepo kulingana na aina ya tukio linalotolewa hoja,Mfunde namna ya kutafuta suluhu kwa mazungumzo na maridhiano kama ulivyokua ukifanya wewe maana ubabe hua una kikoma.
Ni rai yangu kua wewe kama malkia wangu wa nguvu utatumia busara na hekina zako kuweka baadhi ya mambo sawa pindi unapoona hayaendi sawa ikikubidi. Najua kaka yangu Ndungai anao uwezo huo lakini naona pengine darasa lake bado halijamkolea kijana huyu mwanamama maana naamini pia kwa Ndungai kuna kitu ulimwachia kwa muda wote ulipokua pamoja nae.
By Mahanju
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment