Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Meja Jenerali mstaafu, Raphael Muhuga alitoa agizo hilo jana katika kikao baina yake na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa pamoja na waandishi wa habari.
Alikuwa akitoa taarifa ya kubainika kwa watumishi hewa wapya mkoani humo.
Muhuga alisema kuendelea kubainika kwa watumishi hao hewa, itawabidi wakurugenzi kuhakikisha fedha zote zilizolipwa kwa watu hao zinarejeshwa serikalini kwa muda aliowataka wazirejeshe na wampatie taarifa itakayothibitisha fedha hizo kurejeshwa.
Pia, mkuu huyo wa mkoa aliagiza maofisi wa ofisi ya utumishi wachukuliwe hatua ya kinidhamu kwa kusababisha watumishi hao hewa kulipwa fedha.
“Hili siyo suala la bahati mbaya, bali hawa watu walidhamiria kulipa mishahara hiyo hewa naimani wapo wenye maslahi juu ya jambo hili,” alisema Muhuga.
Aliagiza wakurugenzi wote wa halmashauri, wahakikishe maofisa utumishi wanawafuta watumishi hewa wote kwenye leja zao na wawachukulie hatua wote waliohusika na suala hilo.
Hata hivyo, aliishukuru kamati ya watu wanne iliyoundwa kufanya kazi ya uhakiki wa watumishi mkoani humo.
Aliitaka iharakishe kukamilisha uchunguzi wa watumishi 15 ambao taarifa zao zimebainika kuwa na utata.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment