May 6, 2016

Wasomi: Mwelekeo Mzuri Miezi Sita ya Magufuli

Rais John Magufuli anatimiza miezi sita madarakani akiwa ameanza kutekeleza sehemu ya sera zake za uboreshaji utumishi wa umma na kukuza uchumi huku baadhi ya wasomi na wanaharakati wakieleza kuwa zina mwelekeo mzuri na kushauri upungufu uliopo udhibitiwe.

Katika kipindi hicho cha siku 180, Dk Magufuli ametangaza kubana matumizi serikalini, kuongeza ufanisi katika utumishi wa umma kwa kutumbua watumishi wanaotuhumiwa kwa ubadhirifu na uzembe huku akidhibiti ukwepaji kodi uliokuwa umeshamiri nchini.

Sehemu kubwa ya mikakati hiyo inayoendeshwa na kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ imepokewa kwa mikono miwili na wananchi huku baadhi wakionyesha wasiwasi kuwa yapo baadhi ya masuala yanayotakiwa kuwekewa mkazo au kurekebishwa ili kuzuia madhara siku zijazo.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la vyama huru vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Nicholas Mgaya alisema utendaji wa Rais Magufuli kwa miezi sita ya awali unaridhisha “kwa kiasi fulani” katika jitihada za kuwaletea Watanzania maendeleo.

Hata hivyo, Mgaya alisema kuna maeneo ambayo hayajaguswa ipasavyo kama sekta ya elimu, afya na Serikali za Mitaa ambako kuna viongozi wachache wanaotumia nafasi zao kuwanyanyasa wananchi na watumishi na kufanya ubadhirifu wa mali ya umma.

“Huko ndiko kuna uozo mkubwa na Watanzania wengi wanaishi kwenye halmashauri za wilaya, miji na majiji. Rais aweke nguvu kutumbua viongozi miungu watu,” alisema Mgaya.

Katika miezi yake ya awali Ikulu, Rais amekuwa katika kampeni kali ya kubana matumizi ambayo imekwenda sambamba na ufutaji wa safari za nje kwa watumishi wa umma mpaka kwa kibali maalumu akisema kuwa ni “mzigo kwa Taifa”.

Ubanaji huo wa matumizi ulihusisha upigaji marufuku taasisi za umma kutumia kumbi za kukodi kufanyia mikutano na badala yake kutumia majengo ya Serikali, jambo ambalo limepingwa na baadhi ya wachumi.

Honest Ngowi, Profesa wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe alisema kubana matumizi yasiyo ya lazima ni jambo jema lakini ubanaji huo ukifanyika kuzidi kiwango huleta madhara kiuchumi kwa kuwa Serikali inahimizwa kutumia ili kuchochea maendeleo.

“Serikali ni mlaji mkubwa mahali popote ulimwenguni. Wasibane matumizi kupitiliza, uchumi utasinyaa,” alisema.

Hata hivyo, alisema Dk Magufuli amefanya vyema zaidi katika kudhibiti ukwepaji kodi katika maeneo mbalimbali hususan bandarini ambako hali ilikuwa mbaya.

Katika kuhahikikisha nyumba inakuwa safi, Dk Magufuli alianza utawala wake kwa utumbuaji majipu ambao umeshuhudia vigogo wa mashirika makubwa nchini kama Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) wakisimamishwa kupisha uchunguzi wa tuhuma za ufisadi.

Hata hivyo, utumbuaji huo umeonekana kukubalika na wengi lakini baadhi wamepinga staili ya watumishi hao wanavyotumbuliwa ikiwamo kuuliza wananchi kama mtumishi anafaa kutumbuliwa au la kama alivyofanya Rais wakati akimtumbua aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe wiki mbili zilizopita.

“Hawa wanaotumbuliwa wakienda kwenye vyombo vya sheria na kushinda kesi, Serikali italipa fedha nyingi. Huo utumbuaji wa majipu ni mzuri katika kurudisha nidhamu serikalini lakini ni vyema ukazingatia sheria,” alisema Mgaya.

Rais Magufuli amekuwa akieleza kuwa Serikali yake imelenga kuipeleka nchi kuwa na kipato cha kati kwa kukuza sekta ya viwanda na kilimo ili kuongeza ajira na uzalishaji.

Mkurugenzi wa asasi ya kiraia ya Fordia, Buberwa Kaiza alisema hadi sasa utawala wa Rais Magufuli una mwelekeo mzuri katika usimamizi wa kiuchumi lakini amekosa sera kuu ya uchumi.

“Kueleza kuwa nchi ya viwanda ni sawa lakini mwelekeo wa uchumi ndiyo unasaidia kwa sababu viwanda hivyo havijengwi na Serikali, bali wawekezaji,” alisema Kaiza.

Kuhusu utendaji wa Serikali kwa ujumla, Kaiza alisema Rais Magufuli anaipeleka nchi katika mwelekeo mzuri kwa kuwa ameitoa kwenye ngazi hasi hadi sasa ambako ufanisi umeanza kuonekana katika utumishi wa umma.

Alisema kuna madhara ya muda mfupi ya kiuchumi kutokana na ubanaji matumizi na ukwepaji kodi lakini ni bora kuliko kuwa na kampuni inayosaidia ukuaji uchumi kwa kuajiri wengi kwa njia zisizo halali.

Lakini wakati utawala wa Rais Magufuli ukipigiwa chapuo katika miezi sita ya awali, sakata la kuzuia matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge limeanza kuonyesha kuwa huenda Serikali yake ikafanya vibaya kwenye masuala ya utawala bora.

Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Shumbusho Damian alisema mikakati ya Rais kuirudisha nchi kwenye mstari ni mizuri lakini utawala bora utashuka iwapo wananchi wananyimwa uhuru wa kujieleza na kupata habari.

“Unaweza kufanya maboresho ya kila aina nchini kwa kutoa huduma bora lakini usishawishike kudhibiti uhuru wa kujieleza,” alisema.

Pia, alionyesha wasiwasi kuwa utumbuaji majipu unajenga nidhamu ya woga kwa kuwa watumishi wengi wanafanya kazi kwa kuhofia kufukuzwa bila ya kuwa ari ya kuwahudumia wananchi.




Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger