Jun 12, 2016

Maalim Seif ziarani Marekani, Anatarajiwa Kuieleza Jumuiya ya Kimataifa Kilichojiri Kwenye Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amekwenda Marekani na kesho ataiambia jumuiya ya kimataifa, kilichojiri kwenye Uchaguzi Mkuu na kusababisha chama chake kususia uchaguzi wa marudio wa Rais wa Zanzibar ulioipa CCM ushindi.

Mkutano huo umeandaliwa na Kituo cha Elimu ya Kimkakati na Kimataifa cha Marekani (CSIS) na utafanyika makao makuu ya taasisi hiyo yaliyoko Washington DC kuanzia saa 4:00 asubuhi.

“Tumewambia Wazanzibari kuwa ni lazima tudai haki yao ya maamuzi ya kidemokrasia waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba 2015 kupitia kura zao.

"Tumewaambia tutadai haki yao ndani ya Zanzibar, ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na katika jumuiya ya kimataifa,” alisema Maalim wakati akiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Katika barua ya mwaliko iliyoandikwa na mkurugenzi wa CSIS, Jennifer Cooke, Maalim Seif atatoa mada kwenye mjadala uliopewa jina la “The Zanzibar Elections: Democracy Deferred (Chaguzi za Zanzibar: Demokrasia iliyocheleweshwa)”.

Maalim atakuwa miongoni mwa watoa mada watatu. Wengine ni balozi wa zamani wa Marekani nchini Tanzania,Mark Green na naibu mkurugenzi wa kanda wa Kusini na Mashariki mwa Afrika wa Taasisi ya Taifa ya Kidemokrasia (NDI), Mercedeh Momeni.

“Tafadhali jiunge nasi katika kikao hiki, ambacho Bwana Hamad atachangia mtazamo wake kuhusu uchaguzi wa 2015 na ni jinsi gani Zanzibar na Tanzania zinaweza kutatua migogoro ya kikatiba na kisiasa yanayosababishwa (na mambo hayo),” inasema tovuti ya CSIS ikizungumzia mjadala huo wa kesho.

Maalim Seif alikuwa mgombea urais wa Zanzibar mwenye upinzani mkubwa kwa mgombea wa CCM, Dk Ali Mohamed Shein na ameshagombea urais kwenye chaguzi zote tangu siasa za ushindani zirejeshwe mwaka 1992.

Mara zote amekuwa akilalamikia kuchezewa rafu na mwaka jana mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC), Jecha Salim Jecha alitangaza kufuta matokeo ya urais, wawakilishi na madiwani kwa maelezo kuwa sheria na kanuni za uchaguzi zilikiukwa.

Jecha alifanya uamuzi huo Oktoba 28, siku ambayo alitakiwa atangaza mshindi wa kiti cha urais baada ya matokeo ya majimbo 31 kuwa yameshatangazwa na mengine tisa yaliyosalia kuwa yameshahakikiwa.

Kabla ya kutangaza uamuzi huo, hakuonekana Oktoba 27 na siku iliyofuata alitangaza kufuta matokeo akiwa studio za kituo cha televisheni cha Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC).

Katika uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi 20, CUF haikushiriki na imeshatangaza kutoitambua Serikali ya Dk Shein.

Maalim Seif aliondoka juzi jioni akiwa ameambatana na mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa CUF, Ismail Jussa Ladhu, na katibu wake, Issa Kheir Hussein.

Kadhalika taarifa kutoka CSIS zinasema mkutano huo utashirikisha viongozi mashuhuri duniani, wakiwamo wa viongozi wa Ivory Coast na Sierra Leone.

NDI imeeleza kuwa wamemwalika Rais Alessane Watarra wa Siera Leone ili kutoa ushuhuda wa namna demokrasia ilivyoporwa katika nchi yake kabla vyombo vya kimataifa na umma kutumika na kuwaondoa madarakani viongozi waliokuwa madarakani.

Mkutano huo unafanyika wakati ambao wakuu wa NDI wamemwandikia Rais Barack Obama wa Marekani wakimlaumu kwa kuacha mambo yaendelee kama yalivyo nchini Tanzania.

Barua kwenda kwa Obama inasema Rais huyo wa taifa kubwa duniani ameshindwa kusimamia demokrasia barani Afrika, kutofanya maamuzi ya haraka dhidi ya kile kilichojiri Tanzania katika uchaguzi wa mwaka 2015.

“Tanzania imepoteza sifa yake ya kuwa kipimo cha demokrasia na utawala bora miongoni mwa Nchi za Afrika Mashariki na Kati,” inasema barua hiyo ya NDI iliyoandikwa na Cooke.

“Vipi uhusiano wa Marekani uendelee wakati tunajua Tanzania ilipoteza sifa yake ya kutekeleza demokrasia? Na vipi tuweke mazingira ya kusaidia sehemu ambayo demokrasia imeporwa na maamuzi ya watu wa Zanzibar hayakuheshimiwa?”

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger