Jun 17, 2016

Mjadala wa Mikoa Masikini Waligawa Bunge

TAKWIMU kuhusu mikoa mitano masikini zaidi nchini, zimezidi kuzua mjadala bungeni huku wabunge wakizitumia kutaka misaada zaidi katika mikoa yao na wengine wakidai zinawafanya wahofu kwamba kuna ajenda ya siri kwani hawaamini usahihi wake.

Katika mjadala wa jana kuhusu bajeti inayopendekezwa na serikali kwa mwaka wa fedha 2016/17, aliyeanza kulalamikia takwimu hizo na kukataa kuunga hoja hiyo ya serikali ni Mbunge wa Rufiji, Mohamed Mchengelwa.

Mbunge huyo wa CCM alisema katika utafiti wake, amegundua kwamba waziri alipata takwimu hizo kutoka halmashauri, lakini akasema yeye ametafiti na kugundua kwamba kamwe Pwani haiwezi kuuzidi mkoa wa Mwanza kwa utajiri kama takwimu hizo zinavyoonesha.

Alisema takwimu hizo zinaonesha kana kwamba mkoa wa Pwani, una hali nzuri wakati si kweli, kwani hali ni mbaya, vyama vya msingi takribani vyote vimeanguka na kwamba anapata hisia kuwa takwimu hizo, zimetumiwa kuinyima Pwani mambo mengi katika bajeti inayopendekezwa.

“Rufiji, kwa mfano haijawahi hata kupelekewa trekta… Hali ni mbaya na hata bajeti kwa ajili ya kuinua kilimo Rufiji hakuna. Mimi kama mwanasheria niko tayari kuapa kuonesha kwamba takwimu alizotumia Waziri si sahihi,” aling’aka.

Naye Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega (CCM), alisema anadhani mkoa wa Pwani umewekwa kwenye kundi la mikoa tajiri kwa bahati mbaya, kwani akitazama kila kitu hakiendi vizuri.

“Hata korosho ambalo ndilo zao kuu la biashara mkoa wa Pwani tuko chini, hatuwezi kulingana na wenzetu wa Lindi au Mtwara,” alisema na kutaka waziri aeleze vigezo vilivyotumika kuainisha mikoa yenye hali mbaya kiuchumi nchini na yenye hali nzuri.

Lakini Mbunge wa Nyamagana mkoa wa Mwanza, Stanslaus Mabula (CCM), alitumia takwimu hizo kutaka serikali kuanza kwa kuupa mkoa huo Sh milioni 50 zilizoahidiwa katika kila kijiji ili wananchi wa mkoa huo wapunguze ‘umasikini wao’.

 “Ninaomba hizi shilingi milioni 50, zianzie katika mikoa iliyoainishwa kuwa masikini kwa mujibu wa takwimu za waziri ukiwemo mkoa wangu wa Mwanza,” alisema Mabula.

Naye Mbunge wa Bukoba Vijijini (CCM), Jason Rweikiza alitumia takwimu hizo kutaka serikali kuwaondolea wakulima wa kahawa kodi 26 wanazolazimika kulipa pamoja na kudhibiti ugonjwa wa mnyauko unaoshambulia migomba ili kuwaokoa wananchi wa Kagera na umasikini.

“Kahawa inakatwa kodi 26, kwa nini wananchi wasiwe masikini? Migomba inaelekea kumalizika kabisa kwa sababu ya ugonjwa wa mnyauko, kwa nini wananchi wasiwe masikini,” alisema.

Mbunge wa Viti Maalumu, Maria Kangoye anayewakilisha mkoa wa Mwanza alipinga takwimu zinazoonesha kwamba mkoa huo ni miongoni mwa mikoa mitano masikini nchini.

Alisema takwimu za Benki Kuu (BoT) zinaonesha kwamba Mwanza ni mkoa wa pili nyuma ya Dar es Salaam katika kuchangia kwenye Pato la Taifa.

Akiwasilisha bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi ya Mwaka 2015 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa mwaka wa fedha 2016/17, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alitaja mikoa masikini zaidi kuwa ni Kigoma, Geita, Kagera, Singida na Mwanza; wakati mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Arusha, Pwani na Manyara ndiyo mikoa mitano yenye ahueni ya umasikini nchini.

Akiuliza swali la papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa jana, Mbunge wa Biharamulo Magharibi, Oscar Mukasa (CCM), alisema utafiti kuhusu kipato cha kaya, umebaini mikoa mitano inayokabiliwa na umasikini uliokithiri na kumtaka Majaliwa kueleza serikali itafanya nini katika mikoa hiyo ili iondokane na aibu wakati ina fursa za kiuchumi ikiwemo kilimo cha pamba, mibuni na michikichi.

Majaliwa alisema serikali haijaacha jambo hilo kama lilivyo, bali imekuwa ikishawishi wananchi kujianzishia miradi na wengine waunde vikundi, ikiwemo vya Vicoba ili kujijengea mtaji wa pamoja ili waanzishe miradi hiyo.

Alisema kwa Tanzania msingi mkubwa wa kuondokana na umasikini ni kilimo na maeneo ya kulima yapo, ndio maana Serikali inasema ‘Hapa Kazi Tu’ ili watu wajikite katika kilimo.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger