Jun 17, 2016

Mtoto wa Miaka 9 Aichambua SMG Mbele ya Kamanda Sirro

Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema kuna vikundi vinavyowapeleka watoto porini na kuwapa mafunzo ya kigaidi.

Alisema jeshi hilo liliwahi kumkamata mtoto wa miaka tisa, katika pori lililopo wilayani Mkuranga, Pwani, aliyepewa mafunzo ya kigaidi na kuwastaajabisha kwa kuwa na uwezo wa kuichambua silaha ya kivita.

Sirro aliyazungumza hayo jana wakati wa ibada ya shukrani iliyofanyika katika Kanisa la Katoliki Parokia ya Makabe Bikira Maria, katika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika.

Aliwataka viongozi wa Serikali za mitaa kutoa ushirikiano, pindi wanaposikia mzazi amemuachisha mtoto shule na kumpeleka porini kwa ajili ya mafunzo ya kigaidi.

“Haya mambo yanafanyika kwenye mitaa yetu, lakini kinachojitokeza kiongozi wa Serikali ya mtaa anaposikia kuna mtoto wa fulani amejiunga kwenye vikundi viovu, hawatoi ushirikiano kwa Jeshi la Polisi,” alisema.

Akiwa katika maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Kituo cha watoto wanaoishi mazingira magumu cha Child in the Sun, Sirro alisema kuna kikundi kimeibuka ambacho kinawachukua watoto wa shule na kuwapeleka porini, kwa ajili ya mafunzo hayo ambayo alisema hayajengi nchi bali yanabomoa.

Padri wa Parokia hiyo, John Maendeleo aliishauri jamii kuwajengea mazingira mazuri watoto wao ili waweze kuepukana na vitendo vya kihalifu.

Padri Maendeleo aliwataka wazazi wawajibike kwa watoto wao ili wasiingie kwenye dhambi ya uvivu, kwa kumuweka mbele Mungu kwani watakuwa kwenye maadili mema.

Wakati huo huo, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imesema kutofanyiwa marekebisho kwa sheria ya ndoa ya mwaka 1971, inayoruhusu mtoto wa kike kuolewa akiwa na umri wa miaka 15, bado ni tatizo nchini.

Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Francis Nzuki alisema kutoondolewa kwa kipengele hicho ni changamoto, ingawa tatizo hilo linatatuliwa kwa mtoto kupelekwa shule. “Sheria ya elimu inatatua changamoto hiyo ya kisheria, kwa yeyote atakayekatisha masomo ya mtoto kwa namna yoyote kuchukuliwa hatua za kisheria,” alisema.

Alisema adhabu ya miaka 30 kwa atakayekatisha masomo au kifungo cha maisha, imesaidia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa changamoto za ukandamizwaji wa haki za mtoto ikiwa ni pamoja na kukosa nafasi ya kupata elimu.

Alisema kuongezeka kwa vitendo vya kikatili katika jamii kunasababishwa na kukosekana kwa elimu na umaskini katika jamii.

Mratibu wa Shirika lisilo la kiserikali la World Vision, John Massenza alisema kumekuwa na vitendo vya ubakaji na ulawiti wa watoto huku jamii ikiwa kimya.

Alisema Shirika la World Vision limekuwa mstari wa mbele kupigania haki za watoto, lakini wamekuwa wakipata vikwazo kutoka kwenye jamii kufichua maovu yanayotokea, hivyo kuihimiza kutoa taarifa kwa vyombo vinavyohusika.

Imeandikwa na Pamela Chilongola, Colnely Joseph na Filbert Rweyemamu.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger