Jul 29, 2016

CHADEMA wamjibu Msajili wa Vyama vya Siasa juu ya tuhuma za kutumia matusi, uongo, uchochezi

Baada ya kulifanyia uchambuzi na kulitafakari tamko la Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, lililotolewa jana na msajIli mwenyewe, Jaji Francis Mutungi tumeona ni jambo lenye afya kwa ustawi wa demokrasia nchini, kusahihisha upotoshaji uliomo katika taarifa hiyo ili kuendelea kumsaidia msajili na watu wengine, watawala na walio sehemu ya utawala, kuelewa matakwa na maslahi ya wananchi hasa katika wakati huu ambao taifa linapitia.

Kwa hakika tumeshangazwa na kauli zilizotolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa, ambaye pia ni Jaji wa Mahakama Kuu, kutokana na jinsi ambavyo anaanza kuonesha kuyumba katika kutimiza wajibu wake hasa kwa kutumia weledi na ujuzi wake wa sheria kwa kiwango cha nafasi yake kama jaji.

Katika tamko lake alilolitoa jana na kunukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari jana hiyo na leo, ameshindwa kuonesha neno hata moja linaloashiria matusi, kashfa, uongo au hata kuvuruga amani lililotolewa mbele ya waandishi wa habari juzi wakati Chama kikisoma hadharani maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu.

Ni jambo la kushangaza kuwa Msajili Mutungi, Jaji wa Mahakama Kuu ameweza kuweka vifungu vingi vya kisheria akidai kuwa vimevunjwa lakini hawezi kuonesha ushahidi wa namna vilivyovunjwa au maneno yanayothibitisha kuvunja hizo sheria.

Hii si sahihi hata kidogo na inakuwa ‘serious’ zaidi inapofanywa na mtu mwenye weledi wa sheria wa kiwango cha Jaji Mutungi.

Wakati Jaji Mutungi akinukuu vifungu vya sheria na kanuni akionekana dhahiri kuwa kuegemea na kuwatetea watawala ambao wamedhihirisha kuwa wanatamani nchi irudi enzi za ‘ujima’ wa fikra za chama kimoja, kwa sababu anazozijua mwenyewe amesahau au ameshindwa au amefanya makusudi kwa sababu anazozjijua mwenyewe, kunukuu kifungu cha 4(1) (e) cha maadili ya vyama vya siasa za mwaka 2007, ambacho kinatoa haki kwa vyama vya siasa kuendesha shughuli zao za kisiasa ikiwemo mikutano ya hadhara na maandamano kwa mujibu wa sheria.

Tulidhani kuwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye si tu kwamba ni mlezi wa vyama vyote bali pia anasimama kama mwamuzi wa mchezo wa mpira uwanjani, katikati ya timu mbili uwanjani, angelisimamia kifungu hicho muhimu na kukitumia kuwakemea na kuwaonya watawala, akiwemo Rais, Waziri Mkuu na Jeshi la Polisi wasivunje sheria za nchi kuzuia shughuli za siasa nchini kwa sababu yoyote ile kwa sababu hawako juu ya sheria za nchi hii.

Aidha, sasa tunaanza kushtuka na kuanza kujiuliza maswali mengi kuhusu kasi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kujijengea utaratibu usiokuwa na kawaida kwa nafasi yake ya kisiasa na kisheria, kuwa na kasi ya ajabu kutoa kauli au matamko yanayoonesha kuwatetea/kuwalinda watawala wanapovunja sheria zinazosimamia vyama vya siasa.

Jaji Mutungi amekuwa mahiri wa kuvikemea au hata kuvionya vyama vingine tofauti na CCM, kila vinapodai haki za kisiasa ambazo ziko na zinapaswa kutekelezwa kwa mujibu wa sheria, wala si kwa hisani ya mtu yeyote.

Waandishi wa habari na umma kwa ujumla watakuwa mashahidi kwa namna ambavyo CCM wamekuwa wakitumia vyombo vya dola, kuvikandamiza, kuvinyanyasa, kuviwekea mazingira magumu na kuvinyima haki za kufanya siasa vyama vingine washindani wake kwa ajili tu ya kulinda maslahi ya chama kilichoko madarakani.

Katika hali hiyo ambayo hata imekuwa ikisababisha mauaji na umwagaji damu za watu wasiokuwa na hatia kwa sababu tu ni wafuasi wa vyama vingine, Msajili wa Vyama vya Siasa hajawahi kuthubutu kujitokeza hadharani kuwaonya na kuwakemea CCM na walioko serikalini kuwa kutumia vyombo vya dola kwa manufaa yao ya kisiasa ni kosa kwa mujibu wa sheria za nchi kupitia kifungu cha maadili ya vyama vya siasa cha 5(1)(c), za mwaka 2007.

Tulitegemea kwa kutumia umahiri huo huo wa kunukuu vifungu vya sheria na kanuni za maadili ya vyama vya siasa ambao Msajili amekuwa akiuonesha dhidi ya vyama washindani wa CCM kila vinapodai haki za msingi za kisiasa, angekuwa ameutumia pia kuwakemea, kuwaonya au hata basi kuwakumbusha CCM na Rais Magufuli kwa kutumia kifungu cha 5(1) (i) cha kanuni za maadili ya vyama vya siasa za Mwaka 2007, kuwa ni makosa kutumia mamlaka, rasilimali za serikali, vyombo vya dola au wadhifa wa kiserikali, kuvikandamiza vyama vingine kwa manufaa ya kisiasa ya upande mmoja.

Si hayo tu, Jaji Mutungi ama aliamua kuwa kimya au alikuwa na kigugumizi aliposikia;

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Rais John Magufuli na Jeshi la Polisi wakitoa kauli kinyume cha sheria wakitangaza na kuagiza kuzuia shughuli za kisiasa nchini kwa matakwa yao tu.
Mabalozi na wanadiplomasia wakizuiwa kukutana na asasi zisizo za kiserikali au vyama vya siasa.
Kukiukwa kwa misingi ya sheria, kanuni na taratibu za nchi katika uteuzi wa wakurugenzi na makatibu tawala.
Hali tete inayoendelea Zanzibar baada ya watawala kuharibu uchaguzi mkuu mwaka jana kisha wakafanya uchaguzi wa marudio kwa maslahi ya CCM, kinyume kabisa na sheria za nchi.

Hayo ni baadhi tu ya masuala ya muhimu ambayo ofisi ya msajili ilitarajiwa kuwa ingekuwa mstari wa mbele kukemea na kuonya ili kuweka mizania ya ushindani wa kisiasa katika usahihi wake.

Kwa mwenendo huu ambao usipoangaliwa na kufanyiwa kazi ya kuurekebisha haraka, tunachelea kusema kuwa Ofisi ya Msajili na Jaji Mutungi mwenyewe wataanza kujikosesha uhalali machoni pa Watanzania ambao wasingependa kuona siasa ambayo ni maisha yao, ikifananishwa kama vile ni jambo la kawaida tu lisilokuwa na maana.

Kupitia taarifa hii, tunamtaka Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Mutungi kuwa makini na utaratibu huo vinginevyo Watanzania wataanza kuiweka ofisi yake na yeye mwenyewe kwenye kapu moja na aliyekuwa mtangulizi wake, ambaye ilifika mahali wananchi walimuona yeye binafsi, kupitia kauli zake, matendo yake na ofisi yake kwa ujumla, sawa na sehemu ya chama kilichoko madarakani.

CHADEMA kama chama kikuu cha upinzani nchini hakiwezi kuvumilia wala kukubali hiki kinachoanza kujionesha kuwa ni ‘double standards’ za mtu anayetarajiwa kuwa mlezi na refarii, kujitokeza hadharani pale tu ambapo maslahi ya chama tawala na watawala yanapoguswa lakini anakuwa kimya na hata kuweka masikio nta mara vyama washindani wa CCM vinapokandamizwa, kinyume kabisa cha sheria.

Kama chama chenye wanachama na viongozi wanaojua haki na wajibu wao wa kikatiba na kisheria, tutaendelea kufanya shughuli za kisiasa kwa namna itakayosimamia  haki na matumaini ya wananchi kwa ajili ya amani na utulivu wa kweli, kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi si kwa kufuata matamko, kauli au maelekezo ya mtu yeyote.

Ni kwa kuzingatia dhana hiyo, maana Kamati Kuu katika kikao cha dharura kilichofanyika mwishoni mwa juma lililopita na maazimio yake kutangazwa juzi Jumatano, moja ya maazimio yake ni kuanzisha operesheni ya UKUTA (Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania) ambayo inalenga kuwaunganisha Watanzania wote bila kujali tofauti zao zozote zile, kudai haki na matumaini dhidi ya udkiteta katika nchi yao na kuzuia harakati za watawala kuataka kupora mamlaka ya wananchi na kujiweka juu ya sheria kwa namna ile ile ambayo madikteta hufanya.

Imetolewa leo Ijumaa Julai 29, 2016 na;
Prof. Mwesiga Baregu
Mjumbe wa Kamati Kamati Kuu

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger