Jul 29, 2016

Taarifa ya Wizara ya Afya kuhusu kuvamiwa kwa shirika lililokuwa likigawa vilainishi Shinyanga

Wizara imepokea taarifa kuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Shinyanga imevamia ofisi za shirika la Jhpiego mkoani humo na kukamata baadhi ya watumishi wake kwa madai ya shirika hilo kugawa mafuta maalumu yanayodhaniwa kutumiwa kuhamasisha ngono za jinsia moja. Baada ya taarifa hiyo wizara inapenda kutoa ufafanuzi ufuatao:

Si kweli kwamba shirika la Jhpiego limekuwa likihamasisha ngono baina ya wapenzi wa jinsia moja. Shirika hilo kupitia mradi wa “Sauti” linasaidia serikali katika jitihada za kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa makundi yaliyopo kwenye hatari kubwa ya maambukizi.

Moja ya makundi yanayolengwa ni wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao. Shirika limekua likitoa elimu ya mabadiliko ya tabia kwa wanaume hao huku likiwapatia mafuta hayo kama sehemu ya kuwasaidia kupunguza hatari ya maambukizi.

Mafuta hayo yaliingizwa nchini kwa kufuata taratibu za kisheria kwa ufadhili wa Mfuko Maalumu wa Rais wa Marekani wa kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI (PEPFAR).

Ndugu wanahabari, kama mtakumbuka hivi karibuni Wizara kupitia kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu ilisitisha ugawaji wa mafuta hayo maalumu (vilainishi) miongoni mwa makundi hayo maalumu.

Kufuatia agizo hilo, Wizara iliagiza Shirika hilo kukusanya mafuta hayo na kuyarudisha katika ofisi za PEPFAR zilizopo Ubalozi wa Marekani ili yapelekwe katika nchi nyingine zinazofadhiliwa na PEPFAR ambazo matumizi ya mafuta hayo hayajazuiwa.

Ndugu wanahabari, Shirika hilo lilitekeleza agizo la wizara la kukusanya mafuta hayo na kuyaweka katika ofisi zao za kanda, tayari kuyasafirisha kuja jijini Dar es Salaam, ambapo umeandaliwa utaratibu maalumu wa kuyapeleka katika nchi nyingine bila kuyaharibu.

Mnamo tarehe 27 mwezi July, mwaka 2016 Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani Shinyanga ilivamia Ofisi za Shirika hilo na kuchukua mafuta hayo bila kuelewa utaratibu uliotolewa na Wizara wa kukusanya mafuta hayo na kuyarudisha katika ofisi za PEPFAR.

Zoezi hilo la kamati ya Ulinzi na Usalama halikushirikisha wizara ya Afya wala wadau wa sekta ya Afya wilayani humo, ambao wanaelewa vizuri utaratibu uliowekwa na wizara kukusanya mafuta hayo na kuyarudisha mahali husika bila kuyaharibu.

Ndugu wanahabari, tayari Wizara imeshamuandikia barua Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga kutaka mafuta hayo yaliyochukuliwa kurudishwa katika ofisi za mradi wa Sauti zilizopo mtaa wa Mwasele, kata ya Kambarage mkoani Shinyanga ili zoezi la kuyakusanya na kuyarudisha Dar es Salaam liweze kuendelea.

Mwisho, Wizara inapenda kuwajulisha kuwa shirika la Jhpiego ni miongoni mwa wadau wakuu wa Serikali ambao wamekuwa wakisaidia huduma mbalimbali za Afya nchini ikiwemo kusaidia ujenzi wa vituo vya afya, kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kuboresha Afya ya mama na mtoto na Uzazi wa Mpango kwa zaidi ya miaka kumi sasa. Hivyo serikali imeridhia shirika hilo kuendelea kutoa huduma mbalimbali za afya bila kutumia mafuta hayo.

Imetolewa na:

Michael O. John
Kaimu Katibu Mkuu,
Wiza ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

1 comment:

  1. Wale wa haki za binadamu wanalisemeaje hili?
    Mbona hatuwasikii?kwenye ufisadi haki za binadamu,siasa haki za binadamu na hili je?

    ReplyDelete

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger