Jul 24, 2016

Kinana Ajiuzulu, Achaguliwa Tena mbele ya Mkutano Mkuu Kuwa Katibu Mkuu wa CCM

KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana ameandika barua ya kujiuzulu nafasi hiyo kwa Mwenyekiti mpya wa CCM, Rais John Magufuli, lakini Rais amekataa barua yake hiyo.

Badala yake, Rais Magufuli amemtaka Kinana na manaibu katibu wakuu wawili na sekretarieti nzima ya chama hicho, kuendelea na kazi.

Hayo yalisemwa na Rais Magufuli wakati akitoa hotuba ya kushukuru wajumbe wa Mkutano Mkuu Malumu wa CCM, mjini hapa.

“Nimepata barua ya Kinana ya kujiuzulu nafasi yake pamoja na wakuu wa idara za sekretarieti. Nimeamua Kinana na sekretarieti yote waendelee kuwepo.

“Kama kutakuwa na haja baadaye nitaitisha kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) na siyo leo,” alisema Magufuli, akiwatangazia wajumbe hao wa kikao cha Mkutano Mkuu, ambacho ni kikao cha juu cha chama.

Alisema kwa kuwa mkutano huo ndiyo wenye uamuzi wa mwisho kuhusu masuala ya chama, hivyo anawauliza wajumbe kama wamekubaliana na pendekezo lake hilo la Sekretarieti ya chama iendelee.

“Nawauliza wajumbe mnaafiki?” Ambapo wote kwa kauli moja walisema; “Ndiyo.” Magufuli alisema kulikuwa na watu waliokuwa wamejipanga kuchukua nafasi hizo za sekretarieti, lakini “sasa imekula kwao”. Hakutaja watu hao.

Akiongeza kuwa; “Nitaendelea kuwa na Kinana na nina imani yeye na sekretarieti nzima watasimamia vizuri mambo kadhaa niliyoagiza yasimamiwe haraka.”

Magufuli alisema CCM ni chama cha aina yake duniani, kwa kuwa kila upande kuna fursa ya ushauri kutoka kwa wazee wastaafu (huku akiwataja kwa majina), jambo linalofanya kazi iliyo mbele yake kuwa nyepesi.

Rushwa
Akizungumzia kuhusu utendaji wa chama na upitiaji wa muundo wa chama, Magufuli alionya kuwa katika uongozi wake mwanachama atakayetumia fedha kuomba uongozi, hatapita.

Alikumbusha wakati wa kuomba udhamini ili ateuliwe kugombea urais kupitia CCM, kwamba alifika Iringa akakuta Wilaya moja wanachama wote wamenunuliwa, akalazimika kwenda vijiji vya mbali kupata wadhamini.

Magufuli alisema rushwa aliyosema iko ndani ya chama hicho, imekuwa ikiwanyima haki wanachama wengine kugombea na matokeo yake, vyeo vimekuwa vikishikwa na watu wenye fedha na kuacha watu muhimu kwa sababu hawana fedha.

Vyeo kufutwa
Aidha, aliahidi kuongeza maslahi ya wafanyakazi wa chama hicho lakini akaonya kuwa kuna baadhi ya vyeo ambavyo haoni kama vina tija katika siasa za sasa, ambavyo anafikiria kuviondoa.

Alitoa mfano wa makamanda wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), walezi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), washauri wa Jumuiya ya Wazazi na chipukizi, ambao alisema wengi ni wa umri wa kuanzia miaka nane mpaka 15, ambao wanapaswa kuwa shuleni.

Mwenyekiti huyo pia alisisitiza umuhimu wa mwanachama mmoja cheo kimoja na kuonya kuwa hapendi kuona mawaziri, ndio wajumbe wa NEC, ndio makamanda wa vijana na kusema hali hiyo inawanyima cheo wanachama wengine.

Mali za chama
Kuhusu mali za chama hicho, aliagiza sekretari hiyo nayo kuzifuatilia, kuziorodhesha na kuhakiki mali ipi inaingiza mapato yapi na yanakwenda wapi.

Kuhusu ada za wanachama wanaozidi milioni 8.7, ambao Mwenyekiti mstaafu, Jakaya Kikwete alisema kama kila mmoja angelipa ada ya Sh 1,200 kwa mwaka, chama hicho kingepata zaidi ya Sh bilioni nane na kuondokana na ukata wa kutegemea ruzuku, Magufuli aliagiza uhamasishaji wa kulipia ada ufanywe na malipo yawe kwa njia ya kielektroniki.

Kinana
Akizungumza baada ya kurejeshwa madarakani, Kinana alisema baada ya kuandika barua hiyo ya kujiuzulu na hata kuzungumza na Magufuli, amejikuta akigonga mwamba na hivyo anajipanga kuomba tena kupumzika.

Alisema alipokuwa akifanya kazi, kuna wakati alidhani yuko mwenyewe lakini Mwenyekiti Kikwete, alimpigia simu na kumwambia kuwa anamuunga mkono, jambo lililomtia moyo.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger