Jul 15, 2016

Nyaraka Feki za Serikali Zazagaa Kila Kona.....Mpigachapa, Polisi Watoa Onyo kwa Wanaozimiliki

MPIGACHAPA Mkuu wa Serikali, Cassian Chibogoyo amekiri kuwepo kwa nyaraka bandia za serikali katika sekta mbalimbali, nyingi zikiwa za ukusanyaji wa mapato ya serikali, vyeti vya kitaaluma, ndoa na nyinginezo.

Kutokana na hali hiyo, amewaasa wananchi wanaofanya shughuli hizo za kutengeneza nyaraka hizo bandia ambazo ni hatari kwa usalama wa nchi, kuacha kwani wanaendesha oparesheni ya kudumu itakayowabaini na kuchukuliwa hatua kali, ikiwemo kifungo cha miaka 20 jela.

Hivyo amewataka watendaji na wasimamizi katika idara mbalimbali kufanya uhakiki upya wa nyaraka za serikali, kwani zimezagaa sehemu mbalimbali nchini hususan katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), vyuoni na katika maeneo ya kazi.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mpigachapa Mkuu Chibogoyo alisema nyaraka hizo bandia ni pamoja na stakabadhi za malipo, vibali mbalimbali, hati za makontena, leseni za magari pamoja na bima.

Alisema katika oparesheni iliyofanyika mwaka jana ya ‘Okoa Pato la Taifa‘ katika kutafuta nyaraka bandia za serikali, walibaini kuwepo kwa nyaraka za vyeti vya ukaazi au kuzaliwa vinavyomilikiwa na raia wa kigeni, stakabadhi za mapato, leseni za biashara, vyeti bandia vya kitaaluma na vinginevyo.

Alisema nyaraka hizo walizikuta katika vituo vyao vya mauzo na wengine kwenye nyumba zao za kutengenezea uhalifu huo na kubaini kuwa uhalifu huo ni zaidi ya ujambazi kutokana na madhara yake kwa nchi.

Alisema katika oparesheni hiyo walibaini kiwanda cha kutengeneza bidhaa hizo maeneo ya Buguruni katika Manispaa ya llala, Dar es Salaam pamoja na vyeti feki vya Chuo Kikuu cha Kampala (KIU), vitambulisho vya ukaazi ambako kuna raia wa kigeni amepewa cha ukazi akiishi Kariakoo, risiti za usalama barabarani pamoja na shahada za ndoa za Kanisa Katoliki la Mtakatifu Maria Magomeni jijini Dar es Salaam.

Alisema pia walikamata boksi tatu za stika za bima zinazowekwa kwenye magari zikiwa tayari kusafirishwa kwenda mkoani Tanga zikiwa zimewekwa kwenye jokofu bovu lililochakaa karibu na mama ntilie katika maeneo ya Salamander.

“Wananchi wasio waaminifu wanaotaka kupoteza maisha ya wananchi wema na usalama wa nchi ikiwemo kurudisha nyuma maendeleo na uchumi wa nchi, nawapa salamu zangu kuwa mimi na timu yangu tumejipanga kutokomeza vitendo hivyo na tutapigania nchi,” alisema Chibogoyo.

Alieleza kuwa makatazo ya udhibiti wa nyaraka yapo katika Sheria ya Makosa ya Jinai, Sheria ya Ngao ya Taifa, Sheria ya Ushahidi na Sheria ya Usalama wa Taifa, hivyo ukikamatwa na katatasi inayokusudia kutumika kwa udanganyifu, adhabu ni kufungwa miaka saba.

Aidha, alifafanua kuwa Sheria ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1970 inakataza kuwa na nyaraka, mihuri, karatasi maalumu na kumiliki taarifa za serikali isivyo halali na sheria inasema kuwa ni mhalifu na adhabu yake ni miaka 20 jela.

Chibogoyo aliwataka wananchi wema kutoa taarifa pale wanapowabaini watu hao wanaotengeneza nyaraka bandia za serikali pale wanapohitaji nyaraka hizo kwa haraka na ofisi yake itampatia nyaraka halali kwa haraka.

Akizungumzia nyaraka hizo bandia za serikali, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro alisema hali ya nyaraka hizo inatisha kwani ni kubwa kwani nyaraka hizo zote muhimu zipo na zinatumika katika maeneo mbalimbali.

Kamanda Sirro alisema kuna watu wamenufaika kwa nyaraka hizo kama vyeti kutumika kupata ajira hivyo watafuatilia na watawachukulia hata za kisheria wanufaika wote wa nyaraka hizo bandia.

Alisema katika oparesheni waliyoshirikiana na Mpigachapa Mkuu wa Serikali walikamata watu watatu ambao inaonekaan ndiyo mabosi au wakurugenzi wa kutengeneza nyaraka hizo huku wakiwa na mawakala wao katika mikoa mbalimbali kama Mwanza na kwingineko.

Alisema wataendelea kufanya oparesheni ili kuhakikisha suala hilo linakoma kwa kuwakamata wahusika wote.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger