Jul 30, 2016

Polisi wamdanganya Waziri Mwigulu


MAOFISA wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Geita wamemdanganya Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba, kuhusu ukweli wa tukio la kushambuliwa kwa Masanja Shilomero (25) na mwajiri wake ambaye ni raia wa China.

Maofisa hao walimdanganya Waziri Mwigulu ambaye alikwenda mkoani Geita kufuatilia taarifa za kunyanyaswa kwa Masanja ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Nyamitondo, Tarafa ya Butundwe wilayani Geita, kwa kuhofia kuwa akiujua ukweli atawatumbua.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vyake vya kuaminika vilivyo ndani ya jeshi hilo zimeeleza kuwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Wilaya ya Geita (OC-CID), Samweli Kijanga, alikwenda eneo la mgodi akiwa ameambatana na baadhi ya makachero muda mfupi baada ya kuteswa na walinzi na kukutana na uongozi wa mgodi huo.

Julai 6, mwaka huu, Masanja alipigwa na mwajiri wake aliyetambuliwa kwa jina moja la Myo ambaye ni raia wa China baada ya kuomba kupandishiwa mshahara.

Baada ya kupigwa alikamatwa na polisi ambao walimpeleka mahakamani wakiwa wamemfungulia kesi yenye namba CC 278/2016 akituhumiwa kwa kosa la wizi wa mawe.

Tukio hilo lilisambazwa kwenye mitandao ya kijamii na kumfikia Waziri Mwigulu ambaye alifika mkoani Geita Julai 27 na kukutana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kabla ya eneo la mgodi lililo katika Kijiji cha Nyamahuna na baadaye alikwenda gerezani kukutana na Masanja.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Jeshi la Polisi, Kachero Kijanga na timu yake walimkamata Masanja aliyekuwa amejeruhiwa kwa kipigo na kumweka korokoro ya kituo kidogo cha polisi ya Katoro na siku iliyofuata alifikishwa Mahakama ya Mwanzo ya Katoro bila kufikishwa hospitali kwa ajili ya hati ya matibabu (PF3) wala kuchukuliwa maelezo kuhusu unyama aliofanyiwa.

Mmoja wa makachero waliopo mkoani Geita, amelieleza gazeti hili kuwa haiingii akilini kumuona Waziri akiwa na ujuzi wa kuhoji na kubaini dosari akiwazidi polisi ambao wamesomea kazi hiyo.

“Waziri kaja kahoji kwa dakika na kubaini kuna kosa la shambulio dhidi ya anayedaiwa kuteswa na Wachina, kwanini polisi wasigundue?

“Wao upelelezi uliishia kumpeleka mahabusu kwa maelezo ya mlalamikaji na hiyo ilikuwa baada ya OC-CID kukaa faragha na Wachina ambao ni wamiliki wa mgodi huo na walipomaliza kikao chao tulishuhudia kijana wa watu anakamatwa na ikaamuriwa asipewe PF3.

“Alikuwa ameumizwa sana lakini polisi hawakuona hilo wala haja ya kuita mashuhuda wa tukio na kuwahoji tofauti na waziri ambaye kwa muda mfupi aligundua uwepo wa Wachina zaidi ya 50 kinyume cha sheria, lakini tusimlaumu mkuu wa upelelezi maana tunasikia ni maagizo kutoka juu,” alisema polisi huyo.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa baada ya polisi kupata taarifa kuwa Waziri Mwigulu atafika Geita kufuatilia suala hilo, Julai 27, majira ya alfajiri askari polisi wawili ambao majina yao tunayahifadhi kwa sasa wakiwa na Kachero Kijanga walikwenda Gereza la Geita kuomba kuchukua maelezo ya Masanja.

Kwamba polisi hawakuwa na kibali cha kumtoa Masanja gerezani hivyo waliruhusiwa kuchukua maelezo yake wakiwa ofisi za gereza ili kuepuka kutumbuliwa lakini ingetokea Waziri Mwigulu akaitisha jalada la uchunguzi lililofunguliwa dhidi ya Wachina hawakuwa nalo.

Polisi mwingine wa mkoani Geita aliyezungumza na gazeti hili (jina lake tunalihifadhi kwa sababu si msemaji) alieleza kuwa makachero hao walipotoka kuchukua maelezo ya Masanja gerezani ikiwa ni muda mfupi kabla ya waziri kufika, walikwenda kufungua jalada namba GE/RB/5498/2016 la shambulio la kudhuru mwili, mlalamikaji akiwa kijana huyo ambaye mbali na kuumizwa hakupatiwa hata fomu ya matibabu (PF3) na mlalamikiwa akiwa Myo.

“Waziri akiomba jalada hilo hata leo hawabaki kwa sababu litaonyesha ni lini limefunguliwa na atabaini kuwa Masanja alipelekwa gerezani akiwa hana PF3 ambalo nalo ni kosa,” alisema polisi huyo.

Alipoulizwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Geita, Mponjoli Ratson, kuhusu jambo hilo alisema hawezi kutoa taarifa kwa mtu ambaye hamfahamu licha ya kuelezwa mapema kuwa anazungumza na Gazeti la MTANZANIA.

“Mimi siwezi kuzungumza na mtu ambaye simfahamu kwa sababu taarifa nitakazotoa zina athari kwa jamii kama mna mwakilishi wenu huku mwambie aje kuniona ofisini,” alisema Afande Ratson kisha akakata simu.

Takribani wiki moja sasa kumekuwa na hali ya sintofahamu dhidi ya picha zinazoenezwa mitandaoni na kwenye vyombo vya habari zikionesha raia wa Tanzania, Shilomero akiteswa na kufanyiwa vitendo vya kinyama na mwajiri wake ambaye ni raia wa China.

Source: Mtanzania


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger