Aug 18, 2016

Askofu Aelezea Hofu Ushoga Kupandikizwa

ASKOFU wa Kanisa Katoliki Jimbo la Same, Rogatus Kimario amesema ipo mikakati kupitia mitandao ya kijamii kuingiza ndoa za jinsia moja nchini na kusisitiza ikiwa watu wenye kumwamini Mungu hawataweka mikakati katika hilo, zitaingia.

Aliyasema hayo jana alipokuwa akihubiri katika Kongamano la Jubilee ya miaka 35 ya Karismatiki Katoliki Tanzania.

Karismatiki ni moja ya chama cha Kitume katika kanisa hilo. Alisema Wakristo na watu wenye kumwamini Mungu kama hawataweka mikakati ya kupambana na uovu na uvunjifu wa maadili, itakuwa hatari katika jamii.

“Dunia nzima kuna watu wanafanya wanavyotaka. Kama upo katika ‘Whatsapp’ na Facebook kuna vikundi vimejipanga kuingiza ndoa za jinsia moja Tanzania, wapo kimkakati kabisa, tusipoangalia wataingia,” alisema Askofu Kimario.

Akisisitiza kuhusu Wakristo kujipanga kimkakati, alisema lazima kuruhusu neno la Mungu lihubiriwe sana kwa watu wote na kusimamia ukweli.

Alisema uhuru wa dunia kutumia mitandao ya kijamii katika kutekeleza mambo yao unapaswa kuhamia kwa wanaomwamini Mungu ili kuzuia maovu katika jamii.

Akizungumzia Jubilee hiyo ya miaka 35 ya Karismatiki, alisema ni neema za Mungu kufika miaka hiyo na kuwaagiza Wakarismatiki na Wakristo wote kuliishi Neno la Mungu na kutokuwa wavivu kusoma na kuliishi.

Kuhusu Karismatiki, alisema wapo watu wanaweza kudhani imechelewa kuanza ndani ya kanisa, lakini wanapaswa kutambua kuwa wakati wa Mungu ndio sasa na kutakiwa kuruhusu Roho Mtakatifu awatumie.

Juzi akifungua kongamano hilo la Jubilee ya Karismatiki Katoliki Tanzania, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dodoma, Beatus Kinyaiya alimshukuru Mungu na kuwapongeza Wakarismatiki kwa miaka hiyo 35 kuwapo ndani ya kanisa. Aliwataka kuiombea Serikali katika hatua yake ya kuhamia Dodoma na kusisitiza hatua hiyo ni neema kwa Dodoma.

Alisema kongamano hilo limefanyika Dodoma ikiwa ni mpango wa Mungu na kusisitiza kuwa Serikali inatakiwa kuombewa ili lengo hilo litimie na Mungu atukuzwe.

Kuhusu, Kongamano hilo Askofu Mkuu Kinyaiya alisema, katika kumshukuru Mungu Wakarismatiki wanapaswa kumuomba Mungu sana.

Amewataka kumuomba Mungu awape nguvu za kuwaendea wahitaji na ambao hawajaonja neema za Mungu ili wazipate.

Aliwahamasisha wakristo kuacha kulewa pombe na badala yake walewe Roho Mtakatifu maana katika yeye amani, furaha na upendo vinapatikana. Karismatiki Katoliki ni chama cha Kitumendani ya Kanisa kilichoanza nchini mwaka 1981 katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Patris Jimbo la Morogoro kikiwa na idadi ya watu 23 wakiwamo mapadri.

Hivi sasa kimeenea katika majimbo yote nchini. Zaidi ya watu 3,000 wanashiriki kongamano hilo kutoka majimbo yote ya kanisa hilo nchini, nje ya nchi wamo kutoka Marekani, Roma, Canada, Uganda na Kenya, Askofu wa Tanga, Anthony Banzi alikuwepo pia.

Miongoni mwa wageni wanaoshiriki kongamano hilo lililoanza Agosti 16 hadi Agosti 21 ni pamoja na Rais wa Karismatiki kutoka Ofisi ya Baba Mtakatifu, Michelle Moran ambaye anahubiri, wahubiri wengine ni kutoka ndani na nje ya nchi na waumini walei.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger