Aug 9, 2016

Kuhamia Dodoma Ghafla Kutafanyika Bila Madhara?

WIKI chache zilizopita, Rais Dk John Magufuli alifufua ‘ndoto’ za mwaka 1973 za kuhamia Dodoma, zilizoanzishwa na aliyekuwa kiongozi wa nchi hii, Julius Nyerere.  Kama ilivyo kawaida, baada ya kulianzisha jambo hilo, wahusika wengi wakasema mara moja kwamba wako tayari kuhamia huko ambako ni karibu ya kila kona ya nchi.

Tangu Nyerere aamue hivyo na uongozi wake, hivi sasa ni miaka 43 na hakuna lolote la kuonekana lililofanywa katika juhudi za kuhamia Dodoma, ukiacha shughuli za Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Bunge.

Utawala wenyewe wa Mwalimu Nyerere ulikaa madarakani miaka ipatayo 12 baada ya tangazo bila kulitekeleza kikamilifu. Hata hivyo, ugumu wa utekelezaji wa suala hilo waweza kuwa ulichangiwa na uwepo wa vita vya Kagera.

Serikali zilizofuata, za Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete pia zilishindwa kukamilisha jambo hilo zaidi ya kulizungumzia mara chache lakini bila utekelezaji.

Kilichokuwepo ni wahusika kwenda Dodoma kwenye mikutano ya CCM tu na bungeni, baada ya hapo wanarejea Dar es Salaam kuendelea na maisha. Kwa watu waliozaliwa baada ya uamuzi huo na waliokuwa wadogo wakati ukitangazwa, mara zote wamekuwa wakibabaika kila wanapoambiwa Dodoma ndiyo mji mkuu wa Tanzania!

Hivi leo baada ya Rais Magufuli kulifufua suala hilo, siyo tu mamilioni ya vijana wa nchi hii wanafahamu na kukumbuka kwamba makao makuu ya serikali ni Dodoma, bali na watendaji wa serikali, wazee kwa vijana, nao ndipo wanakumbuka kwamba walikuwa na wajibu wa kuhamia Dodoma.

Pamoja na uamuzi huo wenye dhamira njema wa Rais Magufuli ambao umefanywa ‘kwa kushitukiza’, je, jambo hilo litafanyika kwa usalama, hususan kiuchumi?  Uamuzi huo wa kuwahamisha watu laki kadhaa kwenda Dodoma unaweza kweli kufanyika bila madhara kwa jamii ya Watanzania?

Mbali na gharama za kibajeti, je, dhamira kwa wafanyakazi wa serikali kuhamia sehemu hiyo ya nchi ipo ama aliondoka nayo Nyerere?  Hii ni kutokana na ukweli kwamba hata wale waliokuwa wakifanya kazi na Mwalimu wakati huo na wakaendelea kufanya kazi na serikali zilizofuata, walionekana wazi kulipuuza suala hilo na kuendelea kuwekeza mali na makazi yao jijini Dar es Salaam.

Miaka 43 iliyopita ni mingi ya kutosha ambapo tayari serikali ingekuwa imehamia Dodoma, licha ya nchi kutokuwa na rasilimali kubwa kama zilivyofanya nchi nyingine zilizohamisha makao makuu ya nchi zao.  Kilichokosekana katika miaka yote hiyo ni dhamira tu!  Nyerere alipoondoka madarakani, aliondoka na ‘Dodoma’ yake.

Pamoja na uamuzi huo mwema ambao umefanywa mwaka huu wa 2016 ni matarajio ya raia kwamba hautaleta madhara au mzigo mwingine kwa mwananchi wa kawaida ambaye hivi sasa tayari anabeba ‘msalaba’ mzito wa kujinusuru na ukali wa maisha.

Utayari wa kwenda Dodoma ambao kila mhusika amegundua kwamba anao – baada ya kupita miaka 43 – ufanyike salama na kumwacha Mtanzania maskini akiwa salama, kisiasa, kijamii na kiuchumi!

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger