Hivi karibuni kupitia mitandao zilienea taarifa za kifo cha muigizaji huyo aliyewahi kufanya vizuri kwenye filamu ya ‘Sarafina’ amefariki dunia.
Vyombo hivyo vya habari vimeziita habari hizo kuwa ni uongo wa kupindukia. Mtandao wa wasanii nchini Afrika Kusini unaojulikana kama ‘Mzansi’ ulikanusha taarifa hizo za kifo cha Leleti na kusema ni za uongo na umewatoa hofu mashabiki waliopatwa na mshtuko baada ya kupata taarifa hizo.
Msanii huyo alifanikiwa kutembelea Tanzania mapema mwezi Julai mwaka jana kwenye tamasha la ZIFF lililofanyika visiwani Zanzibar na alialikwa kama mgeni rasmi wa tamasha hilo.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment