Aug 16, 2016

Magufuli Amweka Kati Bosi wa UDA, Takururu Waanza Kumchunguza


TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru), imeanza uchunguzi dhidi ya Kampuni ya Simon Group.

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya Rais Dk. John Magufuli, kuviagiza vyombo vya dola kuzirejesha mali za Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza (NCU LTD)  kikiwemo Kiwanda cha New Era kilichouzwa kwa Kampuni ya Simon Group na kurejeshwa NCU.

Akizungumza na MTANZANIA jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Takukuru, Mussa Misalaba,  alisema tayari taasisi hiyo imeanza uchunguzi dhidi ya Kampuni ya Simon Group  ambayo inamilikiwa na mfanyabishara, Robert Kisena.

Pamoja na hali hiyo Misalaba alisema, kinachofanyika sasa ni kuainisha mambo muhimu ikiwemo kuongeza maeneo ya uchunguzi dhidi ya mfanyabishara huyo ambaye pia anaendesha Shirika la Usafiri jijini Dar es Salaam (UDA).

“Kuna mambo muhimu ambayo yameainishwa katika uchunguzi wetu yanamhusu Robert Kisena ambayo yanahitaji muda zaidi ya kuyafanyia kazi ili tuweze kujiridhisha kabla ya kumfikisha kwenye mikono mingine ya sheria,”alisema Misalaba.

Msemaji huyo wa Takukuru, alisema suala la uchunguzi ni hatua ndefu, hivyo basi lazima wahakikishe kuwa mambo yaliyokusudiwa yanakamilika kabla ya kulifikisha katika vyombo vingine ikiwemo mahakamani.

Kampuni ya Simon Group chini ya Mwenyekiti wake Mtendaji, Robert Kisena ndiyo walipewa tenda ya kuendesha Shirika la Usafiri katika Jiji la Dar es Salaam (UDA), ambapo suala hilo hadi sasa bado giza nene limetanda.

Mazonge kwa Simon Group

Pamoja na Rais Magufuli, kutoa agizo la kuhakikisha watu waliopora mali za Chama cha Ushirika cha Nyanza (NCU), wanapatikana na kuzirudisha mali hizo mara moja, huku akiitaja Kampuni ya Simon Group yenye umiliki katika kampuni za UDA na Mabasi ya Haraka Dar es Salaam (UDA-RT), bado kampuni hiyo imekuwa ikiandamwa na matukio mbalimbali yenye utata.

Akiwa jijini Mwanza Rais Magufuli alisema mfanyabiashara Robert Kisena, ambaye ndiye mmiliki wa Kampuni ya Simon Group, alipewa Kiwanda cha New Era kwa Sh bilioni moja lakini fedha aliyolipa ni Sh milioni 32 tu.

Simon Group ni kampuni iliyozaliwa na kampuni ya Simon Agency iliyoanzishwa mkoani Shinyanga na Robert Kisena, kushughulika na ununuzi na uchambuaji wa pamba karibu miaka minane iliyopita.

Hata hivyo kampuni hiyo imekuwa na historia ya kuingia kwenye migogoro mikubwa ya kibiashara na vyama vikuu vya ushirika  katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Vyama ilivyoingia navyo kwenye migogoro ni pamoja na Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Mwanza (NCU) na Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Shinyanga (SHIRECU), ambavyo vinaidai mamilioni ya fedha dhidi ya Kisena kwa madai ya kukiuka mikataba mbalimbali, ikiwamo ya kukodi vinu vya kuchambulia pamba na ununuzi wa rasilimali.

Mkataba wa DART

Licha ya mfanyabishara huyo kuendelea kuaminiwa na hata kudaiwa kukingiwa kifua na baadhi ya vigogo, Serikali bado ilimfuatilia na kunusa harufu ya ufisadi katika mkataba unaoihusisha Kampuni ya Simon Group na Mradi wa Mabasi ya Mwendo wa Haraka (DART).

Aprili 19, mwaka huu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene, ameeleza namna mchezo mchafu ulivyotawala katika zabuni ya mradi huo.

Kwa mujibu wa Simbachawene, zabuni iliyotangazwa ilipaswa iwe katika mfumo wa kimataifa, lakini katika hali ya kushangaza Kampuni ya Simon Group ilianza maandalizi ya kuendesha mradi huo kinyume cha utaratibu.

Simbachawene, alisema Serikali ililazimika kuingilia kati suala hilo kwa lengo la kujiridhisha kuhusu zabuni hiyo.

Alisema katika hatua hiyo, Serikali ilibaini utata katika mkataba wa kampuni hiyo, kwani kila kitu kilikuwa chini ya Simon Group ambao ni wamiliki wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA).

“DART katika kumpata mwekezaji ilitangaza tenda kutokana na maoni mbalimbali ambapo ilitakiwa kutangaza kimataifa (International tender),  lakini ikafanya tofauti na maoni ya watu na kuipa Kampuni ya Simon Group kuendesha mradi huo.

“Kampuni ya Simon Group iliendelea kufanya maandalizi kwa ajili ya mradi na sisi tukaendelea kufuatalia uhalali wa mikataba waliongia na DART ili kuona ni jinsi gani huu mradi uanze lakini tulichokikuta pale kila kitu kipo chini ya Kampuni ya Simon Group kwa kuwa wao ndiyo wamiliki wa Shirika la UDA na wamenunua hisa zote za shirika hilo.

“…ndipo tulipo ulizia zile hisa ambazo haziuzwi bila wana hisa sambamba na kutaka kujua kama fedha zimeshalipwa ndipo napo tukagundua hakujalipwa hata senti tano na haijulikani ni nani kapokea zile hela,” alisema Simbachawene.

Sakata la umiliki wa Shirika la Usafirishaji jijini Dar es Salaam (UDA) ambalo limekuwa likitoa huduma za usafiri katika maeneo tofauti ya Jiji la Dar es Salaam limechukua sura mpya baada ya kuzungumziwa ndani ya Bunge huku Serikali ikishindwa kueleza sababu za shirika hilo kuendeshwa na mtu binafsi.

Hata hivyo wingu dhidi ya Kampuni ya Simon Group, lilikuwa likichukua sura mpya kila kukicha na kuibukia katika Bunge la 10 ambapo wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam walihoji uhalali wa uuzwaji wake.

Source: Mtanzania


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger