Aug 23, 2016

Mkakati Mzito Serikali na CCM Dhidi ya Ukuta Wavuja

Mbowe na Lowassa
MAMBO hadharani. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya taarifa kutoka ndani ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kubainisha kuwa, wanahaha kuikabili Chadema, anaandika Charles William.

Vyanzo vyetu kutoka serikalini na CCM vinaeleza kuwa, miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja na kuwatia hofu wafuasi wa Chadema wanaojipanga kujitokeza kwenye maandamano na mikutano inayoandaliwa kufanyika Septemba Mosi mwaka huu.

Mikutano na maandamano hayo yanafanywa chini ya mwamvuli wa operesheni ya Umoja wa Kupinga Udikteta nchini (UKUTA), jambo ambalo linapingwa na Rais John Magufuli pamoja na Jeshi la Polisi.

Tayari utekelezwaji wa mkakati huo umeanza, ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa taarifa kwenye mitandao ya kijamii kuwa, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema-Taifa hatohudhuria mikutano na maandamano hayo na atakimbilia nje ya nchi.

“Jambo la mikutano na maandamano lipo kikatiba na kiukweli kuzuia ni kukiuka Katiba, jambo linalofanyika ni kujaribu kuwagawa watu.

“Kibaya zaidi ni kuwa, rais kapiga marufuku jambo ambalo hakupaswa kufanya hivyo. Hapa ndipo ugumu unaonekana maana kuna katiba na kauli ya rais inayotoa maelekezo yanayopingana na Katiba,” kinaeleza chanzo hicho kutoka CCM.

Kwa sasa, taarifa zilizopo kwenye mitandao ya jamii zinamtuhumu Mbowe kutaka kutorokea nje ya nchi ili kukwepa kushiriki maandamano na mikutano ya Ukuta iliyopigwa marufuku na Rais Magufuli na polisi.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Mbowe amepanga kusafiri nje ya nchi tarehe 28 Agosti mwaka huu ikiwa ni siku tatu kabla ya kufanyika kwa maandamano na mikutano hiyo.

Taarifa hizo zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii, zimeambatanishwa na kile kilichodaiwa kuwa ni tiketi ya safari hiyo zinadai kuwa, Mbowe anapanga kusafiri ili kukimbia vurugu zitakazotokea Septemba Mosi mwaka huu katika maandamano hayo.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa imeeleza kuwa, ujumbe huo hauna ukweli wowote na kwamba, sababu za kusambazwa kwa ujumbe huo ni nia ovu ya wanaopinga maandamano hayo.

“Mheshimiwa Mbowe yupo mstari wa mbele na anaendelea kutekeleza majukumu yake ya kuhakikisha maazimio ya Kamati Kuu juu ya uanzishwaji na utekelezaji wa operesheni ya Ukuta inafanyika kwa ufanisi.

“Mpaka sasa mwenyekiti anaendelea na vikao vya kimkakati ndani ya Kanda ya Kaskazini kama ilivyopangwa,” imeeleza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa, kile kinachoelezwa kama tiketi ya safari ya ndege ya Mbowe, kimetengenezwa kwa kutumia kompyuta na hakina uhalisia na kusisitiza kuwa Mbowe atashiriki kikamilifu.

Mbali na mkakati huo wa kutengeneza propaganda kuwa viongozi wa kitaifa wa Chadema hawatakuwepo nchini katika siku iliyopangwa kwaajili ya mikutano na maandamano hayo, Jeshi la Polisi kote nchini, linaendelea kukamata watu wote wanaovalia fulana zenye neno; ‘UKUTA’.

Jeshi hilo ambalo limesharipotiwa kukamata watu mbalimbali katika mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam na Mwanza, limeanza pia mkakati wa kufanyisha mazoezi vikosi vyake na kuwaita wanahabari ili waonyeshe mazoezi hayo kwa lengo la kuwatisha wananchi ambao huenda wakashiriki maandamano hayo.

Vikosi vya kutuliza ghasia (FFU), vimekuwa vikialika wanahabari ili kuonyesha mazoezi yanayodaiwa ni ‘kujiweka tayari kukabili uvunjifu wa amani’, Polisi wanaamini kwa kufanya hivyo, wananchi wengi wataogopa kujitokeza katika maandamano ya UKUTA.

CCM pia, imetumia mbinu ya kuwataka vijana wa chama hicho (UVCCM) kutangaza kufanya maandamano nchi nzima, siku moja kabla ya maandamano ya Chadema ili Polisi watangaze kuzuia maandamano hayo na kutengeneza dhana kuwa polisi hawapendelei chama chochote!
Mbinu hii ilitumika pia mwezi Juni, mwaka huu baada ya Chadema kutangaza kufanya mikutano nchi nzima na kisha, Christopher Ole Sendeka, msemaji wa CCM kutangaza kuwa CCM pia itazunguka nchi nzima kufanya mikutano ya kuikabili Chadema.

Jeshi la Polisi lilitumia mwanya huo kudai kuwa, mikutano ya vyama hivyo (CCM na Chadema) itasababisha vurugu na uvunjifu wa amani na hatimaye kuipiga marufuku lakini lengo hasa likiwa ni kuzuia mikutano ya Chadema.

Chanzo:Mwanahalisionline

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger