Jaji Mutungi ameyasema hayo Jumanne hii jijini Dar es salaam alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari ambapo amesema migogoro na changamoto za kisiasa zinazovikabili vyama vya siasa visipojadiliwa vizuri katika meza moja ya majadiliano baina ya pande mbili, inaweza kusababisha kuvunjika kwa amani ambayo imejengwa kwa muda mrefu na waasisi wa taifa.
“Vyama vya siasa nchini vyenye mpango wa kufanya maandamano au mikutano ya kuhamasisha wanachama wake, viache ili kutafuta suluhu za changamoto zinazowakabili kupitia majadiliano hayo ya pamoja,” alisema Mutungi.
Alivitaka vyama vya siasa kutumia mkutano maalumu wa baraza la vyama vya siasa unaotarajiwa kufanyika Agosti 29 na 30 mwaka huu kujadili changamoto zinazowakabili kwa njia ya amani na maridhiano badala ya kufanya maandamano ambayo yanaweza kuhatarisha amani ya nchi.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment