Aug 24, 2016

Mwanafunzi Afukuzwa Shule Kwa Ushirikina

UONGOZI wa Shule ya Sekondari Mwatisi Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, umemfukuza mwanafunzi mmoja (jina tunalo) kwa madai ya ushirikina.

Mwanafunzi huyo anadaiwa kuhusika na kitendo cha baadhi ya wanafunzi shuleni hapo kukumbwa  na matatizo ya kuanguka na mapepo kwa muda wa miezi miwili mfululizo.

Mwanafunzi huyo pia anahusishwa na mzuka wa ajabu uliotokea hivi karbuni, ambapo ulikuwa ukianua vyakula vya watu wakati wakianika nje, huku ukiwakumba wanafunzi wa kike waliokuwa wakikimbilia porini na kuzua taharuki kwa wakazi wa eneo hilo.

Hali hiyo ilisababisha uongozi wa shule hiyo kuitisha mkutano wa hadhara  ulioshirikisha viongozi  wa  dini,  machifu na watu  wengine, lengo likiwa ni kufikia mwafaka  wa sakata hilo.

Furaha Mwakalundwa, Mwinjilisti  wa  Kanisa  la  Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Konde Jimbo la Mwakaleli, alisema kufukuzwa kwa mwanafunzi huyo hakuwezi kuleta tija kutokana na kwamba masuala ya ushirikina hayana uthibisho.

“Siku zote masuala ya ushirikina hayana uthibitisho, hivyo ni vyema hii kazi wangetuachia watumishi wa Mungu, ili tuendelee kuitatua kwa  nguvu za Mungu. Kumwondoa  mwanafunzi  huyo hatuwezi kujua kama kweli ni mhusika au laa,” alisema Mwakalundwa.

Baadhi ya wanafunzi walisema kuondolewa kwa  mwanafunzi mwenzao kumeleta faraja kutokana na hali hiyo kupungua kwa asilimia  90 ukilinganisha na awali.

“Alikua akiingia tu darasani au kila anapokutana na mwanafunzi yeyote walikuwa wakianguka na kupata kama kichaa na kuanguka na kusababisha  wanafunzi na walimu kumchukia,” alisema mmoja wa wanafunzi katika shule hiyo.

Walimu na wanafunzi walikuwa wakimwogopa na kumkimbia  kila anapoonekana ikiwamo kuogopa kumpatia adhabu  wakihofia kukumbwa na sintofahamu hiyo.

Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo, Japhet Boniface, licha  ya  kukiri kuwepo kwa adha hiyo, alisema  kwa sasa hali iko shwari ukilinganisha na alipokuwepo mwanafunzi huyo.

“Vitendo kama hivyo vimekuwa vikijitokeza mara kwa mara kitu ambacho kinatupa wakati mgumu kujua ukweli wa jambo hilo,” alisema.

Mkuu wa  Shule hiyo, Eliza Halinga, alisema mwanafunzi huyo hajafukuzwa shule isipokua uongozi uliamua kumhamishia shule nyingine ili kunusuru hali yake kutokana na kila mwanafunzi kumchukia, hali iliyosababisha wanafunzi na walimu wengi kutofika  shuleni kwa hofu.

“Tuliamua kumwita mzazi wake ili kuongea nae ili tuweze  kumhamishia  shule  nyingine  kwani  kila  mwanafunzi  alikuwa  akimchukia  kutokana na kunguka kwao, pia licha  ya  kunguka  kwao  lakini kila akikutana na wanafunzi wenzake  walikuwa wakianza kuanguka na kujipigapiga,” alisema Halinga.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger