Aug 6, 2016

Yusufu Makamba, Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Anazeeka Vibaya-Mgeja

KHAMIS Mgeja, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga amesema, Yusufu Makamba, Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM anazeeka vibaya, anaandika Charles William.

Mgeja ambaye aliihama CCM mwaka jana na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Meandendeleo (Chadema) amedai kuwa, yupo tayari kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kumchunguza Makamba kwa tuhuma za rushwa na ufisadi.

Madai haya yanakuja ikiwa ni siku mbili mfulululizo tangu Makamba kunukuliwa katika gazeti la Uhuru linalomilikiwa na CCM akimbeza Mgeja kuwa, ni mtu asiyejua lolote kuhusu Katiba ya CCM na kanuni zake licha ya kuwahi kuwa mwenyekiti wa chama hicho ngazi ya mkoa.

“Mzee Makamba anazeeka vibaya sana, mimi nimekuwa kiongozi wa muda mrefu wa chama chake tena katika ngazi mbalimbali na yeye ndiye aliyekuwa akipitisha jina langu ninapogombea. Alikuwa akilipitisha vipi jina la mtu ambaye hajui chochote?” amehoji.

Katika hatua nyingine Mgeja amesema, Makamba hana usafi wala utimamu wa kushambulia watu kwa tuhuma za ufisadi kwani mpaka sasa yeye ni mtuhumiwa mkuu wa ununuzi wa magari ya CCM zaidi ya 200 mwaka 2010 kwa mfumo uliogubikwa na rushwa.

“2010 tukiwa bado CCM, tulihoji Makamba amefanya vipi ununuzi wa Land Cruiser zaidi ya 200 bila kufuata utaratibu na sheria za manunuzi? Makamba hakuwa na majibu na aliagizwa kuleta taarifa kwenye vikao lakini hadi anaondoka nasi tunaondoka hajatoa taarifa,” amesema Mgeja na kuongeza:
“Takukuru ianze kumchunguza Makamba na ufisadi aliofanya ndani na nje ya CCM, huyu si mtu msafi na hili halina ubishi.

“Hata watu walipokuwa wakilalamikia rushwa ndani ya chama kipindi akiwa katibu mkuu, yeye alikuwa akisema, kutoa fedha si rushwa bali ni kuzidiana vipato.”

Pia amesema kama kweli Makamba anajiamini kuwa ni msafi mbele ya umma, aache kutumia gazeti la chama tawala (Uhuru) kushambulia wapinzani na badala yake ajitokeze katika mdahalo wa wazi dhidi ya Mgeja ili aweze kujibu tuhuma za ufisadi alioufanya akiwa katibu mkuu wa CCM.

“Makamba aje katika mdahalo wa wazi, utawala wake mtu asiye na fedha alikuwa hapati nafasi ya ubunge, udiwani au hata ujumbe wa vikao vya juu pia mzee huyu hana maadili ya uongozi, muulizeni kwa nini Mwalimu Julius Nyerere alimfukuza Ukuu wa Wilaya ya Kibondo,” amesema.

Kuhusu tuhuma za ufisadi ambazo Makamba amenukuliwa akimtuhumu Mgeja pamoja na Edward Lowassa, Mgeja amesema; “tumetoka katika dimbwi la rushwa na sisi ni wasafi, unawezaje kuwa mchafu halafu ni mpinzani na serikali hii ya misifa ikakuacha?.”

Makamba alinukuliwa akimshambulia Lowassa tarehe 23 Julai mwaka huu kuwa ni fisadi na ndiyo maana CCM ilimuondoa katika mbio za urais wa chama hicho.

Hata hivyo, Mgeja amepinga akidai Makamba ndiye muasisi na kinara wa rushwa za ndani ya chama hicho.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger