Sep 16, 2016

Kutokuonekana kwa Magufuli Toka Tetemeko, Kunatetemesha!

Na. M. M. Mwanakijiji

Inawezekana kabisa zipo sababu kubwa na za msingi kabisa za kwanini Rais Magufuli, Rais wa wanyonge na mtetezi wa maskini hajaonekana kuzungumza na taifa na sehemu kubwa ya nchi ambayo imekuwa kwenye mshtuko kufuatia tetemeko la ardhi lililopiga Kagera na kurindima sehemu kubwa ya Kaskazini Magharibi mwa nchi yetu Jumamosi iliyopita. Sababu hizi zinaweza kuwa ni za msingi kabisa na zenye maana endapo zitatolewa na watu wote wenye fikra huru wakaweza kukubaliana nazo.

Kuna sababu hata hivyo ambazo zikitolewa – kama zitatolewa – zitawafanya watu waangaliane mara mbilimbili kama wanaozitoa hizo sababu wanazitoa wakifikiria watu wote hawana uwezo wa kufikiri au wanajaribu kulazimisha wasifikiri.

Baadhi ya sababu ambazo haziwezi kutolewa na kwa kweli hazipaswi kutolewa ni kama “hili ni suala la viongozi wa chini, siyo suala la Rais” au “mbona Waziri Mkuu alishaenda na suala la maafa liko chini ya Waziri Mkuu”. Sababu nyingine ambazo hazipaswi kutolewa au hata kujaribiwa kutolewa ni kama kuamua kusema “lilikuwa janga la kawaida tu hawakufa watu wengi”. Wenye kutoa sababu hiyo wanaweza wakasema kuwa ili Rais aonekane na kuzungumzia na kwenda kutoa mahali pole basi janga linapaswa kuwa kubwa sana na lenye vifo vingi sana; kwamba vifo 16 kwenye tukio hili sivyo vya kusitusha sana kwani Watanzania tayari wameshazoea kupata habari za ajali zenye kuua watu wengi.

Wenye kutoa sababu hii wanaweza kuendelea na kusema kuwa tayari ajali za magari zinaua watu wengi sana na siyo mar azote au hata mara moja Rais hajaenda kutembelea maeneo ya ajali. Kwamba, kuna ajali zimeua watu thelathini au ishirini lakini Rais anaishia kutoa pole na rambirambi tu.

Tatizo la sababu hii ni kuwa suala la tetemeko la ardhi ni zaidi ya ajali; ni mojawapo ya matukio makubwa ya nguvu za asili za ulimwengu (natural occurring event) ambayo mwanadamu hajaweza kuyapatia majibu ya kutosha kujiandaa nayo. Kwa maneno mengine, tukio la tetemeko la ardhi siyo “ajali” kwa maana ya ajali bali ni “baa” ni “janga”. Matukio mengine yanatokana na nguvu hizi za asili za ulimwengu ni kimbunga, mafuriko, moto, n.k

Hivyo, kuchukulia janga la tetemeko la ardhi kama ni ajali tu mojawapo ni kutokuwa makini na kutoonesha kujua uzito wa tukio hili. Tetemeko hilo lingepiga hadi kufikiria hata kiasi cha alama namba 7 kwenye kipimo cha Richter basi hadi Mwanza, Mara na inawezekana hata Kigoma kungesikika kilio kama siyo mpaka Dodoma! Hivyo, mshtuko wa tukio hili peke yake kwa eneo kubwa la nchi yetu na lenye watu wengi ingemlazimu Rais mwenyewe kuhakikisha anajitokeza mara moja kuwatuliza wananchi na kuwapa moyo watu waliokuwa kwenye juhudi za kufanya uokoaji.

Lakini pia kuna sababu nyingine ambazo hata zikitolewa bado watu wataona zina shida. Kwa mfano, ni vigumu kuwafanya watu waamini kuwa Rais alikuwa ‘busy’ sana na mambo mengine ya kitaifa – kama kufanya teuzi mbalimbali na kuwaapisha watu mbalimbali – kiasikwamba hakuwa na muda way eye mwenyewe kujionesha kuwa anajali kilichowatokea watu wake. Hivi, watoto wa Kitanzania wanapolala nje, wananchi kukosa makazi ya kudumu, watoto (kwa maelfu) kuwa katika hali ya mshtuko wasijue wazazi wao watafanya nini kuwahakikisha malazi, makazi na vyakula siyo sababu ya Rais mwenyewe kujionesha na kuwatuliza moyo wananchi hawa na familia zao? Siwezi kuona ubusy wowote ule ambao unaweza ukawa sababu au kisingizio cha kwanini Rais hajatokea kuzungumza na taifa na kutembelea Bukoba.

Ni MAKALA NDEFU - kwa wanaoependa kuendelea kusoma Bonyeza HAPA

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger