Sep 1, 2016

Serikali Yashikilia Msimamo Kupinga ndoa za Jinsia Moja

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kushikilia msimamo wake wa kupinga ndoa za jinsia moja,kuongeza uwigo wa uhalalishaji wa utoaji mimba,adhabu ya kifo,kuweka sera ya kutonyonga wanaokutwa na adhabu ya kifo na uridhiwaji wa mikataba ya Kimataifa inayozuia masuala ya utesaji kwa kuwa masuala hayo yanaonekana kutoendana na Katiba na Sheria za nchi, Sera,mila desturi na tamaduni za watanzania ikiwa ni sehemu ya mapendekezo 72 yaliyokataliwa na Serikali wakati wa mapitio ya taarifa ya nchi ya ukuzaji na usimamizi wa haki za binadamu.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Ndugu Gerson Mdemu ameyasema hayoleo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifunga kikao maalumu cha siku mbili cha wadau mbalimbali wa masuala ya haki za binadamu ambapo ameeleza kuwa Serikali ilipokea jumla ya mapendekezo 227 yaliyotolewa na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mwezi Mei 2016 chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum (The Universal Periodic Review).

Mdemu ameongeza kuwa mapendekezo hayo kwa ujumla yalijikita katika majukumu ya Tanzania kwenye mikataba ya kimataifa ,Mifumo ya kikatiba na kisheria,miundombinu ya kitaasisi ya haki za binadamu ,masula ya kisera,ushirikiano na vyombo vya kikanda na kimataifa,utawala wa sheria,uendeshaji haki,masuala ya kulinda haki za msingi za binadamu kama vile haki ya kuishi,haki ya afya,haki za walemavu,watoto,haki ya habari na kujieleza,afya elimu mazingira haki za watu asilia na wakimbizi.

Hata hivyo, Tanzania ilikubali kutekeleza mapendekezo 130 tu kati ya 227 yaliyokuwa yanahusu mchakato wa Katiba,kuijengea uwezo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kuhuisha Sera za nchi ili ziendane na malengo endelevu ya Dunia ,kuandaa taarifa za nchi za utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu na kuziwasilisha kwenye vyombo vya vya umoja wa mataifa kwa wakati.

Vilevile Serikali iliahirisha jumla ya mapendekezo 25 ambayo yalijikita katika marekebisho ya sheria ya Takwimu, 2015, Sheria ya makosa ya mtandao, 2015,ukamilishaji wa Sheria ya Habari, Sheria ya vyombo vya Habari,uandaaji wa mikakati na mipangokazi ya utekelezaji wa msuala ya kuzuia ndoa za utotoni na za kulazimishwa ,upitishaji wa sera mpya mbalimbali ikiwemo ya kutoa vyeti vya kuzaliwa na usajili wake kuwa bure na masuala ya uchaguzi Zanzibar, kwa lengo la kuyapitia tena kwa kina na kushirikisha zaidi wadau ili hatimaye kuweka msimamo stahiki kabla mapendekezo hayo hayajawasilishwa tena Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kwa hatua za mwisho za kupitisha rasmi taarifa ya nchi katika kukuza na kulinda haki za Binadamu.

Aidha, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ametumia fursa hiyo kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kulinda na kukuza haki za bindamu ikiwa ni pamoja na kupokea hoja na maoni ya wadau ili kuboresha taarifa ya nchi itakayowasilishwa katika Baraza la Haki za Binadamu la umoja wa mataifa kabla au ifikapo tarehe 9 Septemba, 2016 na kuwataka watanzania wote kushiriki ipasavyo katika dhana nzima ya kukuza na kulinda haki za bindamu nchini.

Utaratibu wa Mapitio kwa kipindi maalum (The Universal Periodic Review) wa masuala ya haki za binadamu ulianzishwa na Umoja wa Mataifa mnamo mwaka 2006 kwa lengo la kuzifanyia mapitio nchi 192 ambazo ni wanachama wa Umoja wa Mataifa, Tanzania ikiwa miongoni, kwa lengo la kuangalia utekelezaji wa masuala ya kulinda na kukuza haki za binadamu nchini mwao.

Naibu Mwanasheria mkuu wa Serikali Mhe. Gerson Mdemu akiongea na wajumbe kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia wakati wa ufungaji wa kikao kuhusu mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa mataifa, Leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Masuala ya Katiba na Haki za Binadamu Kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bi. Sarah Mwaipopo.

AG2-Wajumbe kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia wakimsikiliza Naibu Mwanasheria mkuu wa Serikali Mhe. Gerson Mdemu wakati wa ufungaji wa kikao kikao kuhusu mapendekezo yaliyotolewa kwa serikali wakati wa majadiliano ya taarifa ya nchi ya utekelezaji wa masuala ya haki za binadamu chini ya mfumo wa mapitio kwa kipindi maalum na baraza la haki za binadamu la umoja wa mataifa, Leo Jijini Dar es Salaam.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger