Oct 25, 2016

ESTER Bulaya Aanza Kupangua Gia za Wasirra Mahakamani


SHAHIDI namba moja wa upande wa wajibu maombi katika kesi namba moja ya mwaka 2015 ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la Bunda Mjini, Estar Bulaya, ameanza kutoa ushahidi wa kutetea ubunge wake katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana.


Katika utetezi wake huo kwenye Mahakama Kuu mjini hapa jana, Bulaya aliulizwa maswali yaliyojikita kwenye ufafanuzi juu ya kutofautiana kwa idadi ya wapigakura waliojiandikisha kwenye hati yake ya ushahidi na idadi iliyojazwa na msimamizi wa uchaguzi katika fomu namba 24(B).

Bulaya aliyetangazwa mshindi wa kiti cha ubunge katika jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana alianza kutoa ushahidi wake mbele ya Jaji Noel Chocha wa Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya, anayesikiliza shauri hilo katika Mahakama Kuu mkoani Mara.

Mbunge huyo alihojiwa na mawakili wa upande wa waleta maombi akiwamo Hajira Mungura, aliyemtaka kuieleza Mahakama kwanini fomu ya matokeo yaliyotangazwa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Lucy Msoffe, ilionyesha idadi ya wapiga kura tofauti na kiapo chake.

Wakili Hajira: Shahidi aeleze Mahakama katika kiapo ulicholeta mahakamani Julai 11, aya ya saba inaonyesha idadi ya wapigakura waliojiandikisha ni 69,369, wakati kielelezo cha ushahidi kilicholetwa mahakamani hapa na msimamizi wa uchaguzi wajimbo hilo, Lucy Msoffe, kinakinzana na idadi ya wapigakura waliopo katika hati yako ya ushahidi huku kikionyesha idadi sahihi ya wapigakura ilikuwa 69,460 tofauti na yako.

Bulaya: Tarakimu zilizopo kwenye kiapo changu zipo sahihi, mimi sijakosea kuandika idadi ya wapigakura waliojiandikisha 69,369, ndivyo ilivyo, msimamizi ndiyo aliyekosea katika kielelezo 24(B), aliandika idadi ya wapigakura 69,460 ambayo siyo sahihi, ninachokiamini mimi ni kile nilichokiandika katika kiapo changu na siyo vinginevyo.

Wakili Hajira: Ieleze Mahakama, msimamizi wa uchaguzi alitangaza idadi ya wapigakura waliojiandikisha walikuwa ni wangapi? Kila mgombea alipata kura ngapi hadi alipomtangaza mshindi?

Bulaya: Mimi sikumbuki idadi waliyopata wagombea wenzangu ninachokumbuka wakati msimamizi anatangaza idadi ya wapigakura waliojiandikisha walikuwa ni 164,794 ambayo ilikuwa imezidi maana alitangaza idadi hiyo ilikuwa ni ya majimbo matatu ambayo ni Bunda Mjini, Mwibala na Bunda Vijijini, ndizo alizomtangazia mshindi wa jimbo la Bunda Mjini lakini niligundua kuwa amekosea, nikamwambia akafanya marekebisho ya kukata hiyo namba.

Wakili Hajira: Shahidi alieze mahakama, wakati wa msimamizi wa matokeo alipokuwa akifanya majumuisho katika chumba, alikuwa akiwashilikisha kufahamu matokeo ya vituo ili muweze kwenda naye sambamba, mlikuwa mkitumia fomu namba 24(B)?

Bulaya: Mimi sikuwa na hiyo fomu namba 24(B) tulikuwa tukiangalia katika TV (Sceen) aliyokuwa akitumia msimamizi wa uchaguzi, hivyo mimi kuwa nayo fomu hiyo niliamini kile alichokuwa akikifanya msimamizi.

Wakili Hajira: Ieleze Mahakama, wakati mnahakiki kura ulisema ulikuwa na wakala wa mgombea wa CCM ambaye ni Janeth Ezekiel, alikwambia alikuwa mahali hapo kwa niaba ya mgombea, Steven Wasira, alikuonyesha kielelezo chochote kinachomuonyesha yuko sahihi mahali hapo au ulishuhudia wakati akiapa?

Bulaya: Mimi nilimwona Janeth Ezekiel ambaye ni mleta maombi wa tatu na wagombea wengine ndani ya ukumbi wa majumuisho, nilipomuuliza alinijibu yeye ni wakala wa mgombea wa CCM, lakini hakunionyesha barua wala kielelezo chochote kinachomwonyesha kuingia humo, wala sifahamu kama aliapishwa.

Jaji Chocha alianza kusikiliza kesi hiyo majira ya saa 3:00 asubuhi kisha akaiahirisha saa 10:28 jioni na itaendelea leo kwa shahidi wa pili kwa upande wa wajibu maombi kutoa utetezi wake.

Shahidi huyo ni msimamizi wa uchaguzi ambaye anatarajiwa kuwasilisha hati ya kiapo chake cha ushahidi.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger