Oct 9, 2016

Mbunge wa Budalang’i nchini Kenya Asimulia Jinsi Rais Magufuli alivyoiteka Kenya


Mbunge wa Budalang’i nchini Kenya, Ababu Namwamba amesema Rais John Magufuli anavuma kwa umashuhuri nchini humo akitajwa kwa namna anavyopambana na ufisadi na kubana matumizi ya Serikali, lakini akasema sifa hizo zitapendeza iwapo huduma muhimu kwa wananchi zitaboreshwa na kuthibitika kwenye tafiti zitakazofanywa.


Akizungumza na waandishi wa habari wakati alipohudhuria mkutano wa demokrasia ulioandaliwa na ACT – Wazalendo jana, Namwamba ambaye pia ni kiongozi wa chama cha Labour of Kenya (LPK), alisema Rais Magufuli ana mtandao Kenya unaomshabikia kwa uongozi wake, ikiwamo harakati zake za kupambana na ufisadi


“Lakini swali kuu katika fikra za  Wakenya wengi ni sasa je, mambo yote tunayoona kwenye vyombo vya habari ni porojo tu ama ile inaitwa propaganda au ni masuala kweli yanayobadili maisha ya Watanzania wengi? Hivyo ingawa sifa za Magufuli zinaenea huku na kule, tungependa kuona mabadiliko halisi hapa Tanzania,” alisema.


“Tungependa kuona kwa mfano takwimu za ufisadi zimepungua. Takwimu za kuonyesha hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida imebadilika huduma kama vile maji, elimu na afya kwamba kweli zimebadilika hilo ndilo la muhimu zaidi, kinyume cha hapo hatutapata sababu ya kuamini au kuona kwamba mabadiliko hayo ni halisi.”


Namwamba, ambaye Julai 7 mwaka huu alijiuzulu ukatibu mkuu wa chama cha ODM kinachoongozwa na Waziri Mkuu mstaafu, Raila Odinga baada ya kutoelewana, alisema siasa za nchi hizo mbili zinakaribiana kwa kuwa mashindano ya wanasiasa yaliyopo nchini ni kama yalivyo Kenya.


 “Kila mara mnapokuwa na uchaguzi hapa sisi hutazama kwa makini sana kwa sababu kuna mengi ya kujifunza.

"

 Hata hivyo, Namwamba alionya kuwa suala la ukabila nchini ni la kutiliwa maanani kwa kuwa kufanya siasa kwa misingi hiyo kumesababisha maafa makubwa ikiwamo mgawanyiko kwa wananchi.


 Alisema siasa nzuri zinazopaswa kuendelezwa nchini ni zile za kuwaleta wananchi pamoja na kama ni mashindano, yawe ya sera, dhana, huduma bora kuliko kumtazama kiongozi wa chama au mgombea kwa kabila lake.


Alisema amekuja nchini kushirikiana na Kiongozi wa ACT – Wazalendo, Zitto Kabwe kupanda mbegu ya ushirikiano na kwamba atashiriki kuhamasisha vijana kutambua viongozi walioweka historia wakiwamo Mwalimu Julius Nyerere na Nelson Mandela.


 Zitto akizungumza katika mkutano huo alieleza kuwa chama chake kinaunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Magufuli katika kurejesha nidhamu ya kazi kwa watumishi wa umma na kupambana na ufisadi.


 “Lakini tungependa kuona hatua zinachukuliwa zaidi ikiwa ni pamoja na kuwafikisha kwenye vyombo vinavyohusika watumishi 154 wachukuliwe hatua zinazostahili.Pia suala la Escrow nalo linapaswa kuchukuliwa hatua na mengine mengi.” 


Mshauri wa ACT, Profesa Kitila Mkumbo aliwasilisha mada ya; “Sisi ni kina nani?” akilenga kuwaelimisha wanachama wake kujihusisha na maisha ya watu, kwa kuwa kushughulikia changamoto na matatizo ni mchakato unaoendelea iwe ndani au nje ya Serikali.


“Chama chetu siyo cha kuvizia makosa ya Serikali ndipo tufanye siasa, tunajipanga kushindanisha ubora wa sera, kina itikadi yake kamili, ni jukumu letu kukosoa Serikali lakini jambo la muhimu ni kuonyesha tuna vitu gani bora kwa wananchi.”


 Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba, Deus Kibamba ambaye alitoa mada iliyohusu masuala ya Katiba alisema mchakato wa Katiba hauna budi kurudishwa nyuma kwa hatua moja hadi kwenye rasimu.


“Kuna mambo mengi yamejitokeza ambayo yamewachanganya wananchi, hivi sasa wengi wanatofautiana hawajui uliishia kwenye hatua gani. Pia, hali iliyojitokeza kule Zanzibar ambapo wakati unajadiliwa awali kulikuwa na Serikali ya umoja ambayo sasa haipo. Kuna mambo mengi ambayo tumekuwa tunarudi nyuma hatua tano kisha kwenda mbele hatua mbili.”


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger