Oct 7, 2016

Msajili Amtambua Lipumba, Maalim Seif

OFISI ya Msajili wa Vyama ya Siasa imetoa orodha ya vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu na viongozi wa vyama hivyo ambako inasisitiza kuwa Profesa Ibrahim Lipumba ndiye Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) na Katibu Mkuu ni Seif Shariff Hamad.

Kwa mujibu wa barua hiyo ya Oktoba 4, 2016 iliyoandikwa kwenda kwa makatibu wakuu wa vyama vyenye usajili wa kudumu, Profesa Lipumba ambaye Baraza Kuu la chama hicho limetangaza kumfukuza uanachama, anaonekana kwenye orodha hiyo kama Mwenyekiti wa CUF.

Jina la Profesa Lipumba ambaye alitangaza kujiuzulu nafasi hiyo mwaka jana, limerejeshwa kwenye orodha na Msajili wa Vyama ya Siasa baada ya yeye mwenyewe kutangaza kutengua barua yake ya kujiuzulu.


Kwa hatua hiyo ya Msajili, uteuzi wa Julius Mtatiro ambao umefanywa na Baraza Kuu kuongoza Kamati ya Uongozi ya CUF hautambuliwi na Ofisi ya Msajili wa Vyama ya Siasa.

Uamuzi huo wa Ofisi ya Msajili umekuwa unalalamikiwa na upande unaoongozwa na Maalim Seif kuwa unakiuka Katiba ya CUF wakati yeye akisisitiza kuwa yuko sahihi kumtambua Profesa Lipumba kwa mujibu wa Katiba hiyo.

“Baada ya zoezi la uhakiki na utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa mengine ya sheria ya vyama vya siasa kwa vyama vyenye usajili wa kudumu kukamilika, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imehuisha taarifa za vyama vya siasa zilizopo katika orodha ya vyama vya siasa.

“Hivyo pamoja na barua hii, nawasilisha orodha ya vyama ya siasa ilivyo leo tarehe 4 Oktoba 2016 kwa taarifa na kumbukumbu zenu. Endapo kuna taarifa ambayo siyo sahihi mnaombwa kuwasiliana na ofisi ya msajili wa vyama ya siasa mapema iwezekanavyo ili irekebishwe,” ilisema barua hiyo.

Barua hiyo imevitaja vyama 22 ambayo vina usajili wa kudumu na chama cha mwisho kusajiliwa ni Alliance for Change and Transparency (ACT-Wazalendo) ambacho viongozi wake ni Anna Mghwira ambaye ni Mwenyekiti na Katibu Mkuu ni Juma Sanani.

Chama hicho kilipata usajili Mei 5, 2014. Vyama vingine ni Chama Cha Mapinduzi ambacho Mwenyekiti wake ni John Magufuli na Katibu Mkuu ni Abdulrahman Kinana. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mwenyekiti wake ni Freeman Mbowe na Katibu Mkuu ni Dk Vincent Mashinji.

Chama kingine ni Union for Multiparty Democracy (UMD) ambacho Mwenyekiti wake ni Kamana Masoud na Katibu Mkuu ni Moshi Kigundula. Chama cha National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi) Mwenyekiti wake ni James Mbatia na nafasi ya katibu iko wazi.

Mwenyekiti wa Chama cha National League for Democracy (NLD) bado kinaonesha kuwani marehemu Oscar Makaidi na Katibu wake ni Tozy Matwanga, United Peoples’ Democratic Party (UPDP) Mwenyekiti ni Fahmi Dovutwa na Katibu Mkuu ni Hamadi Ibrahim, National Reconstruction Alliance (NRA) Mwenyekiti ni Marsheed Humudi na Katibu Mkuu ni Simai Abdullah.

Chama cha Haki na Ustawi (CHAUSTA) kwa mujibu wa orodha hiyo Mwenyekiti ni James Mapalala, Katibu Mkuu ni Mwaka Mgimwa, Chama cha Democratic Party (DP) nafasi ya Mwenyekiti iko wazi na Katibu Mkuu ni Georgia Mtikila. Chama hicho kilikuwa kinaongozwa na Mchungaji Christopher Mtikila ambaye alifariki kwa ajali ya gari.

African Progressive Party of Tanzania (APPT-Maendeleo) kinaongozwa na Mwenyekiti wake wa siku nyingi Peter Mziray, Katibu Mkuu ni Nziamwe Samwel, Jahazi Asilia kinaongozwa na Kassim Bakari Ali na Katibu Mkuu ni Mtumweni Jabir Seif, Sauti ya Umma (SAU) Mwenyekiti ni Paul Kyara na Katibu Mkuu ni Ali Kaniki.

Tanzania Farmers Party (AFP) kinaongozwa na Said Soud Said na Katibu Mkuu ni Rashid Ligania Rai, Chama cha Kijamii (CCK) Mwenyekiti wake ni mwanahabari wa siku nyingi Constantine Akitanda na Katibu Mkuu ni Renatus Muabhi, Alliance for Democratic Change (ADC) Mwenyekiti ni Hamad Rashid Mohamed na Katibu Mkuu ni Doyo Hassan Doyo wakati Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kinaongozwa na Hashim Rungwe na Katibu Mkuu ni Ali Omar Juma.

CHANZO: HABARI LEO

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger