Oct 27, 2016

Msimamizi wa Uchaguzi Bunda Akiri Kukosea Kura


Msimamizi mkuu wa uchaguzi katika Jimbo la Bunda Mjini mwaka 2015, Lucy Msoffe amekiri kufanya makosa ya kuandika idadi ya wapigakura wakati wa kutangaza mshindi wa nafasi ya ubunge.

Akizungumza katika mahojiano na wakili wa upande wa mjibu maombi wa pili, Tundu Lissu katika kesi namba moja ya kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo hilo inayoendelea mjini Musoma jana, msimamizi huyo alisema siku ya kutangaza matokeo alikuwa hajalala tangu tarehe 24 usiku hadi muda ambao alitangaza matokeo saa 11:11 jioni.

Alisema kutokana na uchovu mwingi ndiyo maana akawa anakosea kuandika idadi ya wapigakura mara mbili mfululizo wakati wa kutangaza mshindi. Sehemu ya mahojiano yao ilikuwa:

Lissu: Ieleze Mahakama kuwa wewe ulikuwa msimamizi wa uchaguzi wa majimbo matatu ya Wilaya ya Bunda, jimbo la Mwibara, Bunda na Bunda Mjini kweli si kweli.

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni kweli.

Lissu: Wewe ulikuwa msimamizi wa majimbo matatu ya uchaguzi katika wilaya hiyo kweli si kweli.

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni kweli.

Lissu: Ieleze Mahakama umeshika nafasi ya ukurugenzi kwa muda gani?

Shahidi: Nimekuwa mkurugenzi tangu mwaka 2007 na nimekuwa mkurugenzi katika sehemu mbalimbali hadi 2016.

Lissu: Ulikuwa msimamizi wa Uchaguzi Mkuu 2015 kwa mara ya pili kweli si kweli?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni sahihi.

Lissu: Ni kweli kwamba Jimbo la Bunda lilikuwa na vituo vya kupigia kura 467?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji kumbukumbu yangu ninakumbuka kuwa idadi ya vituo ilikuwa 468.

Lissu: Ni kweli kabisa kuwa baadhi ya vituo hivyo viko visiwani?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni kweli.

Lissu: Mweleze mheshimiwa Jaji siku ya tarehe 24/10/205 ulilala saa ngapi?

Shahidi :Mheshimiwa Jaji siku ya tarehe 24/10/2015 nililala saa nane au tisa hivi usiku.

Lissu: Tarehe 25/10/2015 uliamka saa ngapi?

Shahidi: Tarehe 25/10/2015 niliamka saa 11:30 alfajiri Lissu: Tarehe hiyo ulianza kupokea masanduku ya kupigia kura kuanzia saa ngapi?

Shahidi: Nilianza kupokea masanduku ya kupigia kura saa 11:30 jioni hadi tarehe 26/10/2015 saa saba mpaka nane usiku.

Lissu: Ni kweli zoezi la kuhesabu kura lilianza tarehe 26/10/2015 asubuhi?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji, ndiyo zoezi lilianza saa 5:11 asubuhi.

Lissu: Ni kweli zoezi hilo lilienda hadi saa 11:11 jioni?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ndiyo.

Lissu: Kwenye fomu yako namba 24B ya kutangazia matokeo kuna namba 164,794 imefutwa futwa. Kweli si kweli?

Shahidi : Mheshimiwa Jaji ni kweli.

Lissu: Hiyo namba iko kweli idadi ya waliojiandikisha kwenye daftari?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni kweli.

Lissu: Pembeni mwa namba hiyo iliyofutwa kuna namba 69,460 kweli si kweli?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni kweli.

Lissu: Shahidi kielelezo P2 kina orodha ya vituo vya kupigia kura uliyowapatia vyama vya siasa kweli au si kweli?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni kweli.

Lissu: Kielelezo hicho kilikuwa na idadi ya wapiga kura, kweli si kweli?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni kweli.

Lissu: Mwishoni mwa hiyo karatasi uliyoshika kuna idadi ya wapigakura wa jimbo zima la Bunda Mjini wangapi?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji idadi ya wapigakura katika Jimbo la Bunda ni 69,369 .

Lissu: Idadi ya 164,794 ilikuwa ya kimakosa kweli si kweli?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji kweli.

Lissu: Hizo tarakimu zilizokosewa za 164,794 ulizitoa wapi?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji nilizitoa kwenye idadi ya waliojiandikisha kwenye daftari kwenye majimbo matatu.

Lissu: Eleza idadi ya wapigakura kila jimbo.

Shahidi: Idadi ya kila jimbo ilikuwa kama ifuatavyo, Mwibara 59,436, Bunda Mjini 69,369 na Bunda ni 35,898.

Lissu: Jumla yake ni ngapi?

Shahidi: Jumla ni 164,794.

Lissu: Mbona hesabu yako ni tofauti na yangu? Hapa inaonyesha ni 164,703.

Shahidi: Mheshimiwa Jaji labda nilikuwa nimekosea

Lissu: Ilikuaje ukafuta 164,794 nini kilitokea?

Shahidi: Baada ya kujaza hii fomu na mawakala kusaini hii fomu nilienda kutangaza matokeo na wakati ninatangaza ndiyo wakaniambia kuwa nimekosea na nikafuta.

Lissu: Ulipofuta uliandika namba ngapi?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji niliandika 69,460.

Lissu: Hiyo namba mpya uliyoiandika ya 69,460 vilevile ulivikosea kweli si kweli.

Shahidi: Mheshimiwa Jaji ni kweli nilikosea.

Lissu: Sasa shahidi mueleze mheshimiwa jaji hayo makosa yaliyojitokeza mara mbili katika kujaza fomu yalitokana na nini?

Shahidi: Mheshimiwa Jaji makosa hayo yaliyotokea mara mbili katika kujaza fomu yalitokana na uchovu niliokuwa nao.

Hadi tunakwenda mitamboni, kesi hiyo ilikuwa inaendelea.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger