Mkuu wa wilaya ya Ilala Sofia Mjema akizungumza na waandishi wa habari amesema zoezi hilo litaanza mapema asubuhi na kuwataka wafanyabiashara hao kwenda katika maeneo waliyopangiwa ikiwemo soko Mburahati, Kigogo Sambusa na maeneo rasmi yaliyoainishwa.
Katika eneo la kariakoo chanel ten imeshuhudia adha kubwa kwa wananchi wanaotembea kwa miguu ambapo wanalazimika kupita katikati ya barabara ya magari ya mwendo wa haraka huku magari hayo yakipita kwa kasi na kuhatarisha maisha yao kutokana na wafanyabiashara hao kupanga biashara zao katika njia za watu wanaotembea kwa miguu.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment