Oct 20, 2016

Wanafunzi chuo kikuu cha Dar, wagoma kusaini fedha ya kujikimu (Boom)

KITENDO cha wanafunzi wa vyuo vikuu kunyimwa mikopo huku wachache waliopewa wakipunguziwa fedha za kujikimu kimeichukiza Serikali ya Wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO) na kuamua kuwazuia wanafunzi wa mwaka wa kwanza kusaini malipo ya fedha hizo

Serikali ya Tanzania, kupitia kwa Abul-Razaq Badru, Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu (HESLB) imetangaza kutoa mikopo kwa wanafunzi 21,500 tu kati ya 88,000 wa mwaka wa kwanza, sawa na asilimia 24.4 ya walioomba mikopo hiyo mwaka wa masomo 2016/2017.

Serikali pia imeanzisha utaratibu mpya wa kutoa fedha za kujikimu kwa mwanafunzi kulingana na asilimia yake ya mkopo. Mfumo ambao umesababisha baadhi ya wanafunzi kupewa Sh. 350/= kama fedha ya kujikimu kwa siku, tofauti na mwaka jana ambapo wanafunzi wote wenye mikopo walikuwa wakipewa Sh. 8,500/= kwa siku.
View attachment 421402

Erasmi Leon, Rais wa DARUSO, akitoa msimamo wa Serikali ya wanafunzi wa UDSM amesema wanapinga mfumo huo mpya wa HESLB na kwamba wanafunzi wa mwaka wa kwanza hawatasaini fedha hizo mpaka pale kasoro hiyo itakaporekebishwa.

“Kwa majina ambayo yameshatoka hakuna kwenda kusaini mpaka pale tutapowaruhusu na tutawaruhusu mara baada ya kufanikisha haki yenu. Nawasihi tuwe wamoja, tunaenda wawakilishi ili tusikilizwe na wajue tuna hoja gani.

Tuna kila sababu ya kusikilizwa na tukinyimwa nafasi tutaenda tukiwa wengi zaidi. Tutakapowahitaji muda wowote, kwa lolote naomba tushirikiane, twende pamoja, tusimame na tumalize pamoja kuhakikisha tunapata 8,500/= kwa kila mwanafunzi kama fedha ya kujikimu kwa siku,” amesema Erasmi.

Alikuwa akiwahutubia wanafunzi wa mwaka wa kwanza huku akitangaza uamuzi wa kuwachukua baadhi ya wanafunzi na kwenda makao makuu ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ikiwa ni hatua yao ya kwanza ya kutafuta suluhu kabla ya kuchukua uamuzi mkubwa zaidi.

Kwa upande wake Kasunzu Eliudi, Waziri wa Mikopo DARUSO, ameieleza *MwanaHALISI Online* kuwa, utaratibu mpya wa serikali utafuta ndoto ya maelefu ya wanafunzi kupata elimu ya Chuo Kikuu.

“Hatuwezi kukubaliana na uonevu huu, watoto wa masikini hawataweza kuendelea na masomo, wanapewa mpaka Sh. 500/= ya chakula na malazi kwa siku. Elimu ndiyo chimbuko la ukuaji wa sekta zote, lazima serikali iwekeze, kuwatelekeza wanafunzi ni kulitelekeza taifa,” amesema.

Mpaka sasa serikali imetoa mikopo kwa wanafunzi 11,000 tu nchi nzima na imeahidi kuongeza wanafunzi 10,500 katika awamu nyingine ili kufanya idadi kamili ya waliopewa mikopo ifikie 21,500 tu kati ya 88,000 walioomba mikopo.

Hata hivyo licha ya kutangaza kutoa mikopo kwa wanafunzi 3,996 kati ya 8,000 wa mwaka wa kwanza wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, HESLB imepeleka majina 949 tu chuoni hapo jambo linalosababisha wanafunzi wengi washindwe kujisajili na kuanza masomo.

“Wanafunzi wamezagaa tu, hawajui pa kwenda na hawana fedha za kujikimu mpaka sasa. Wamekuwa kama kuku waliopotea banda lao huku giza likizidi kutanda,” amesema Kasunzu.

Mpaka tunaenda mitamboni, msafara wa wanafunzi wa UDSM ukiongozwa viongozi wa serikali pamoja na wawakilishi wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza walikuwa wamefika wizara ya elimu huku wakikwama kuonana na Waziri Profesa Joyce Ndalichako.

“Tumeambiwa Waziri na Naibu wote hawapo, sisi tunahitaji kuzungumza na mtu anayeweza kufanya maamuzi na tunataka kwenda Ofisi ya Waziri Mkuu ingawa kwa sasa Katibu wa wizara ya Eimu ametuomba tuzungumze na yeye kwanza,” amesema Boniface Emmanuel, Waziri Mkuu wa DARUSO.

Wakati fukuto hili likiendelea UDSM na hatima yake ikiwa bado haijajulikana, taarifa ambazo bado hazijathibitishwa zinasema kuwa Ijumaa ya kesho Rais John Magufuli atakuwa mgeni rasmi katika sherehe ya maadhimisho ya miaka 55 ya chuo hicho.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger