jamaa mmoja tupo naye mtaani amechana na mkewe kwa kisa cha kutembea na kumtia mimba msichana wake wa kazi. yule mama amesema wazi hawezi mrudia mumewe hata kwa bunduki.anasema ni uchavu na kuishiwa sera kwa mumewe.pamoja na jamaa kuwa ni tajiri sana mke ameamua kuacha mali zote na kwenda kupanga chumba kimoja kuanza maisha mapya. amebembelezwa sana. sana na watu wa aina yote na jamaa amesema hata yupo tayari kumnunulia gari alitakalo kumfanya amsamehe.mke kamwambia atakuwa na mdanganya maana hatoweza tena kufanya naye mapenzi so ndo yao automatically itakuwa imekufa.
nikajiuliza inakuaje mwanaume mzima unamrubuni dada wa kazi unamalalia? unampumulia? unamwegamia? nao ni binadamu sikatai basi ukiona hali ipo hivyo si mwondoe kazini then mkafanyie uhuni wenu huko? nyumba moja unakuka dada wa kazi?kweli??????
dada zangu nawaambia usikubali kuishi na mwanaume aliyeishiwa sera kiasi hicho. ambaye anategemea mteremko..huyu ni hatari maana sasa amekuwa kama fisi. hachagui habagui atakayezikwa anye hamjui.
kuna wanaume kweli wao hawana viwango vya mwanamke wa kutembea naye. awe mweupe,mweusi,mnene,mwembamba,mrefu,mfupi yaani yeyote yule ili mradi tu awe na nani.....wanaume wa namna hii ni wenye ulemavu wa mbaya sana na hawa mara nyingi wanakuwa ni mafisi. lazima mwanaume uwe na kigezo. mwanaume wa namna hii anaweza kutembea na hata ndugu zako au zake.
jaman njaa hii njaa gani? hadi mnakula mizoga? na nawapenda kuwapa tahadhari hii. HAKUNA BINADAMU RAHISI KUPATA MIMBA KAMA HOUSE GIRLS. MIMBA ZAO ZIPO KARIBU SANA. SIJUI WAMEUMBWAJE? na utafiti unaonesha ni nadra sana kupata HOUSE GIRL MGUMBA. msije sema sikusema
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment