Oct 7, 2016

Watoto 22 na Mwalimu wao wa Madrasa Watiwa Mbaroni Kwa Madai ya Kujifunza UGAIDI

JESHI la polisi mkoani Pwani ,limewakamata watoto 22 wa madrasa ya Arahma pamoja na mwalimu wa madrasa hiyo Ashura Said(47) ambae alikuwa akiendesha mafunzo ya kigaidi kwa watoto hao,huko Kimarang’ombe ,kata ya Nianjema ,Bagamoyo.

Aidha jeshi hilo limefanikiwa kukuta bomu moja la moshi lenye namba G2020c.SS-STCS katika makazi anayoishi mwalimu huyo .

Akizungumzia tukio hilo,kamanda wa polisi mkoani Pwani,Boniventure Mushongi,alisema Ashura anashikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi kuhusiana na kuhusika kuendesha mafunzo ya kigaidi kinyume na sheria.

Alieleza kuwa taarifa hiyo ilitolewa na raia wema juu ya mwenendo wa mwalimu huyo wa madrasa na baada ya kumfanyia upekuzi polisi walifanikiwa kukuta na bomu moja la moshi.

Kamanda Mushongi,alisema uchunguzi wa awali ulibaini makazi hayo yanamilikiwa na taasisi ya kiislamu iitwayo Akha Laagul Islam,iliyosajiliwa kwa lengo la utoaji huduma kwa watoto yatima kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Dar es saalam ,Tanga,Handeni,Mlandizi na Bagamoyo kwa mkoa wa Pwani.

“Badala yake watoto hao wamekuwa wakitumika kwa mafunzo yasiyofaa kwa watoto wa kituo hicho”alisema kamanda Mushongi.

Hata hivyo alisema jeshi la polisi limewamakata watoto 22 ambao walikuwa wakijaribu kukimbia ambao kati yao 16 ni wakike na 6 ni wa kiume kwa ajili ya uchunguzi wa tukio.

Katika tukio jingine ,Bakari Saidi (45)mkazi wa Kimanzichana Kusini ,wilayani Mkuranga, ameuwawa kwa kupigwa risasi kifuani upande wa kulia na kutokea chini ya bega la kushoto ,mgongoni na watu wasiofahamika.

Katika tukio hilo,Omar Ally (55)ambae ni afisa mtendaji wa kijiji cha Kimanzichana Kusini,alijeruhiwa kwa kupigwa risasi kwenye mkono wake wa kushoto na amelazwa katika hospitali ya wilaya hiyo kwa matibabu.

Kadhalika katika eneo la tukio kumekutwa maganda mawili ya risasi yanayotumika kwenye silaha ya SAR/SMG .

Kamanda Mushongi alisema watu hao walivamia katika ofisi ya serikali ya kijiji cha Kimanzichana Kusini na kufanya mauaji hayo ambapo  mtu huyo alifariki dunia  na mwingine mmoja kujeruhiwa.

Anasema tukio hilo limetokea octaba 5 mwaka huu katika kitongoji cha Ukwama kata ya Kimanzichana tarafa ya Mkamba wilayani hapo.

“Wakati marehemu akiwa anajaza fomu za mkopo wa benki ya  akiba  Commerce bank(ACB),ghafla walitokea watu wawili wakiwa na silaha mbili na kuanza kuwafyatulia risasi na kutoweka kusikojulika wakitumia usafiri wa pikipiki"alisema kamanda Mushongi.

Kamanda huyo alifafanua kuwa mwili wake umehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya Mkuranga na utakabidhiwa kwa ndugu zake kwa ajili ya mazishi mara baada ya uchunguzi kukamilika.

Jeshi hilo limewahakikishia wananachi wote usalama wao na kwamba linapambana kwa nguvu na wale wenye nia ya kuwatia hofu wananchi,kwani hawataweza kufanikiwa katika mipango yao .

Limewaasa wananchi kuwafichua wahalifu ambao ni sehemu ya jamii wanapoishi badala ya kuoneana muhali pamoja na kutoa taarifa pale wanapobaini kuna watu ama raia asiyemwema

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger