Nov 11, 2016

ASKARI Wapandishwa Kizimbani Kwa Kuwaingilia Kimwili kwa Nguvu Wanafunzi wa Kidato cha Nne

ASKARI wawili waliofukuzwa kazi na Jeshi la Polisi mkoani Mbeya wamepandishwa kizimbani jana katika Mahakama ya Mkoa wa Mbeya wakikabiliwa na jumla ya mashitaka 13 waliyoyatenda dhidi ya wanafunzi wa kidato cha nne likiwamo la kuwaingilia kimwili kwa nguvu.

Waliopandishwa kizimbani ni Konstebo Petro Magana aliyekuwa wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mbeya na Konstebo Lucas Ng’weina wa Wilaya ya Kipolisi Mbalizi.

Katika kesi namba 147 ya mwaka 2016, ilidaiwa na Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Catherine Paul mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Mbeya, Zawadi Laizer kuwa washitakiwa walitenda makosa hayo Novemba 4, mwaka huu saa tano usiku katika Shule ya Sekondari Isuto iliyopo wilayani Mbeya.

Mwendesha Mashitaka aliiambia mahakama hiyo kuwa katika shitaka la kwanza la kosa la udhalilishaji wa hali ya juu linalomkabili Konstebo Petro pekee, siku ya tukio mshitakiwa alijaribu kumwingilia kimwili mwanafunzi (jina linahifadhiwa) mwenye umri wa miaka 14 huku pia akimdhalilisha mwanafunzi huyo jambo ambalo ni kinyume cha sheria Kifungu namba 138 A cha Kanuni ya Adhabu.

Alisema kwa shitaka la pili la kosa la udhalilishaji wa hali ya juu pia linalomkabili Konstebo Lucas peke yake, siku ya tukio mshitakiwa alijaribu kumwingilia kimwili mwanafunzi (jina linahifadhiwa) mwenye umri wa miaka 16 na kisha kumdhalilisha jambo ambalo pia ni kinyume cha sheria Kifungu namba 138 A cha Kanuni ya Adhabu.

Mwendesha Mashitaka huyo wa Serikali alizidi kubainisha kuwa mashitaka mengine yote kuanzia shitaka namba tatu hadi 13 yanayohusu shambulio yanawakabili washitakiwa wote wawili kwani kwa pamoja waliwashambulia wanafunzi 11 wa kidato cha nne kwa kuwachapa viboko sehemu mbalimbali za miili yao jambo ambalo ni kinyume cha Sheria Kifungu cha 240 cha Kanuni ya Adhabu.

Aliwataja wanafunzi walioshambuliwa na askari hao kuwa ni Neema Mabalanjo, Vicky Mwaya, Tumpe Jonas, Ombeni Tuonee, Lutabite Landa, Jane Msukulu, Zulfa Julius, Atupole Boniface, Betha Joseph, Blandina Mwaigaga na Zainabu Leonard.

Hakimu Mkazi Laizer aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 14, huku akisema dhamana kwa washitakiwa wote wawili iko wazi kwa masharti ya kila mmoja kutosafiri nje ya Mkoa wa Mbeya bila idhini ya mahakama hiyo na pia kila mshitakiwa kuleta mdhamini mmoja ambaye ni mtumishi wa umma ambaye ataweka dhamana ya malikauli isiyopungua thamani ya Sh milioni saba.

Hadi kesi hiyo inaahirishwa mahakamani hapo washitakiwa wote ambao kwa pamoja wanatetewa na Wakili wa Kujitegemea, Josephat Kazeula walishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kutakiwa kurudishwa rumande.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger