Nov 12, 2016

Benki Yaomba Mahakama iizuie Tanesco kuilipa IPTL, Yastukia Escrow

Tanesco
Benki ya Standard Chartered Limited ya Hong Kong (SCB-HK) imefungua maombi Mahakama Kuu ikitaka, pamoja na mambo mengine, Shirika la Umeme (Tanesco) lizuiwe kuilipa kampuni ya uzalishaji nishati hiyo ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL).

Badala yake, SCB-HK inaomba malipo hayo yahifadhiwe mahakamani hapo hadi Tanesco itakapolipa dola 148 milioni za Kimarekani (sawa na zaidi ya Sh320 bilioni) kwa benki hiyo kama Mahakama ya Kimataifa ya Utatuzi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) ilivyoagiza mwezi Septemba, tofauti na ilivyokuwa wakati wa mgogoro wa Tanesco na IPTL wakati fedha zilipowekwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Katika uamuzi wake uliotolewa Septemba 12, 2016, ICSID iliamuru Tanesco iilipe SCB-HK dola 148.5 milioni, pamoja na riba ya asilimia 4, kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia Septemba 30, 2015, hadi malipo yote yatakapokamilika.

Uamuzi wa ICISD ulikuja takriban miaka mitatu baada ya Serikali kuidhinisha malipo ya takriban Sh306 bilioni kutoka akaunti ya escrow iliyofunguliwa na Tanesco kwa kushirikiana na IPTL kusubiria uamuzi wa Mahakama Kuu kuhusu mgogoro wa malipo ya tozo ya uwekezaji.

Mwaka 2005 SCB-HK, ilinunua deni ambalo benki ya Danaharta ya Malaysia ilikuwa ikiidai IPTL baada ya kampuni hiyo kukopa dola 101.7 milioni za Kimarekani ili kununua mtambo wa ufuaji umeme wa Tegeta wenye uwezo wa kuzalisha megawati 100. Lakini wakati fedha hizo zilipotolewa, ililipwa kampuni ya Pan African Power Solutions (PAP), jambo lililofanya SCB-HK kufungua kesi hiyo ICSID ikidai ndiyo iliyostahili malipo hayo, kesi ambayo benki hiyo ilishinda.

Umuzi huo wa ICSID umeshakubaliwa na kusajiliwa na Mahakama Kuu Tanzania kupitia maombi namba 687, ya mwaka 2016, yaliyofunguliwa na SCB-HK, na hivyo unatambulika kama uamuzi wa mahakama hiyo.


IPTL inafua umeme ambao unauzwa kwa Tanesco.

Lakini SCB-HK imewasilisha maombi kwa hati ya dharura ikiomba mahakama iizue Tenesco kuendelea kuilipa PAP, ambayo inamiliki IPTL na badala yake pesa hizo ziwe zinahifadhiwa mahakamani hapo hadi deni hilo litakapolipwa lote.

Benki hiyo inaiomba mahakama isikilize upande mmoja bila Tanesco kuwepo na iamuru fedha za malipo hayo ya uwekezaji yanayofanywa na Tanesco kwa PAP, ziwe zinalipwa mahakamani hapo kusubiri usikilizwaji na uamuzi wa maombi hayo.

Kwa mujibu wa hati ya dharura iliyoambatanishwa na maombi hayo, wakili wa SCB-HK, Gaspar Nyika anataka maombi hayo yasikilizwe kwa dharura akidai kuwa benki hiyo ndiyo ina haki na malipo hayo kulingana na uamuzi wa ICSID.

Pia anasema kama malipo hayo hayatahifadhiwa mahakamani kusubiri uamuzi wa maombi hayo, SCB-HK itaathirika kwa kupata hasara ambayo haiwezi kufidiwa.

Wakili Nyika anadai kuwa benki hiyo ilipewa haki dhidi ya mali na shughuli zote IPTL, baada ya kampuni hiyo kushindwa kurejesha mkopo iliouchukua kutoka benki ya Danaharta ulionunuliwa na SCB-HK mwaka 2005.

Katika uamuzi wake, ICSID ilieleza kuwa kwa mujibu wa Mkataba wa Mauziano ya Umeme (PPA) baina ya  benki hiyo na Tanesco, SCB-HK ndiyo yenye uhalali wa kisheria wa shughuli zote za IPTL.

Hivyo anasema fedha zilizolipwa kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow hazikuliondolea Tanesco wajibu wake kwa SCB-HK kwa mujibu wa PPA na hivyo hayawezi kupunguzwa kutoka katika kiasi inachodaiwa na benki hiyo. Pia ICSID ilisema kuwa malipo yaliyolipwa kwa IPTL/PAP tangu Agosti 2013, hayondoi  wajibu wa Tanesco kwa SCB-HK chini ya PPA na hivyo hayawezi kupunguzwa katika deni la SCB-HK, chini ya PPA.

Pia ICSID ilisema kuwa kuchotwa kwa pesa zilizokuwa kwenye Akaunti Maalumu ya Tegeta Escrow ( na kampuni ya Pan Africa Power Solution PAP inayodai kununua hisa zote za IPTL) hakukuiondolea benki hiyo haki katika kampuni hiyo ya IPTL.

Uamuzi wa ICSID uliwasilishwa Mahakama Kuu Oktoba 11, 2016 ili usajiliwe kwa ajili ya utekelezaji.

Hata hivyo siku hiyohiyo, Tanesco ilifungua maombi namba 686, ya mwaka 2016, ikiomba kusimamishwa kwa usajili na utekelezaji wa uamuzi huo, kusubiri usikilizwaji na uamuzi wa  maombi yake ya kusimamishwa kwa utekelezaji wa uamuzi huo katika ICSID.

By James  Magai,




Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger