Nov 13, 2016

Bunge Lanusa Ufisadi Mpiga Chapa Mkuu

BUNGE limenusa ufisadi katika Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali baada ya kubaini kuna mashine ya uchapaji ilinunuliwa kwa gharama kubwa, ikafanya kazi kwa muda mfupi na mpaka sasa, haifanyi kazi.

Aidha, Bunge limebaini ofisi hiyo haina usiri wa nyaraka za serikali zinazochapwa kwa kuwa baadhi ya nyaraka zinachapwa nje ya ofisi na inajiendesha chini ya viwango.

Waliishauri Serikali ifanye mabadiliko ya Menejimenti kwa kuwa muda mrefu hakuna ufanisi, taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo ilieleza hayo.

Taarifa hiyo iliridhiwa na Bunge bila kujadiliwa na wabunge juzi wakati Mwenyekiti wake, Andrew Chenge alipokuwa akifanya majumuisho mafupi bungeni mjini hapa.

Taarifa hiyo iliwasilishwa Alhamisi, Novemba 10 na Makamu Mwenyekiti wa kamati na Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM) lilipaswa kujadiliwa juzi lakini haikuwezekana kutokana na kifo cha Mbunge wa Dimani, Hafidh Ali Tahir (CCM) kilichotokea ghafla usiku wa kuamkia juzi mjini hapa.

Pia shughuli za Bunge ziliahirishwa mara mbili katika Mkutano huo wa Tano wa Bunge la 11, kutokana na kifo cha Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa, Samuel Sitta.

Akiwasilisha taarifa hiyo ambayo ilifanyiwa majumuisho mafupi na Chenge juzi, Ngeleja alisema Kamati hiyo ilifanya ziara katika Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali Machi 15 mwaka huu na kujionea shughuli za ofisi hiyo za uchapaji wa nyaraka za serikali, zikiwemo Sheria Ndogo.

“Hata hivyo Kamati hii imebaini kuwa Idara hii haiendeshwi kwa viwango vinavyokidhi mahitaji yaliyopo. Kwa mfano katika vikao vya Kamati vilivyopita, Kamati haikupokea kwa wakati Sheria Ndogo mbalimbali kwa sababu hazikuwa zimechapwa na Mpiga Chapa wa Serikali,” alisema Ngeleja.

Kamati hiyo ilisema kuwa dosari hiyo inatokana na ukweli kwamba ofisi hiyo inatekeleza majukumu yake chini ya kiwango kinachotakiwa na iko nyuma kiteknolojia.

“Kamati haikuridhishwa na maelezo ya Menejimenti ya Idara hiyo kuhusu uendeshaji na utendaji kazi na pia haikuridhishwa na hatua ya idara hiyo kutumia fedha za umma kununua mashine ya uchapaji kwa gharama kubwa na mashine hiyo kufanya kazi kwa muda mfupi… kamati inashangaa kwa nini hadi wakati Kamati inafanya ziara hiyo, mashine hiyo ilikuwa haifanyi kazi,” alisema Ngeleja bila kueleza ni kiasi gani kiligharimu manunuzi ya mashine hiyo.

Ngeleja alisema kamati ilibaini pia kuwa, kazi nyingi za idara hiyo zinafanywa nje ya idara kwa sababu printa ya ofisi hiyo huzidiwa na kazi.

“Kwa kutoa kazi hizo nje, kazi huchelewa lakini pia inapoteza usiri wa nyaraka za serikali na fedha nyingi kupotea,” alisema na kuongeza kuwa Kamati hiyo iliishauri serikali kuchukua hatua za haraka kuiboresha idara hiyo ili iachane na tabia ya kuchapisha nyaraka za serikali nje ya ofisi hiyo kwani inahatarisha usalama wa nyaraka na kuongeza gharama.

Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria katika taarifa yake kuhusu bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ilishauri pia kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu iboreshe mitambo na mazingira ya Idara ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kwa kuiwezesha kufanya shughuli zake kibiashara zaidi.

Kamati ya Sheria Ndogo katika ziara yake ilibaini pia kuwa mitambo ya Idara hiyo ni chakavu, majengo yaliochini ya kiwango pamoja na uhaba mkubwa wa vitendea kazi na kuishauri serikali, menejimenti ya Ofisi ya Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali ifanyiwe mabadiliko kwa sababu kwa muda mrefu imekuwa haitekelezi majukumu yake kwa ufanisi.

Imeshauri pia maslahi na mazingira ya kazi kwa watumishi wa ofisi hiyo yaboreshwe ili kuendana na shughuli wanazozifanya. Akifanya majumuisho ya taarifa hiyo juzi, Mwenyekiti wa Kamati hiyo na Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge aliitaka Serikali ifanyie kazi mapendekezo hayo ya Kamati ili kuboresha maeneo yaliobainishwa kuwa na changamoto.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger