Nov 12, 2016

Godbless Lema Arudishwa Rumande Baada ya Kunyimwa Dhamana Kwa Mara ya Pili

Ujanja wa kisheria uliosababisha mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kukaa mahakamani kwa saa 10, umemfanya kada huyo wa Chadema kukosa tena dhamana.

Jana, Mahakama ya Hakimu Mkazi ilishatupilia mbali hoja za Serikali za kupinga dhamana ya mbunge huyo, lakini mawakili walitumia silaha nyingine ya kukata rufaa Mahakama Kuu kupinga uamuzi wa kumpa dhamana Lema.

Mawakili wa Serikali walifanya hivyo muda mfupi baada ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Arusha, Desderi Kamugisha kutupa hoja za kuzuia dhamana ya Lema na hivyo kumzuia hakimu kuendelea na utaratibu wa kumwachia mbunge huyo kusubiri uamuzi wa rufaa hiyo, hali iliyoibua vilio mahakamani.

Kutokana na maamuzi hayo, hatma ya Lema kupata dhamana inasubiri Mahakama Kuu kupanga jaji wa kusikiliza shauri hilo.

Lema, ambaye alifikishwa mahakamani saa 2:00 asubuhi, alirudishwa mahabusu akiwa kwenye basi la magereza lililokuwa na ulinzi mkali saa 11:00 jioni.

Katika uamuzi wake uliotupilia hoja za awali za Serikali kupinga dhamana, Hakimu Kamugisha alisoma maamuzi kwa saa 2:35 na kutoa dhamana kwa Lema.

Hakimu Kamugisha alisema upande wa mashtaka uliwasilisha hoja tatu za kupinga dhamana ya Lema katika kesi za uchochezi namba 440 na 441/2016 na hati ya kiapo ya Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha(RCO).

Alisema hoja ni kuwa mshtakiwa ametenda makosa hayo, wakati akiwa nje kwa dhamana kwa kesi namba 351 na 352 za mwaka 2016, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Hakimu Kamugisha alisema hoja nyingine ni kutaka Lema anyimwe dhamana kwa ajili ya kulinda usalama wake, hasa kwa kuwa kauli zake za uchochezi dhidi ya Rais John Magufuli zimewaudhi wananchi.

Hoja ya tatu kujali maslahi ya Taifa. Hoja hizo ziliandamana na hati hiyo ya kiapo cha RCO.

Hata hivyo, hakimu alisema mawakili wa utetezi waliokuwa wanaongozwa na John Mallya walipinga hoja hizo, wakisema dhamana ni haki ya mshitakiwa na kuwa nje kwa dhamana katika mashauri mengine ambayo hayajamtia hatiani mtuhumiwa, hayawezi kuwa sababu ya kumnyima dhamana.

Alisema mawakili hao, pia walipinga hoja za kutokutolewa dhamana kutokana na usalama wake na maslahi ya Jamhuri na pia wakakosoa hati ya kiapo kuwa ina mapungufu, hasa ya kutokuwa na uthibitisho wa mambo yaliyoelezwa.

Hakimu Kamugisha alisema msingi wa haki ya dhamana ni wa Katiba ibara ya 15(1) na (2) ambayo inaelezea uhuru wa mtu.

Alisema pia ibara ya 17 ya Katiba inatoa haki ya mtu kutembea popote na kuongeza ibara ya 16(6) B inaeleza mahakama inamchukulia mtuhumiwa yeyote kuwa hajafanya kosa hadi anakapotiwa hatiani.

Alisema washitakiwa hupelekwa mahabusu ili iwe lazima mtuhumiwa kufika mahakamani.

Hakimu Kamugisha alisema, siku zote dhamana haitolewi ikiwa tu kuna mazingira ya kisheria ambayo yameelezwa na kuwekewa masharti na utaratibu wake.

Alitolea mfano kesi ya Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP) dhidi ya Daudi Beda ambapo ilielezwa haki za mshtakiwa na sababu ambazo zinaweza kuzuia dhamana.

Alisema katika kesi hiyo, mahakama iliamua kuwa ili kunyimwa dhamana lazima kuwepo mazingira yaliyoanishwa kisheria na utaratibu ulioanishwa kisheria.

“Nimeshindwa kupata kifungu chochote cha sheria ambacho kinazuia kutoa dhamana kwa mtuhumiwa aliye nje kwa dhamana ambaye ametenda makosa mengine ambayo hayahusiani na masharti ya dhamana ya awali,” alisema.

Alisema hata maelezo kuwa watu waliohudhuria mkutano hawakuridhishwa na kauli za Lema na kwenda kulalamika kwa RCO, hayana panapoonyesha usalama wa mtuhumiwa upo mashakani.

Alisema ili hoja ya dhamana izuiwe kwa maslahi ya Jamhuri, inakuwa na hati ya maombi hayo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP) na si RCO hivyo haoni msingi wa kutotoa dhamana hiyo “Hivyo kwa uchambuzi huu wa kisheria natoa dhamana kwa mshitakiwa,” alisema.

Hata hivyo, wakati anajiandaa kuandika masharti ya dhamana, ndipo wakili mwandamizi wa Serikali, Paul Kadoshi aliwasilisha notisi za kupinga uamuzi wa dhamana hiyo.

Alisema anawasilisha notisi hiyo chini ya kifungu cha 379 (1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura ya 20 ya mwaka 2002.

Alisema nia ya kuwasilisha notisi hiyo inatokana na mabadiliko ya Sheria za Makosa ya Jinai namba 27 ya mwaka 2008.

Alisema kifungu cha 31 aya G katika sheria hiyo kifungu 379(1 ) (a) kwa kuongeza maneno kuwa notisi ya kukata rufaa inaweza kujulikana kama ni rufaa.

Alisema mabadiliko ya sheria hiyo yalimpa hadhi DPP anapoeleza notisi ya rufani kuwa tayari ni rufani kamili na hivyo notisi hiyo ikitolewa mwenendo wa kesi nzima unapaswa kusimama.

Kadoshi alisema maamuzi hayo, yamefikiwa katika kesi ya Jamhuri dhidi ya Harry Kitillya na wenzake wawili, pale DPP alipowasilisha notisi na rufani na kesi kusimama.

Hata hivyo, licha ya mawakili wa utetezi, Sheki Mfinanga na Richard Shediel kupinga hoja hiyo, Haklimu Kamugisha, ambaye aliomba dakika 10 kutafakari suala hilo, alikubaliana na hoja za upande wa Serikali za kumkatalia Lema dhamana.

Kutokana na maamuzi hayo Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu amesema chama hicho kimewataka wanasheria wake, Tundu Lissu na Peter Kibatala kwenda Arusha kuongeza nguvu katika kudai haki ya Lema kuwa huru.

Mke wa Lema, Neema Lema aliwataka wakazi wa Arusha kuwa watulivu, akisema mbunge huyo anapigania uhuru wa wananchi.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger