Nov 11, 2016

KOCHA Pluijm Awaaga Vizuri Yanga, Amkaribisha Lwandamina Kwa Ushindi Wa 2-1

KOCHA Mholanzi, Hans van der Pluijm leo amewaaga vizuri wana Yanga baada ya kuiongoza timu hiyo kushinda 2-1 katika mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Ushindi huo unaifanya Yanga imalize na pointi 33 nyuma ya Simba SC yenye pointi 35 kileleni baada ya mechi 15 za mzunguko wa kwanza.

Sifa zimuendee kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima kwa ushindi wa leo kutokana na kuseti bao la kwanza na kufunga bao la pili.

Lakini Yanga ililazimika kutoka nyuma baada ya Ruvu kutangulia kwa bao la Abrahman Mussa aliyemalizia krosi ya Fully Zulu Maganga dakika ya saba na kumtungua kipa Benno Kakolanya.

Hata hivyo Nahodha wa Yanga leo, Niyonzima akamtoka kwa chenga maridadi kabisa beki Mau Boffu kabla ya kutia krosi iliyounganishwa nyavuni na winga Simon Msuva kuisawazishia Yanga dakika ya 32.

Refa Mathew Akrama wa Mwanza alisindikizwa na Polisi huku akitolewa maneno ya ukali na kocha wa Yanga, Pluijm baada ya kupuliza filimbi ya kukamilisha dakika 45 za kipindi cha kwanza.

Na haikuwa ajabu refa huyo alipomtoa kwenye benchi Pluijm kabla ya kuanza kipindi cha pili.

Niyonzima aliifungia bao la ushindi Yanga dakika ya 56 kwa shuti la mbali kufuatia mpira uliorudi baada ya shambulizi kali langoni mwa Ruvu.

Yanga wakatulia na kuanza kucheza kwa kupasiana ili kuumiliki mpira kwa lengo la kuwapunguza kasi Ruvu wafanikiwe kuulinda ushindi wao.

Pluijm anaondoka Yanga kumpisha Mzambia, George Lwandamina atakayeanza kazi mzunguko wa pili wa Ligi Kuu.

Na Pluijm anaondoka baada ya kuiongoza Yanga kwa awamu mbili tangu mwaka 2014 akicheza jumla ya mechi 128, akishinda 80, kufungwa 23 na sare 25.

Mwaka 2014 aliiongoza Yanga katika mechi 19, akishinda 11, kufungwa mbili na sare sita kabla ya kuondoka kwenda Al Shoalah FC ya Saudi ya Arabia na nafasi yake ikachukuliwa na Mbrazil, Marcio Maximo.

Maximo alifanya kazi kwa nusu msimu kabla ya Pluijm kurejeshwa Januari mwaka jana.  Saudi Arabia ambako alikwenda na aliyekuwa Msaidizi wake, Yanga SC, Charles Boniface Mkwasa – Pluijm  aliondoka baada ya kutofautiana na uongozi wa timu uliotaka kumsajilia wachezaji asiowataka.

Na kuanzia Januari mwaka jana, Pluijm ameiongoza Yanga katika mechi 109, akishinda 69, sare 19 na kufungwa 21.

Na Pluijm anaiachia Yanga mataji mawili ya Ligi Kuu, mawili ya Ngao ya Jamii na moja Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC).

Katika mchezo wa leo, Pluijm hakuketi kwenye benchi la Yanga, bali alichukua kiti na kuketi pembeni ya benchi hilo kuashiria kwamba anaondoka.

Kikosi cha Yanga leo kilikuwa; Beno Kakolanya, Hassan Kessy, Mwinyi Hajji, Kevin Yondan, Andrew Vincent, Thabani Kamusoko, Simoni Msuva, Haruna Niyonzima, Donald Ngoma/Matheo Anthony dk86, Amissi Tambwe na Obrey Chirwa/Juma Mahadhi dk60.

Ruvu Shooting; Abdallah Rashid, Said Madega, Mau Ali Bofu/Yussuf Nguya dk79, Renatus Kisase, Shaibu Nayopa, Jabir Aziz, Abrahman Mussa, Zubeiry Dabi/Raphael Kyala dk60, Issa Kanduru, Fully Maganga/Said Diliunga dk70 na Chande Magoja.

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger