Nov 11, 2016

RAMBO Mkata Mapanga Awa Tushio Kubwa Kipawa...Akata Watu Mapanga na Kuwaibia


Dar es Salaam. Wakazi wa kata ya Kipawa jijini Dar es Salaam wameingiwa na hofu baada ya kuibuka kijana anayejiita ‘Rambo mkata mapanga’ anayedaiwa kufanya uhalifu kwa kujeruhi watu kwa kuwakata mapanga kisha kuwapora fedha na mali zao.

Kijana huyo ambaye jina lake halisi ni Abdul Chata ameibuka ikiwa ni wiki kadhaa zimepita tangu kuibuka kwa sakata la ‘Scorpion’ aliyeshtakiwa kwa tuhuma za uporaji na kujeruhi ikiwamo kutoboa macho.

Miongoni mwa watu waliovamiwa, kukatwa mapanga na kuporwa na anayedaiwa kuwa Rambo mkata mapanga ni walimu watatu wa Shule ya Msingi Mogo, iliyopo kata ya Kipawa.

Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti, wakazi wa eneo hilo walisema tangu kuibuka kwa mkata mapanga wiki mbili zilizopita, hali ya amani ya eneo hilo imekuwa mbaya kiasi cha kushindwa kutembea usiku kuanzia saa moja.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Karakata, Kata ya Kipawa Andrew Olutu alisema hadi sasa ofisi yake imethibitisha zaidi ya matukio manne ya watu kuporwa kisha kujeruhiwa kwa mapanga.

“Ni mtu hatari na amewapa hofu kubwa wananchi kwa sababu hawezi kupora kitu chochote bila kukukata mapanga, tumekumbwa na taharuki,” alisema Olutu.


Alisema kijana huyo hutembea na mapanga mawili ambayo huyaficha mgongoni na kwamba huwa haijalishi muda gani anaweza kufanya tukio japo, matukio mengi yamefanyika usiku.

Akisimulia zaidi, mwenyekiti huyo alisema tukio jingine lilitokea usiku wa kuamkia Novemba 3, ambapo kijana huyo aliteka bodaboda kisha kumjeruhi dereva kwa panga usoni akimlazimisha ampakie na kumpeleka eneo analotaka. “Inavyoonekana kulikuwa na mvutano baina ya Rambo na dereva wa bodaboda, kwa sababu tulikuwa tunalinda sungusungu tukasikia kelele na kwenda haraka na kumkuta bodaboda akivuja damu. Alikuwa amecharangwa mapanga usoni,” alisema.

Hata hivyo, alisema hawakufanikiwa kumkamata ‘Rambo’ ambaye alikimbia baada ya kuona sungusungu lakini walitoa taarifa za tukio hilo polisi na kumpeleka majeruhi hospitali.

Olutu alisema kutokana na hali kuwa mbaya zaidi, wamelazimika kuunda vikosi vya sungusungu viwili vikiongozwa na kamati ya ulinzi na usalama ya mtaa ili kuwanusuru watu wanaovamiwa.

Baadhi ya wananchi walisema kutokana na hali hiyo wanalazimika kurejea majumbani mapema ili kukwepa mapanga ya Rambo anayeonekana kuwa tishio.

Mkazi wa Mtaa wa Mkarakata, Sam Aidan alisema alinusurika kucharangwa mapanga ya ‘Rambo’ mwishoni mwa wiki iliyopita na kilichomuokoa siku hiyo ni gari lililotokea mbele yao.

“Ilikuwa saa mbili maeneo ya mji mpya nikakutana na ‘Rambo’, nashukuru Mungu muda huo huo lilitokezea gari akakimbia na kuniacha salama. Tangu hapo ni bora nilale huko huko au nikodi teksi ili nirejee nyumbani, kama nikiona giza limeingia,” alisema.

Aliliomba jeshi la Polisi lisaidie kumkamata mhalifu huyo ili wapate amani.

Diwani wa Kata ya Kipawa, Kennedy Simon alisema kijana huyo alianza kufanya matukio ya uhalifu mwaka jana akiwajeruhi wananchi na kuwapora mali zao.

Alidai hali hiyo iliwafanya kumvizia siku moja na kumkamata kisha kumpiga kabla hajaokolewa na polisi.

Simon alisema alifikishwa kituoni, kisha mahakamani ambako alihukumiwa kifungo jela.

“Wiki mbili zilizopita tumeshangaa amerejea mtaani kwa kasi kubwa, safari hii anaitwa ‘Rambo mkata mapanga’ na ukikutana naye, ni bora ujaliwe kutimua mbio kwa sababu hawezi kukuibia bila kukuachia alama ya panga,” alisema.

Alisema taarifa za matukio hayo zimeripotiwa polisi na wanaendelea kumtafuta japo hadi sasa hajakamatwa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni alithibitisha kuwapo kwa kijana huyo anayejiita ‘Rambo mkata mapanga’ na kusema tukio linalofahamika hadi sasa ni lile la uvamizi wa shule.

Aliwataka wananchi kusaidia kutoa taarifa za eneo analopatikana mtuhumiwa huyo ili wamkamate.

“Taarifa za ‘Rambo mkata mapanga’ ninazo, tumeshaweka mitego mbalimbali ili kumkamata na niwasihi wananchi wakimuona tu watoe taarifa ili adhibitiwe,” alisema.



Tukio shuleni

Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Mobo, jijini Dar es Salaam walisema wanasoma kwa hofu tangu walimu wao walipovamiwa, kuporwa na kuibiwa.

“Alikuja kama saa 10:00 jioni, akaenda moja kwa moja kwenye eneo walikokuwa walimu akawaumiza na kuwapokonya vitu vyao zikiwamo simu, tunaogopa kwa sababu anaweza kuja tena,” alisema.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Magreth Fredrick alithibitisha kutokea kwa tukio la kujeruhiwa walimu watatu na kwamba taarifa zaidi zimefikishwa kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger