Zima moto wameudhibiti moto huo katika mji wa kaskazini wa Haifa ambapo takriban watu 80,000 walilazimishwa kuondoka.
Lakini maafisa wanasema moto midogo midogo bado inaendelea kukabiliwa katika maeneo tofauti.
Netanyahu: Moto mkubwa Israel umesababishwa makusudi
Moto huo umesababishwa na hali ya kiangazi pamoja na upepo mkali.
Watu kadhaa wametibiwa kwa kuvuta moshi lakini hakuna majeraha yalioripotiwa.
Ndege zinazosaidia katika harakati ya kuuzima moto mkubwa unaonedelea kulichoma taifa la Israel
Ndege zinazosaidia katika harakati ya kuuzima moto mkubwa unaonedelea kulichoma taifa la Israel
Waziri mkuu wa Israel awali alisema kuwa iwapo moto huo ulianzishwa kwa makusudi basi washukiwa watakabiliwa na mashtaka ya ugaidi
Waziri wa elimu Naftali Bennet ,kiongozi wa chama cha Jewish Home Party ,aliashiria kwamba huenda kuna mkono wa Waarabu ama Wapalestina kupitia ujumbe wake wa Twitter uliosoma: Ni wale wasiotoka katika taifa hili ambao wanaweza kulichoma pekee.
Vuguvugu la rais wa Palestina Mahmoud Abbas, Fatah limesema kuwa maafisa wa Israel wanatumia moto huo kuwalaumu Wapalestina.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment