Nov 25, 2016

Sinema Mpya Sakata la Polisi Wanne Kumvua Nguo Mchungaji


Moshi. Siku moja baada ya gazeti hili kuripoti tukio la polisi wanne wanaodaiwa kumvua nguo mchungaji wa kanisa moja nchini akiwa na mtu mwingine na kumhusisha na vitendo vya ushoga kisha kumdai Sh10 milioni ili kulimaliza, shuhuda mmoja amejitokeza na kusimulia mkasa mzima.

Katika tukio hilo la Novemba 18, mchungaji huyo anadaiwa kufanyiwa kitendo hicho baada ya kukaribishwa katika nyumba moja ya wageni huko Bomang’ombe, Hai na mtu mmoja waliyekuwa na miadi ya kibiashara ambaye alitaka ajue mahali alikofikia.

Shuhuda huyo, mmoja wa wahudumu katika nyumba hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe, amesema mtu huyo ndiye aliyewaita polisi alipotoka na kumwacha mchungaji chumbani na kabla ya kuwapigia simu askari hao, aliagiza chai kwenye mgahawa huo.

“Alikuwa akiwahimiza polisi wafanye haraka kabla hajarudi chumbani. Wale polisi walipokuja akawaambia wasubiri dakika chache ndipo wamfuate chumbani. Yeye akarudi chumbani lakini kiukweli hawakuwa wamefanya hicho kitendo (ushoga),” alisema.

Alisema aliwasihi polisi wasiwatoe watu hao muda huo (saa kumi na moja alasiri) akisema kufanya hivyo kungeweza kuharibu jina la hoteli yao.

Polisi, Takukuru wamsaka


Akizungumzia sakata hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Koka Moita alisema jana kwamba wako njiapanda kwa vile maelezo ya mchungaji huyo kwa Takukuru yanatofautiana na yale aliyoyatoa polisi.

“Wakati akisimulia huo mkasa kule Takukuru mimi nilikuwepo na ndiyo haya yaliyopo kwenye gazeti (Mwananchi) lenu la leo (jana) lakini cha ajabu maelezo aliyoyatoa polisi ni tofauti kabisa,” alisema. “Hatuwezi kusema moja kwa moja kuwa tunamtafuta kwa sababu yeye siyo mtuhumiwa lakini tungependa aje atueleze utofauti huu wa hadithi yake.”

Kamanda wa Takukuru Mkoa Kilimanjaro, Alex Kuhanda alisema jana kuwa, “Sisi ndiyo tuliompokea na kumsikiliza na baadaye tukawakabidhi wenzetu wa polisi lakini tangu Jumamosi (Novemba 19), hatumpati kwenye simu ili atupe mrejesho,” alisema Kuhanda licha ya kuahidi kufika katika ofisi hizo kwa ajili hiyo.

Ilivyokuwa

Mchungaji huyo anadaiwa kukutana na dereva wa malori eneo la Njiapanda ya Himo na kuweka miadi ya kuwasiliana kwa ajili ya biashara ya pumba hivyo walipeana namba za simu ili zikipatikana apigiwe.

Siku iliyofuata mtu huyo alimpigia akisema amepata magunia 150 na kumtaka mchungaji afike Bomang’ombe kuziona pumba hizo. Alipofika, kabla ya kwenda kuziona, alimuomba mchungaji amsindikize ili achukue chumba kwani siku hiyo angelala hapo kusubiri wenzake kutoka Segera.

Walifuatana na baada ya kupewa funguo, alimtaka mchungaji aingie kukiona kabla ya kumwambia amsubiri hapo akanunue sigara ili akirudi waende kuangalia na aliporudi tu, ndipo walipoingia na watu wengine ambao baadaye wanne walibainika kuwa polisi na kuwalazimisha mchungaji na mtu huyo kuvua nguo, na kuwarekodi kwa picha wakiwatuhumu kufanya ushoga.

Ilidaiwa kwamba waliwachukua wakiwa nusu uchi hadi kituo cha Polisi cha Bomang’ombe na kutaka wapewe Sh10 milioni ambazo hata hivyo hazikupatikana na badala yake wakapewa Sh5.4 milioni.


Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger