Nov 13, 2016

Uchambuzi:Namna Ambavyo Mkataba wa EPA Ungeliangamiza Taifa

Wakati  wabunge wamemsihi Rais John Mafuguli kutotia saini mkataba wa ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Ulaya (EPA), Imebainika kuwa Tanzania ingepoteza dola milioni 984 (zaidi ya Sh. trilioni mbili) kwa mwaka kutokana na kuingia kwa bidhaa kutoka kwenye nchi hizo ambazo hazitalipiwa kodi.

Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa na Utawala wa Umma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Sabatho Nyamsenda, aliyasema hayo juzi mjini Babati, Manyara kwenye mkutano wa tisa wa Mtandao wa Wakulima Tanzania (Mviwata).

Nyamsenda alisema athari ya kupoteza mapato hayo kwa taifa ni kubwa na awali, Rais Magufuli alishaonyesha njia kwa kukataa kutia saini makubaliano hayo na pia wabunge walipoukataa imekuwa jambo jema. Alisema takwimu zilizotolewa kuwa nchi itapoteza dola milioni 32 (Sh. bilioni 64) kwa mwaka si sahihi kwa kuwa ni takwimu za miaka iliyopita.

Alisema taasisi ya South Centre ilianzishwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, kwa ajili ya kupigania ushirikiano wa nchi za kusini, zinaeleza kuwa fedha hizo zitapotezwa kutokana na ushuru wa bidhaa ambazo hazitalipwa baada ya mkataba wa EPA.

 Aidha, nchi ambazo zilikuwa zinatozwa mapato nchini hazitatozwa tena na nchi zingine zitashindwa kushindana kwenye soko kutokana na bidhaa za Umoja wa Ulaya, zinazozalishwa kwa unafuu na pia hazitalipishwa kodi.

“Kutokana na mkataba huo, kutakuwa na upotevu mkubwa wa mapato na pia viwanda vya ndani vitakufa kwani havitaweza kushindana kwenye soko na bidhaa hizo kutoka kwenye nchi za Ulaya,” alisema.

Endapo nchi ikiingia makubaliano hayo, itasalimisha ushuru, ujenzi wa uchumi wa viwanda na kuendelea kufanya kazi ya utumwa, kwa kuwa viongozi wa nchi za Ulaya wanataka tuendelee kuwa wazalishaji wa malighafi kwenye soko lao.

“Tutaendelea kuzalisha mali ghafi za pamba, kahawa na mazao mengine na kupeleka Ulaya kisha wao wanazalisha nguo wanazivaa na kutuletea mitumba na kuja kutuuzia sisi bila wao kulipia ushuru wa kuingiza bidhaa,” alisema.

Nchi kama nchi haitakuwa na viwanda vya ndani kwa kuwa itashindwa kuvilinda na kuhakikisha unajiwekea ukomo wa aina ya bidhaa zinazoingia nchini na kwa hali hii tutapoteza dhana ya uchumi wa viwanda.

“Wakulima, wafugaji na wazalishaji wa chini wataendelea kufanya kazi za hali ya chini kwa kuendelea kuchuma pamba, kuchunga mifugo na kurudishwa kwenye hali ya utumwa kupitia makubaliano ya EPA,” alisema.

Mratibu wa Mviwata wa Mkoa wa Manyara, Martin Pius, aliipongeza serikali kwa kutotia saini mkataba huo kwa sababu makubaliano hayo yanagusa maendeleo ya jumla ya wananchi wa Tanzania hasa wakulima wadogo.

Alisema wakulima wa Ulaya wanapatiwa ruzuku kwa ajili ya uzalishaji na masoko tofauti na wakulima wa Tanzania, hivyo mkataba huo utakuwa unaumiza kwa kuwa bidhaa zao zitakuwa na bei ndogo tofauti na bidhaa za wakulima wa Tanzania.

 – Nipashe

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger