Nov 13, 2016

Ufafanuzi wa Madaktari Baada ya Mtoto Aliye Wekewa Betri Kwenye Moyo Kufariki

Siku chache tangu kutokea kifo cha mtoto Happiness Josephat (6), aliyekuwa amefanyiwa upasuaji wa kupandikizwa betri ndani ya moyo wake, hali ya wasiwasi imetanda miongoni mwa wagonjwa waliopandikizwa kifaa hicho.

Wasiwasi huo umetanda kutokana na taarifa zinazosambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, watumiaji wa mitandao hiyo wakidai kifo hicho kimesababishwa na kifaa hicho kushindwa kufanya kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi alisema taarifa hizo si za kweli na kwamba ni za upotoshaji.

“Kwanza jamii ielewe kwamba, JKCI tumesikitishwa mno na kifo cha Happiness kwa sababu tulikuwa tukifuatilia maendeleo yake kwa ukaribu, na kifo chake kimetushtua kwani kimetokea ghafla.

“Baada ya kifo kile kumekuwa na taarifa nyingi zinazosambazwa mtandaoni ambazo si sahihi na zimepelekea wagonjwa wetu tuliowafanyia upasuaji wa aina hiyo kuwa na hofu na wasiwasi.

“Ukweli ni kwamba kifaa kile tulichomuwekea hakikuwa na tatizo lolote, kilikuwa kinafanya kazi sawa sawa na hii ni kwa mujibu mama yake, Elitruda Malley ambaye tulihojiana naye kujua alipatwa na shida gani.

“Akatueleza kuwa alianza kulalamika kuwa anasikia maumivu ya tumbo, akachukua kifaa cha kupima mapigo ya moyo ambacho tulimpatia, alipompima kifaa kilionesha kuwa yalikuwa sawa sawa.

“Lakini akatueleza bado mtoto alilalamika tumbo linamuuma, akampeleka hospitali ya Selian lakini hawakugundua tatizo na wakampatia dawa ya diclofenac kutuliza maumivu,” alisema.

Profesa Janabi alisema hata hivyo tatizo hilo liliendelea ambapo mama huyo alimrudisha tena mwanawe hospitalini hapo kwa uchunguzi zaidi.

“Lakini bado tatizo halikuonekana, na alipokuwa akipimwa mapigo ya moyo kifaa kilikuwa kinasoma yapo sawa sawa, ripoti ya awali ya madaktari wa selian inaeleza kuwa alisumbuliwa na tumbo, tumeomba watupatie uchunguzi ufanyike kwa kina na watupatie taarifa kamili,” alisema.

Dk. Janabi alisema wanataka kufanya uchunguzi zaidi kwani hadi sasa jumla ya wagonjwa 31 wamefanyiwa upasuaji wa kupandikizwa kifaa na wanaendelea vizuri pasipo shida yoyote.

“Happiness ndiye mtoto wa kwanza nchini kuwekewa kifaa hiki ndiyo maana tulisema ni upasuaji wa kihistoria, tumesikitishwa mno na kifo chake, taarifa zetu zinaonesha alizaliwa Desemba 16, 2012 huko Mbulu, Manyara na Julai 15, mwaka huu tulimfanyia upasuaji wa kumpandikiza kifaa hicho baada ya kugundulika kuwa alizaliwa na tatizo lijulikanalo kitaalamu ‘heart break’.

“Mfumo wa umeme wa moyo wake haukuwa unafanya kazi sawa sawa kama inavyotakiwa, ndio maana mapigo yake yalikuwa kati ya mara 20 hadi 25, madaktari wa JKCI tulifanya upasuaji huo kwa kushirikiana na wenzetu wa marekani na aliruhusiwa wiki mbili baadae, Agosti mosi, mwaka huu.

“Tulitamani hata tungeweza kuufanyia mwili wake ‘postmotum’, ili tujue nini hasa kimesababisha kifo chake ikiwa kifaa tulichomuwekea kilikuwa kinasoma mapigo ya moyo vizuri,” alisema.

Daktari Bingwa wa Upasuaji Moyo Idara ya Watoto, Edwin Sharau alisema kila mwaka duniani watoto 22,000 huzaliwa na tatizo kama alilokuwa nalo marehemu Happiness.

“Takwimu zinaonesha Tanzania kwa mwaka huzaliwa mtoto mmoja, hali hiyo hutokea pale nguvu ya kupigana na magonjwa ya mama wakati wa ujauzito ‘antibody’ zinapovuka kwenye kondo la mama kisha kuingia kwa mtoto akiwa tumboni.

“Asilimia 70 ya watoto wanaokumbana na nguvu hiyo, hufariki dunia, asilimia 25 huzaliwa lakini hufariki katika miezi ya kwanza na asilimia 85 kati ya hawa asilimia 25 ambao huzaliwa hufariki kwa sababu moyo wao hushindwa kufanya kazi ipasavyo,” alisema.

 – MTANZANIA

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger