Nov 17, 2016

Ukweli kuhusu Papa "kuruhusu talaka" kwa ndoa za kanisa katoliki

Wenzetu nchi zilizoendelea waandishi wa habari wanaoandika habari za aina fulani ni lazima wawe ma uweledi wa jambo hilo.Ukiwa unaandika habari za uchumi,basi ni lazima walau uwe na ABC za mambo ya uchumi,siasa kadhalika,habari za afya na hata zile za mambo ya uhandisi.Ndio maana si ajabu kukuta mwandishi wa habari kaandika habari za mambo ya usafiri wa anga,akaandika "Kutana na mwanamke wa kwanza kurusha ndege aina ya BOEING AIRBUS".Wakati kiukweli hakuna aina ya ndege hiyo duniani.

Habari za kanisa,pia zinahitaji walau mwandishi awe na ABC za mambo ya kanisa na kupata ufafanuzi wa uelewa wa mambo mengi ndani ya kanisa.

Kuna habari inazagaa,na imetolewa ufafanuzi makanisani,sio kweli kuwa Papa ameruhusu "Talaka" kwa ndoa za kanisa katoliki,ila ukweli ni kuwa Papa amerahisisha njia za "utatuzi wa migogoro" ya ndoa ndani ya Kanisa Katoliki.

Ifahamike kuwa toka miaka na miaka,ndoa za kanisa katoliki zimekuwa zinafuata mlolongo mrefu pale zinapoonekana kuwa zina hitilafu ili kuweza kuwa "invalid".Kutokana na elimu ndogo juu ya sheria za ndoa ndani ya kanisa kwa waumini,wapo waumini wengi wanaodhani hawawezi kubatilisha ndoa zao hasa kama zilifungwa bila kufuata vigezo.

Sasa badala ya maamuzi haya kufanyika Vatican kwenye Mahakama ya Ndoa "Rota Romana" sasa jambo hili limaweza kuwa mikononi mwa Askofu Mkazi.Hivyo kuondoa ule mlolongo wa mtu kutoka kigango cha Luhumbo Kishapu Jimbo la Shinyanga kwenda Rota Romana Vatican na sasa mtu huyo ataenda Cathedral Ngokolo Shinyanga kupeleka shauri lake.Huu ndio msingi wa ujumbe wa Papa,kuleta madaraka katika majimbo mahalia.

Kuna kutazamwa kwa ndoa zilizobatilishwa kwa namna mbili,ya kwanza ni "Annulamento",hii ni ndoa inayotenguliwa mahakama za kiraia lkn kanisa linakuwa kinaendelea kuitambua kama ni ndoa "valid" sbb kuharamishwa kwake hakujafuata taratibu na sheria za kanisa,bali za kidunia.Mahakama huzibatilisha ndoa hizi kutokana na "magumu ya dunia".Hivyo Mahakama za kidunia hutalakisha ndoa ambayo ni "valid" kikanisa.Kanisa katoliki inawachukulia watu hawa ni wanandoa,na hiyo inakuwa ni "impediment" kwa wao kufunga ndoa nyingine.

Namna ya pili ni "Nullità",kingereza ni "Nullity".Nullity maanake hiyo ndoa toka "inazaliwa" haikuwa ndoa halali na hivyo kanisa inaibatilisha.Ndiyo maana kanisa katoliki hutangaza ndoa husema "wenye kizuizi",na matangazo huwa kwa muda mrefu na hutangazwa mahali pote wanandoa walipowahi kuishi.

Kuna sababu za Mahakama ya Kanisa ku-nullify ndoa iliyofungwa kanisani,sababu hizo ni kama vile


  • Uhuru,iwapo itathibitika pasi na shaka kuwa mmoja kati ya wanandoa alilazimishwa.
  • Kumficha mwenzako kama ulikuwa na watoto nje
  • Kuficha kuwa upo huru wakati ulishafunga ndoa
  • Kuwa impotent (hanisi/tasa) bila uwazi kabla
  • Kwa Padre kufunga ndoa na mwanamke bila yeye kusema ni padre


Ili mtu upate kibali cha kufunga ndoa ya pili hizo juu ni sababu mojawapo katika kanisa katoliki, inabidi upate kibali kutoka katika "Mahakama ya Kanisa".Hizi mahakama za "Nullity of Matrimony" zipo katika kila Jimbo Tz,huundwa na mahakimu watatu ambapo hata walei wanaweza kuwepo lkn katika hao watatu ni mkleri ambaye anatakiwa awe kiongozi.

Askofu wa Jimbo lolote anaweza kutoa "nullity" kwa ndoa zile ambazo evidence zake zipo wazi.Kila jimbo palipo na askofu tayari ile ni mahakama.Sasa Maaskofu wanaweza kukubaliana wakaunda mahakama moja inayojumuuisha majimbo kadhaa.Mfano Mahenge,Kilosa na Morogoro wakawa na mahakama moja.

Na katika kila shauri la "Nullity of Matrimony" huwa yupo Padre mwingine kwa ajili ya "defend of matrimony",ambaye lazima awe padre aliyebobea katika sheria za kanisa(Canon law).Na hata wakitokea wanandoa wanakubaliana yeye huwa against na huweza ku-appeal mahakama ya juu ili ndoa hiyo isiweweze kuwa "invalid"

Kuna muundo wa Kimahamaka pia ndani ya kanisa,toka Mahakama ya mwanzo hadi rufaa.Hii huanzia kwa mahakama za kijimbo,ikishindikana shauri hupelekwa kwenye mahakama ya Metropatania(Jimbo Kuu),hapo ikishindikana shauri hupelekwa kwa Askofu Mkongwe(Kwa umri) ktk eneo husika na rufaa ya mwisho huwa Rota Romana Vatican.

Wenzetu wa nchi zilizoendelea,ambao elimu ya sheria za kanisa hutolewa kwa waumini wa kawaida kwa nafasi na uwazi,mambo haya wanayafuatilia na kufahamu.Wapo wakristo Afrika ambao ndoa zao ni "invalid",lkn kwa "kukaririshwa" kuwa ndoa za Kanisa ni mpaka "kufa na kuzikana" basi wanaendelea kukaa katikati ya uvuli wa mauti,lkn kumbe wanaweza kufuata hatua hizi na endapo ikathibitika pasi na shaka,basi ndoa zao zinakuwa "Nullified".Sasa Papa kapunguza mlolongo huu,na sio karuhusu "talaka"

Zamani mashauri haya yote yaliruka moja kwa moja mpaka Rota Romana,Vatican,lkn sasa imerahisishwa,kurahisishwa huku kwa kuanzia ngazi ya Maaskofu,basi waandishi wasiotafiti wanaishia kusema "Papa aruhusu Talaka ndoa za kanisa Katoliki".

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger