Klabu hiyo ya Ligi Daraja la Kwanza nchini humo ambayo inajulikana kama Segunda Division ikiwa ni hatua moja baada ya Ligi Kuu ambayo ni La Liga imekubali kiwango cha uchezaji cha winga huyo ambapo inasubiri kufanya mazungumzo na klabu yake ya Azam FC ili kuweza kumtwaa.
Farid alifanya majaribio nchini humo kwa takribani wiki mbili na ameonekana kukubalika na klabu hiyo.
Taarifa za ndani zinaeleza Tenerife na Azam FC wamekubaliana katika umiliki wa kinda huyo mwenye kasi ambaye imeelezwa anarejea nchini leo akitokea Hispania.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment