Aug 7, 2016

Chama Cha CUF Kufa Kifo Cha Mende?

CHAMA cha Wananchi (CUF) ni kama kipo kuzimu. Kimelegea, kimechuja na kwa sasa kimegota, anaandika Faki Sosi.

CUF ya Prof. Ibrahim Lipumba, aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho taifa kabla ya kujiweka pembeni, si hii inayoongozwa na Twaha Taslima ambaye amebeba mikoba ya uenyekiti kwa ‘dharura’.

Wapo wanaochekelea kuiona CUF ya sasa ikikosa miguu ya kusimama, ikipoteza mvuto na mvumo wake katika siasa za nchini hii.

Wapo wanaotamani CUF ifutike leo kesho, wapo wanaovutiwa na mwenendo wa kuchechemea wa CUF kwa sasa lakini pia wapo wanaotamani Taslima awe mwenyekiti wa taifa wa chama hicho.
Si kwa mwema, isipokuwa ni kwa imani kwamba, Taslima ndio njia sahihi ya kuzima nuru ya CUF kwenye uwanja wa siasa nchini.

Dalili hizo zipo wazi, tangu Taslima aingie madarakani chama hicho hakijulikani kinafanya nini, kina mipango gani na kina mwelekeo upi? Chama hicho kwa upande wa Bara ni kama kimebemendwa.
CUF inayovuma ni ile ya Zanzibar chini ya Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa chama hicho. Kwa sasa unapozungumzia CUF unazungumzia Zanzibar. CUF ya Bara ipo ziiii!
Sababu ni kwamba, CUF ya Bara baada ya Prof. Lipumba haijapata mbadala, anayeshika mikoba yake hana sifa, uwezo, ubunifu na hata uono wa kisiasa.

CUF ya Bara kwa sasa inajifichwa kwenye kwapa la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). Inategemea huruma ya matamko ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama cha NCCR-Mageuzi ili kusikika.

CUF ya Taslima imepoa, haina harakati kama zile zilizokuwa zikifanywa na Prof. Lipumba. Watendaji wa CUF kwa sasa wanaishi kwa majungu.

Baadhi yao wana fikra finyu kuhusu mwelekeo wa chama hicho. Unapozungumza nao hawaoneshi mwelekeo wa chama hicho, wanachojali ni kwamba ‘wapo huru’.

Prof. Lipumba alijiuzulu Agosti mwaka jana kwa madai kuwa, viongozi wenzake wanne kutoka Ukawa  kumkaribisha ndani ya umoja huo Edward Lowassa na kisha kumteuwa kuwa mgombea wake wa urais.

Na ndipo Taslima akatwaa nafasi hiyo kwa muda. Kinachofanyika ndani ya chama hicho hakieleweki, mwelekeo wa CUF unatia mashaka.

Taslima ana utofauti mkubwa na Prof. Lipumba kwenye siasa za ushindani katika nchi hii, ni kwa kuwa Prof. Lipumba alikuwa na uwezo wa kuchambua na kuandika mambo ya kijamii, kiuchumi na kisasa jambo ambalo halipo kwa kaimu mwenyekiti wa sasa (Taslima).

Prof. Lipumba ana ushawishi mkubwa na kwa watu wengi tofauti na Taslima ambaye mpaka sasa sehemu kubwa ya Watanzania hawamjui, hawajawahi kumuona na pia uwezo wake hauonekani.
Kwa bahati mbaya Magdalena Sakaya, Naibu Katibu Mkuu (Bara) hana uwezo wa kuhuisha harakati za CUF.

Lipo la kujifunza kwa Chadema wakati walipoamua kumtwaa Lowassa ambaye alikuwa amechafuka kutokana na kauli zao za awali.
Tathimni ndani ya Chadema zilionesha kuwa Lowassa bado ‘keki’ kwa taifa. Licha ya baadhi ya viongozi wa chama hicho kutotaka kumpokea lakini alijiunga na chama hicho hivyo kuwa mwiba kwa CCM.

Chadema ilisoma alama za nyakati na kwa kuwa, lengo la siasa ni mafanikio, ilimtwaa Lowassa ambaye mafanikio yake ndani ya Chadema na Ukawa hakuna anayeweza kubeza.
Chadema ilimpoteza Dk. Willibrod Slaa kwa kuwa, thamani yake mbele ya Lowassa ilikuwa ndogo.
Turudi CUF, thamani ya Taslima ni kubwa kuliko Prof. Lipumba katika mazingira ya sasa? Sihitaji jibu.

Bila shaka, uamuzi wa kukurupuka, uliojaa chuki, husda na ujinga uliotamalaki unaweza kuizika CUF.

Pamoja na kutangaza nia ya kuitaka nafasi ya uenyekiti, lakini kwa sasa Taslima sio mtu sahihi kwa nafasi hiyo vinginevyo chama hicho kitakufa kifo cha mende.

Source:Mwanahalisi

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger