Aug 14, 2016

Mbinu Zilizotumika Kusuka Ukuta wa Chadema

Kama Chadema wana mikakati inayoisumbua CCM; inayoisumbua Serikali au inayovisumbua vyama vingine vya siasa, basi kuna mtu nyuma ya pazia anayebuni na kuratibu mipango hiyo.

Mbinu tofauti zilizotumika wakati wa Uchaguzi Mkuu zilizofanya wapinzani waweke ushindani wa kihistoria, mbinu zinazotumika wakati likitokea sakata lolote bungeni na mkakati uliotangazwa hivi karibuni wa kupambana na kile kinachodaiwa kuwa ni ukandamizaji wa demokrasia na kupinga ukiukwaji wa sheria, ni mambo yanayokifanya chama hicho kiendelee kuwa midomoni mwa wananchi.

Si mwenyekiti Freeman Mbowe, mwanasheria mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu wala kiongozi mwingine yeyote anayebuni mipango hiyo peke yake bila ya kumshirikisha ‘mchawi’ huyo.

Ni John Mrema; yule kada aliyekuwa anaendesha mikutano yote ya kampeni za urais za Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka jana. Ndiye mchawi wa mikakati ya Chadema kwa sasa ndani na nje ya Bunge.

Ingawa mgombea wa CCM, John Magufuli aliibuka mshindi kwa kupata kura milioni 8.8, Mrema anaweza kuwa alichangia sehemu kubwa iliyomuwezesha Edward Lowassa kuweka rekodi ya wagombea wa upinzani kwa kupata kura milioni 6.07, takriban mara mbili ya kura walizokuwa wakipata wagombea urais wa upinzani.

Mrema ni kada wa Chadema ambaye alikuwa meneja wa kampeni za urais za Lowassa, ambayo iliundwa na CUF, NCCR-Mageuzi, NLD na chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Ndani ya Chadema, Mrema sasa ni mkurugenzi wa itifaki, mawasiliano, uenezi na mambo ya nje na kabla ya kupewa cheo hicho, alikuwa mkurugenzi wa masuala ya Bunge na Halmashauri.

“Mimi si mchawi, lakini habari za Chadema hazikauki kwenye mitandao na kwenye vyombo vya habari. Nataka muende wenyewe mkafanye utafiti muone jinsi Chadema inavyotawala kwenye mitandao ya kijamii,” alisema Mrema katika mahojiano na Mwananchi yaliyofanyika Ijumaa iliyopita.

“Kazi kubwa tunayofanya ni kuangalia hali ya kisiasa na kuamua kipi kifanyike na wakati upi. Ikiwa ndani ya Bunge unaangalia kuna hoja gani na muibue jambo gani.

“Mimi si intelijensia ya Chadema, bali ninachofanya ni kuibua hoja na kutengeneza ‘issue’ (kadhaa za kibunge ambazo wabunge hutumia kupambana na Serikali.”

Chadema imekuwa ikitumia mbinu tofauti kuhakikisha jina la chama linaendelea kung’aa. Wakati wa Bunge la Katiba, chama hicho na vingine vitatu, vilisusia vikao kwa maelezo kuwa chombo hicho kiliachana na Rasimu ya Katiba iliyotokana na maoni ya wananchi na kuingiza ajenda ya CCM na baadaye kuunda Ukawa.

Wakati wa sakata la uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, chama hicho na vingine vya upinzani vilibadili mbinu. Badala ya kususia vikao, wabunge walisimama ndani ya Bunge kupiga kelele kukwamisha shughuli kuendelea hadi matakwa yao yaliposikilizwa.

Lakini baada ya uongozi wa Bunge kuanza kutumia nguvu ya dola kuwaondoa ukumbini, wabunge wa chama hicho na vingine, sasa wanaingia na mbinu tofauti; wanabeba mabango yenye ujumbe, kususia vikao vinavyoongozwa na Naibu Spika mara baada ya sala ya asubuhi, kuziba midomo au kuvaa nguo nyeusi kufikisha ujumbe wao kwa wananchi.

“Ukiwa mkurugenzi wa Bunge wa chama, lazima uwafanye wabunge wote wawe katika himaya yako,” alisema wakati akizungumzia jinsi Chadema inavyoweka mikakati yake bungeni.

“Na lazima uzipitie hoja zao kabla



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger