Ameyasema hayo Ahamisi hii katika maadhimisho ya miaka 52 jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) eneo la Lugalo ambapo alishiriki usafi na viongozi wa dini mbalimbali katika eneo la jeshi Lugalo.
“Kwahiyo tarehe moja ni tarehe ya upandaji miti katika jiji la Dar es Salaam, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama, jeshi la wananchi, polisi, wahamiaji, magereza,JKT, vitakuwa pamoja nasi na viongozi wetu wa dini tumekaa vikao jana tumeongea, namna gani ambavyo watatusaidia katika makanisa na misikiti kuhakikisha tunapanda miti mingi katika mkoa wetu wa Dar es Salaam, “alisema Makonda.
Aidha Makonda alitoa wito kwa vyombo vya usalama ambavyo vipo kando ya barabara kuhakikisha kuwa vinakuwa mfano katika uboreshaji wa mazingira katika eneo husika.
“Mmefanya kazi kubwa sana naomba niwapongeze, kwa barabara yetu hii ya kutoka Kawe mpaka Mwenge barabara ambayo imekuwa ni mfano na nimeshamuagiza Kamishna Sirro, nataka kuona upande wao kule nako barabara yao inakuwa mfano. Sehemu yoyote ambapo kuna kambi ya Jeshi lakini mbele yao kuna barabara lazima barabara zifanane kama vile mlivyofanya wanajeshi katika barabara kutoka Kawe mpaka Mwenge,” alisema Makonda.
Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
0 [disqus]:
Post a Comment