Sep 5, 2016

Padri Mapunda Akosolewa Vikali Baada ya Kumshukia Rais Magufuli

VIONGOZI WA DINI MSITUMIKE VIBAYA MTABOMOA TAIFA LETU.

Baada ya kusoma gazeti la Tanzania Daima, Toleo NA.4284 la September 5,2016 ninaomba nimkosoe vikali Baba Padri Baptiste Mapunda kwa alichokiongea kanisani akiendesha misa takatifu tarehe 4,September 2016 katika kanisa katoliki la Manzese Dar es salaam.

Baba padri Mapunda aliongea Maneno makali na yasiyofanyiwa utafiti wa kina, na pengine maneno yasiostahiri kusemwa katika mahubiri maana yanaweza kubomoa Taifa letu na kupandikiza chuki miongoni mwa wahumini husika na kuweza kuchukia serikali yao, mfano,padri Mapunda alisema "Rais Magufuli awe na busara na kufuata mwenendo wa Nabii Suleiman....."tafasili yake ni kwamba Mh,Rais wetu hana busara na kama hana busara sisi wote Tanzania tuliomchagua hatuna busara na hii dhahiri kuwa baba Padri anataka tumchukie mh,Rais kwa kisingizio cha kwamba hana busara.

Padri Mapunda anaenda mbali na kusema nina nukuu "wananchi wanalalamika kuongezeka kwa ugumu wa maisha kwa kutokuwa na fedha na kukosekana kwa demokrasia" anamalizia kwa kuhalalisha uongo huu kuwa ukweli kwa kusema nanukuu "Mungu yupo na anayaona mateso ya watanzania".

Ndugu msomaji wangu kama utatafakali hizo nukuu hizo hapo juu utagundua pengine huyu mh,Baba Padri alitakiwa kuwa mwanasiasa ila kakosea kusomea upadri maana anasahau hata maandiko ya Mungu yanayosema "asiyefanya kazi na asile" hakika kuna watanzania wanalalamika kutokuwa na fedha Wakati wakishinda vijiweni, wakishinda wanacheza pulu na wengine hushinda vilabuni na hakuna serikali yeyote inayoweza kumletea mtu pesa mfukoni bila kufanya kazi.

Kuhusu swala la demokrasia, ilipaswa Baba padri useme ni demokrasia ipi wewe unataka na watanzania umesikia wanataka hawana,na mh,Rais kaibana? Je ya kuuza madawa ya kulevya?,ya kuua Tembo?, au ya ufisadi maofsini?. maana haya ndo mh,Magufuli hataki kuyaona na hakika amefanikiwa kuyapiga marufuku nami namuomba aendelee kuyazuia.

Jambo lingine padri Mapunda anasema mh,Magufuli akubali kukosolewa kama mwenyezi Mungu alivyokuwa akikosolewa na Nabii Mussa, nanukuu Maneno yake,naomba nimkumbushe Baba padri kuwa kukosoa ni sahihi wala mh,Magufuli hajasema hapendi kukosolewa lakini siyo kila jambo lazima ukosoe pengine unaweza kukosoa na kisichostahili kwa maslahi ya umma.

Hata Nabii Mussa mwenyewe kitendo chake cha kumkosoa Mungu kwa kila jambo kulimsababishia mauti, akiwa anatoka Misri kuwakomboa wana wa Israel kuelekea katika nchi ya ahadi, na akafa kabla ya kuiona nchi ya ahadi. Kwahiyo sio wote wanaomkosoa Mh,Rais wako sahihi,wengine ni kutaka kujiona jeuri zaidi ya Mh,Rais kwakutofuata sheria,maelekezo na utawala wa sheria kama Nabii Mussa huyo uliyemsema alivyokataa kufuata maelekezo ya mwenyezi Mungu na kuishia pabaya.

Lakini kuna maswali ya kujiuliza hapa kabla ya kuendelea;

1, Je huyu mwandishi wa habari nani aliyemuita kanisani kuja kuchukua hii habari?
2, Na kama hajaitwa yeye alijuaje kuwa Baba padri anaenda kumkosoa mh,Magufuli na yeye kuja kuandika?

3, Na kama kaitwa nani aliyemlipa hiyo pesa? maana kwa uzoefu waandishi wa habari wamekuwa wakilipwa posho pindi wanapoitwa.

4, Je baba padri yeye kama kiongozi wa dini ameomba nafasi ya kuonana na Mh,Magufuli ili amshauri amekosa?

5,Mpasuko aliodai uko nchini hakika una chanzo chake na Chanzo ni Chadema kutangaza maandamano ya nchi nzima, swali Je Chadema ilipotangaza maandamano Padri Mapunda aliwaita na kuwakanya pamoja na kuwapa ushauri? au ndo kutaka umaarufu? Au kapewa pesa na Chadema kuja kuanza chokochoko?

Baada ya kujiuliza maswali hayo utagundua kuna kitu kimejificha katikati, kwasababu haiwezekani Padri Mapunda ainuke na kuhukumu kuwa Mh,Rais ni mbaya na hana busara kabla ya kukaa na hizi pande mbili na kuzihoji, ikumbukwe kuwa chombo pekee cha kuhukumu kuwa nani mbaya kati ya Mh,Magufuli na Chadema ni Mahakama na baada ya kusikiliza pande zote kwakufuata katiba ya nchi ibara ya 13.

Hata mwenyezi Mungu kabla ya kumuhukumu Adam na Hawa aliwasikiliza wote baadae ndo katoa adhabu mbili tofauti; Hawa akaambiwa atazaa kwa uchungu, na Adamu kaambiwa atakula kwa jacho.

Mwisho nimuombe Baba padri Mapunda aige mfano wa Bwana yetu Yesu kristu mpatanishi aliyekuwa aegemei upande wowote katika kuhubiri injiri na wewe baba padri uwe mpatanishi, usiwapotoshe wana kondoo wa Mungu uliyopewa kuwafundisha kwa kuwachochea uhasama dhidi ya serikali yao.

Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema akunyooshee mkono wake wa kuume ewe padri Mapunda upate kuhubiri neno lake na sio siasa.
Imeandaliwa na mhumini wako,
MWITA NYARUKURURU
mwitanyarukururu@gmail.com

Source:Jamii Forums

Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

1 comment:

  1. Nakuunga Mkono Padre Mapunda. Ni shupavu tu ndio wanaosimama. Wengine wote Waoga na wasiwe viongozi.

    ReplyDelete

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger