Sep 11, 2016

Wabunge Wapigilia Msumari Sheria Uhalali wa Mtoto

WABUNGE wametaka mara baada ya kupitishwa Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ya Mwaka 2016 ambao pamoja na mambo mengine utaiwezesha maabara hiyo ifanye uchunguzi unaohusisha matumizi ya teknolojia ya vinasaba, ikiwamo uhalali wa mzazi kwa mtoto, serikali ihakikishe inatunga kanuni mapema na kutenga bajeti ya kutosha ili sheria ianze kazi mara moja.

Wakichangia muswada huo juzi jioni wabunge hao kwa nyakati tofauti walisema muswada huo umekuja kwa wakati na itawezesha Mkemia Mkuu kufanya kazi kwa ufanisi.

Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe (CCM) akichangia muswada huo kwanza alishauri mkemia mkuu apewe muda wa kazi wa miaka mitano hadi 10 ili afanye kazi yake kwa ufanisi.

“Naomba pia serikali sheria hii itakapopita mara moja serikali iweke kanuni ili ianze kazi, tumezoea hapa tunachangia na kupitisha sheria halafu makabrasha yanakwenda kuwekwa kwenye makabati hakuna utekelezaji,” alisema Bashe.

Alitaka pia serikali kutenga bajeti kwa ajili ya maabara ya mkemia mkuu pamoja na kuwalipa wanafunzi wa kemia watakaokuwa wakifika kwa ajili ya mafunzo ya vitendo kabla ya kuhitimu na kuongeza kuwa maabara hiyo ni eneo muhimu la kimkakati nchini.

Mbunge wa Bunda Vijijini, Boniface Getere (CCM) alitaka maabara ya mkemia mkuu ipewe ruzuku ili watu wasio na uwezo wa kulipia vipimo wapimwe bure.

Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi, Jaku Hashim Ayoub (CCM), alisema mkemia mkuu ana majukumu mengi na nyeti hivyo anapaswa kuwekewa bajeti ya kutosha kwa ajili ya kuendesha shughuli zake na kununua vitendea kazi.

“Nchi nzima hii mashine ya ya kupima vinasaba vya binadamu (DNA) iko moja tu na mashine moja ni karibu milioni saba, mimi naona sasa kwa sheria hii mkemia mkuu atakuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa uhuru na ufanisi, aongezewe bajeti, zinunuliwe mashine mpya hata sita haraka,” alisema.

Alisema idadi ya watumishi 192 kwa mkemia mkuu ni ndogo, hivyo waajiriwe haraka watumishi wapya angalau wafike hata 400 ili kuwezesha ofisi ya mkemia mkuu kufanya kazi kwa ufanisi na haraka zaidi.

Katika maoni na ushauri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Mwaka 2016 yaliyowasilishwa na Faustine Ndugulile, ilishauri mara tu baada ya kupitishwa sheria mamlaka iwezeshwe kibajeti ili kuongeza mashine na vitendea kazi vingine ili viendane na kazi na jukumu iliyopewa.

Kamati hiyo pia ilishauri serikali kuhakikisha inatunga kanuni mapema ili sheria iweze kuanza kufanya kazi mapema, lakini pia ilitaka serikali ihakikishe inatoa kibali cha ajira ya watumishi 100 ili mamlaka iwe na watumishi wa kutosha na wenye sifa zinazotakiwa kutekeleza majukumu kwa ufanisi.



Bonyeza Play Hapa Chini Kuona Walichofanya Bilnass na Rosa Ree:
Soma Hizi Habari Zetu Kirahisi Kupitia Application ya Simu ya Udaku Special, Bonyeza HAPA
Share:
Weka Maoni yako Hapa

0 [disqus]:

Post a Comment

Follow Us

Popular Posts

Powered by Blogger.

MKRdezign

Blog Archive

Technology

[blogger]
Contact us
Ajirayako.co.tz
E-mail: ajirayako@gmail.com
DISCLAIMER:
This Website |Ajirayako.co.tz| is Not Affiliated In Any Way
With The Companies Whose Vacancies Are Published Here.
AVOID SCAMS
Never Pay to Have Your CV/Application Pushed Forward. Any job vacancy requesting payment for any reason is a scam.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tags

Abdallah Zombe (3) ACT Wazalendo (7) Afande Sele (6) Afya (42) Air Tanzania (11) Ajali (31) Ajira (16) Akson Tulia (4) Alberto Msando (1) Ali Kiba (10) Almaz Ayana (1) Anna Makinda (2) Anthony Lusekelo (1) Arusha (1) Arusha Felix Ntibenda (1) Asha Rose Migiro (2) Askofu Gwajima (6) ATCL (3) Augustine Lyatonga Mrema (4) Aunty Ezekiel (2) Babu Tale (2) Bajeti (1) Bakwata (3) Baletol (1) Bandari (3) Baraka da Prince (2) Bavicha (1) Benjamin Mkapa (1) Benki Kuu Tanzania (1) Bernad Membe (1) Biashara (1) Bodi ya Mikopo (1) Bongo Movies (7) BOT (1) Breaking News (3) Buhari (1) Bungeni (48) Burudani (45) CCM (5) Chadema (20) Charles Kitwanga (3) Chibok (1) Chid Benz (2) Chris Brown (3) Clouds FM (1) CUF (26) Dangote (3) Daniel Ole Njolay (1) Dart (2) David Kafulila (7) Desmond Tutu (2) Diamond Platnumz (18) DJ Fetty (1) Dk. Reginald Mengi (1) Donald Trump (23) Dr Mwaka (1) Dr Mwaka Aacha Vilio Kwa Wagonjwa...Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Septemba 30 (1) DR Shein (2) Dr Slaa (4) Dr. Ramadhan Kitwana Dau (1) Edo Kumwembe (1) Edward Lowassa (30) Elimu (75) EPA (1) Escrow (3) Ester Bulaya (9) Faiza Ally (1) Fast Jet (1) Featured (3) Flaviana Matata (1) Freeman Mbowe (31) Fumanizi (1) Gadner (1) George Masaju Masaju (1) Gerald Hando (1) Godbless Lema (31) Godwin Gondwe (1) Halima Mdee (2) Hamad Rashid (1) Harmonize (3) Hillary Clinton (3) Iddi Amini Dadaa (1) Idriss Sultan (2) Iphone (1) Irene Uwoya (1) Ivo Mapunda (1) Jack Wolper (3) Jaji Francis Mutungi (3) Jakaya Kikwete (13) Jambazi (2) James Mbatia (1) January Makamba (1) JB (1) Jecha Salim (1) Jenerali Ulimwengu (1) Jerry Muro (3) Jeshi la Polisi (32) Jobs (1) John Cheyo (1) John Mnyika (3) John Pombe Magufuli (83) Joseph Kabila (2) Josephine Mshumbushi (1) Joshua Nassari (1) Julieth Kairuki (1) Julius Mtatiro (9) Jussa (1) Kamanda Sirro (1) Kenyan News (14) KFC (1) Kicheko (1) Kigwangalla (1) Kilimo (1) Kinana (3) Kitanzi (1) Koffi Olomide (2) Korea (1) Kuliko Jana (1) Leicester City (1) Livingstone Lusinde (1) Lugumi (1) Lulu Michael (1) Maajabu (3) Maalim Seif (14) Madam Rita (1) Madawa ya Kulevya (7) Magazeti (49) Mahakamani (7) Mai Mai (4) Maisha (2) Majambazi (7) Makahaba (1) Makalio Makubwa (1) Makamba (1) Malaika (1) Malezi (1) Mama Salma (1) Man Fongo (2) Man United (1) Mange Kimambi (2) Manji (7) mape (1) Mapenzi (76) Marcus Rashford (1) Mashine ya MRI (1) Matiko (1) Matokeo (3) Mauaji (31) Mauji (2) Mbeya (2) Mbunge Lusinde (1) Mbwana Samatta (8) Mchungaji Anthony Lusekelo (1) Meya wa Kinondoni (1) Michael Shirima (1) Michez (1) Michezo (201) Miss Tanzania (2) Mizengo Pinda (1) Mongela (1) Mr Blue (3) Mrema (7) Mrisho Gambo (3) Mrisho Mpoto (2) Msigwa (2) Mugabe (1) Museven (1) Music (85) Muungano (1) Mwakyembe (2) Mwanafunzi (3) Mwendokasi (1) Mwigulu Nchemba (2) Nape Nnauye (13) Navy Kenzo (1) Nay wa Mitego (2) Ndanda FC (1) Ndugai (1) Necta (3) Nida (1) Nigeria (2) NSSF (1) Nuh Mziwanda (2) Nyerere (1) Obama (9) Ommy Dimpoz (2) Original Comedy (2) Oscar Pistorius (1) Paul Makonda (34) Paul Pogba (2) Pep Guardiola (1) Peter Msigwa (4) Petitman (1) Polisi (4) Pombe (1) Pride (1) Prof Mkumbo (2) Prof. Benno Ndulu (1) Prof. Ibrahim Lipumba (12) Prof. Lipumba (23) Prof. Tibaijuka (3) Profesa Benno Ndulu. (1) Profesa Muhongo (3) Q-Chief (1) Raila Odinga (2) Rais Magufuli (35) Ray C (1) Reginald Mengi (2) Rihanna (1) Robert Mugabe (4) Ruby (5) Rushwa (3) Sadaka (1) Saed Kubenea (3) Saida Karoli (2) Salama Jabir (1) Salum Mwalimu (2) Samia Suluhu (1) Samsung Galaxy (1) Samwel Sitta (5) Sauti Sol (1) SBL (1) Scorpion (3) Serengeti Boys (1) Shamsa Ford (2) Sheikh Abubakar Zubeiry (2) Shibuda (2) Shilole (1) Siasa (1945) Siasa Huru App (3) Siasa za Kenya (1) Simba (1) Slaa (1) Snura (1) South Africa (1) Sudan (1) Sugu (1) Sukari (4) Sumaye (8) Supu ya Pweza (1) Tanesco (9) Tanzia (22) TB Joshua (4) TBS (1) TCRA (5) TCU (4) Technology (3) Tetemeko (13) TFDA (1) Thereza May (1) Thomas Mashali (1) TRA (4) Tundu Lisu (20) Tyrant (1) Ubakaji (4) Uchambuzi (1) Uchawi (1) Uchumi (90) Udaku (46) Udaku Spesho (21) UDSM (1) Ufisadi (2) Ugaidi (6) Uhuru Kenyatta (2) Ujambazi (4) Ujauzito (1) Ukahaba (1) Ukatili (1) Ukawa (11) Ukuta (11) Ummy Mwalimu (1) Urembo (15) Ushirikina (1) Utafiti (2) Utapeli (3) UVCCM (4) Vioja (1) Wastara (1) Watumishi Hewa (1) Waziri Mahiga (2) Waziri Mkuu Majaliwa (18) Wema Sepetu (6) Wiliam Lukuvi (6) Yanga (7) Yaya Toure (1) Zitto Kabwe (33) Zuckerberg Mark (1)

Categories

Advertisement

Main Ad

Facebook

Responsive Ads Here

Featured

Recent

Udaku Special Test

Copyright © Udaku Special Test | Powered by Blogger